Je, ripoti ya ajali ya ndege ya Precision Air, itawekwa hadharani au itafichwa "kabatini" kama tulivyozoea ripoti nyingine za nyuma?

Je, ripoti ya ajali ya ndege ya Precision Air, itawekwa hadharani au itafichwa "kabatini" kama tulivyozoea ripoti nyingine za nyuma?

Mystery

JF-Expert Member
Joined
Mar 8, 2012
Posts
15,843
Reaction score
31,057
Ni kawaida kwa nchi hii, watawala wetu kutuambia wameunda Tume kuchunguza matukio mbalimbali yanayotokea ya ajali, lakini Tume hizo zinapokamilisha Kazi zake na kukabidhi kwa watawala, huwa hazisomwi kwa Umma na badala yake, zinafichwa!

Nieleze kwa kutoa mifano michache, iliundwa Tume ya kuchunguza ajali ya moto, Katika soko la Kariakoo, jijini Dar mwezi July mwaka jana na Tume hiyo ikakamilisha Kazi yake na kuikabidhi kwa Serikali, lakini hadi hivi leo, ripoti hiyo imefichwa kabatini na imekuwa SIRI, Ili wananchi tusijue nini kilitokea!

Ripoti nyingine iliyofichwa "kabatini" baada ya Tume iliyoundwa kukamilisha Kazi yake ni ya Mauaji ya mfanyibiashara wa madini huko Mtwara, Mussa Hamisi, aliyeuawa na Polisi na baadaye kumpora pesa zake zake za madini, kiasi cha shilingi milioni 70, ambapo Tume hiyo iliundwa mwezi February mwaka huu, ambapo hadi leo hii, ripoti hiyo nayo imefichwa na wananchi hatujaelezwa nini kilibainika Katika ripoti hiyo!

Kwa hiyo ndiyo maana wananchi tunakuwa na shauku, pamoja na kauli hiyo ya Serikali, kuwa ripoti hiyo ya ajali ya ndege, itakuwa tayari ndani ya siku 14, tokea ndege hiyo ilipopata ajali tarehe 6 mwezi huu, je ripoti hiyo itatolewa kwa Umma wa watanzania, au ndiyo kama kawaida ya Serikali hii ya CCM, kuamua kuificha, Ili isijulikane kwa Umma wa watanzania, kama walivyozoea?

Ifahamike kuwa Umma wa watanzania una Haki ya kujua nini kilitokea siku hiyo ya ajali, kwa kuwa wanaamini kuwa kulikuwa na uzembe wa hali ya juu, wa vikosi vya uokoaji Katika ajali hiyo ya ndege, hadi kusababisha vifo vya watu 19, na Ili dhana hiyo itoweke vichwani mwa watu, ni LAZIMA ripoti hiyo itolewe hadharani kama ilivyoahidiwa na Serikali.

Ndiyo maana wengi tumeshuhudia, yule Kijana mvuvi, Jackson Majaliwa, akipewa "promo" kubwa baada ya kubainika kuwa yeye ndiye aliyekuwa shujaa siku hiyo, baada ya kuuvunja mlango wa ndege, kwa kutumia Kasia ya mtumbwi wake na hivyo kunusuru Maisha ya watanzania 26 waliokuwemo ndani ya ndege hiyo.

Mungu ibariki Tanzania
 
Sitegemei jipya zaidi ya niliyokwisha sikia! Labda wake wachunguzi huru toka nje ya nchi na waruhusiwe kufanya kazi yao kwa weledi
 
Sitegemei jipya zaidi ya niliyokwisha sikia! Labda wake wachunguzi huru toka nje ya nchi na waruhusiwe kufanya kazi yao kwa weledi
Huo uliouleza Mshana Jr ndiyo utofauti Kati ya Tume za huko siku za nyuma na hii ripoti ya safari hii, kwa kuwa ripoti ya safari hii inaundwa na Tume huru ya watengenezaji wa ndege yenyewe ya Precision Air kutoka Ufaransa.

