Je, samaki anatapika watoto, anazaa au anataga mayai?

Je, samaki anatapika watoto, anazaa au anataga mayai?

secretarybird

JF-Expert Member
Joined
Aug 22, 2024
Posts
2,998
Reaction score
4,948
Leo mchana katika pita pita nilikuta watu katika mtaa mmoja wanabishana kuhusiana namna ambavyo samaki hupata watoto au vifaranga kama watu wengine wanavyodai. Katika mjadala huo kulikuwa na baadhi ya watu waliodai kuwa samaki anazaa watoto na kulikuwa na wengine waliodai kuwa samaki ana taga mayai. Ubishi ulichukua takribani dakika 45 bila suluhu na Kwa kuwa mimi biology niliacha kuisoma tangu nilipokuwa form one nilibaki njiapanda.

Mungu si Athumani alijitokeza mwalimu mmoja wa shule ya sekondari iliyopo katika mtaa ule na Kwa bahati nzuri alikuwa mwalimu wa biology. Tukamwita huku tukidhani kuwa ana jibu lililo sahihi, tulipomwuliza swali hilo alitabasamamu kidogo na kuanza kushusha nondo, akasema.

"Samaki anatapika watoto au Kwa lugha nyepesi anatema watoto, hii ni Kwa sababu samaki haendi nje ya maji kama mamba, hivyo inamuwia vigumi kutaga majini, isitoshe samaki hana uke na wote hapa ni mashahidi katika hilo labda kama Kuna mtu amewahi kuona uke wa samaki atuambie. Ukiachilia mbali taalima yangu ya ualimu, baba yangu ni mvuvi kule Kanda ya ziwa, tulishavua samaki tukakuta midimoni mwao wana watoto wengi so samaki anatema watoto tumeelewana! "

Mi nilifikiri Kwa sekunde kadhaa nikamwambia Kwa hiyo kama samaki hawana uke wanawezaje kujamiiana hadi wakapata mimba? Mwalimu kusikia hilo swali akajifanya amepigiwa simu ya dharura, akasogea pembeni kidogo, mara huyoooo! katokomea. Kwa kweli waalimu wa TZ ni bongolala Wala tusiwaani.
 
Samaki wana uke. Ninachojua huwa wanataga mayai na kuya release kwenye maji ambapo vifaranga vitakua kivyao bila uangalizi
 
mouthbreeder, any fish that breeds its young in the mouth. Examples include certain catfishes, cichlids, and cardinal fishes. The male of the sea catfish Galeichthys felis places up to 50 fertilized eggs in its mouth and retains them until they are hatched and the young are two or more weeks old.
 
Muwe mnapita haraka haraka.

JIBU:

Samaki wanazaliana kwa style nyingi kuu ikiwa ni mayai, kuzaa, au kwa njia ya mdomo (kuweka mayai mdomoni) etc
Kwa hiyo hao wanaozaliana Kwa njia ya mdomo ndo wale ambao hawana uke hivyo wanafanya mapenzi/ kunyanduana Kwa njia ya mdomo siyo.
 
Kutaga, kutapika na kuzaa yote ni majibu sahihi inategemea na aina ya samaki.
 
Leo mchana katika pita pita nilikuta watu katika mtaa mmoja wanabishana kuhusiana namna ambavyo samaki hupata watoto au vifaranga kama watu wengine wanavyodai. Katika mjadala huo kulikuwa na baadhi ya watu waliodai kuwa samaki anazaa watoto na kulikuwa na wengine waliodai kuwa samaki ana taga mayai. Ubishi ulichukua takribani dakika 45 bila suluhu na Kwa kuwa mimi biology niliacha kuisoma tangu nilipokuwa form one nilibaki njiapanda.

Mungu si Athumani alijitokeza mwalimu mmoja wa shule ya sekondari iliyopo katika mtaa ule na Kwa bahati nzuri alikuwa mwalimu wa biology. Tukamwita huku tukidhani kuwa ana jibu lililo sahihi, tulipomwuliza swali hilo alitabasamamu kidogo na kuanza kushusha nondo, akasema.

"Samaki anatapika watoto au Kwa lugha nyepesi anatema watoto, hii ni Kwa sababu samaki haendi nje ya maji kama mamba, hivyo inamuwia vigumi kutaga majini, isitoshe samaki hana uke na wote hapa ni mashahidi katika hilo labda kama Kuna mtu amewahi kuona uke wa samaki atuambie. Ukiachilia mbali taalima yangu ya ualimu, baba yangu ni mvuvi kule Kanda ya ziwa, tulishavua samaki tukakuta midimoni mwao wana watoto wengi so samaki anatema watoto tumeelewana! "

Mi nilifikiri Kwa sekunde kadhaa nikamwambia Kwa hiyo kama samaki hawana uke wanawezaje kujamiiana hadi wakapata mimba? Mwalimu kusikia hilo swali akajifanya amepigiwa simu ya dharura, akasogea pembeni kidogo, mara huyoooo! katokomea. Kwa kweli waalimu wa TZ ni bongolala Wala tusiwaani.
Kule ni kuzaa sio kutapika
 
Leo mchana katika pita pita nilikuta watu katika mtaa mmoja wanabishana kuhusiana namna ambavyo samaki hupata watoto au vifaranga kama watu wengine wanavyodai. Katika mjadala huo kulikuwa na baadhi ya watu waliodai kuwa samaki anazaa watoto na kulikuwa na wengine waliodai kuwa samaki ana taga mayai. Ubishi ulichukua takribani dakika 45 bila suluhu na Kwa kuwa mimi biology niliacha kuisoma tangu nilipokuwa form one nilibaki njiapanda.
Waende SUA kuna Prof mmoja anafuga sana samaki na anafundisha mambo mengi kuhusu samaki, watajionea maajabu mengi pale
 
Samaki anataga mayai kama kawaida then anayaweka mdomoni sijui ndo yapate joto afu baada ya hapo anayatema yakiwa tayari,nilifuga samaki nikiwa mdogo na mwalimu wangu(teacher Mikidadi) pia alinifundisha hivyo
 
Eti mwalimu mzima wa biology na degree yake anasema samaki hana uke🤣🤣🤣🤣 bongo bahati mbaya karibu Sudan kusini.
 
Back
Top Bottom