Kama Tume hiyo haitaingiliwa na watawala, basi Umma wa watanzania tutegemee ripoti iliyo huru na itakayotolewa kwa Umma wa watanzania na Dunia kuwa ujumla, Katika siku chache zijazo
 
Cha msingi ni kuchukua hatua kabla ya Majanga kutokea na kujifunza kutoka a na Majanga ambayo yameshatokea, na waliopewa dhamana kukubali kuwajibika hata kinafki tu angalau intosha
 
Hiyo ripoti naona inaweza kutolewa kwasababu haionekani kama imegusa moja kwa moja maslahi ya vigogo wa CCM na serikali yake.

Swali ni kwamba, Je, itakuja na majibu sahihi ya maswali yaliyotokana na ajali ile? hala ndipo pa kutazama kwa makini.

Binafsi, naona kama wanaweza kuja na ripoti itakayokwepesha baadhi ya mambo ya msingi, ili kuwaondolea lawama wale walioonekana kuzembea ilipotokea ajali ile.

Zaidi, naona ripoti itasema wahanga wa ajali ile walipwe fidia jambo ambalo tayari mamlaka husika imeshalitolea ufafanuzi kwamba wanajiandaa kufanya hivyo, na huo ndio utakuwa mwisho wa habari.
 
Hiyo ripoti naona inaweza kutolewa kwasababu haionekani kama imegusa moja kwa moja maslahi ya vigogo wa CCM na serikali yake.

Swali ni kwamba, Je, itakuja na majibu sahihi ya maswali yaliyotokana na ajali ile? hala ndipo pa kutazama kwa makini.

Binafsi, naona kama wanaweza kuja na ripoti itakayokwepesha baadhi ya mambo ya msingi, ili kuwaondolea lawama wale walioonekana kuzembea ilipotokea ajali ile.

Zaidi, naona ripoti itasema wahanga wa ajali ile walipwe fidia jambo ambalo tayari mamlaka husika imeshalitolea ufafanuzi kwamba wanajiandaa kufanya hivyo, na huo ndio utakuwa mwisho wa habari.
Lakini nadhani ripoti hii, itakuwa tofauti na ripoti zingine za nyuma, kwa sababu inahusisha na wachunguzi wengine wa nje, ambao ni watengenezaji wa ndege hiyo ya Precision Air.

Kwa hiyo nadhani, haitokuwa na kukwepesha mambo, itakuwa ya kueleza ukweli zaidi.

Kama vyombo vya uokoaji, vilizembea wakati wa uokoaji, Tume hiyo itaeleza hivyo, kutakuwa hakuna kuficha ficha mambo, kwa lengo tu la kuwalinda baadhi ya vigogo serikalini
 
Ni kawaida kwa nchi hii, watawala wetu kutuambia wameunda Tume kuchunguza matukio mbalimbali yanayotokea ya ajali, lakini Tume hizo zinapokamilisha Kazi zake na kukabidhi kwa watawala, huwa hazisomwi kwa Umma na badala yake, zinafichwa!
kama hujui kitu unyamaze repoti ya ajali hiyo ya ndege serikali haina mamlaka nayo, itachunguzwa na kuwekwa hadharani
 
Lakini nadhani ripoti hii, itakuwa tofauti na ripoti zingine za nyuma, kwa sababu inahusisha na wachunguzi wengine wa nje, ambao ni watengenezaji wa ndege hiyo ya Precision Air.

Kwa hiyo nadhani, haitokuwa na kukwepesha mambo, itakuwa ya kueleza ukweli zaidi.

Kama vyombo vya uokoaji, vilizembea wakati wa uokoaji, Tume hiyo itaeleza hivyo, kutakuwa hakuna kuficha ficha mambo, kwa lengo tu la kuwalinda baadhi ya vigogo serikalini
Nijuavyo, kuficha mambo kupo kwenye DNA yetu, na hii ndio sababu matatizo huwa hayatuishi kwasababu tuna tabia ya kuyaficha badala ya kuyafanyia kazi kwa kuyatafutia solution, hivyo hata hii ripoti kwangu sioni kama itakuwa na tofauti.

Anyway, let's wait and see!.
 
Back
Top Bottom