Je, Sancho ndio suluhisho la matatizo ya Man United?

Je, Sancho ndio suluhisho la matatizo ya Man United?

Yohimbine

JF-Expert Member
Joined
Jan 6, 2019
Posts
873
Reaction score
1,841
Wakati dirisha la usajili likikaribia kufungwa huko barani ulaya kumekuwa na habari mbalimbali zikiendelea lakini kubwa ni winga wa Borrusia Dortmund Jadon Sancho akihusishwa na kujiunga Manchester United.Msimu uliopita ulikua ni msimu mzuri sana kwa Jadon Sancho kwani aliweza kufunga magoli 17 katika Bundesliga na kutoa assist 11 lakini ukiangalia aina ya mpira wanaocheza man united kuna wachezaji wengi wa aina yake mfano rashford na martial kwani wote wana wana kasi nzuri ya kuendana na mchezo.

Tatizo la man united naliona lipo katika namba tisa ya nguvu mfano Harry Kane mtu mwenye uchu wa kuliona goli kwani man united wanapoteza nafasi nyingi sana za kufunga hasahasa rashford na martial.Tatizo la pili ni mabeki wa pembeni ,Wan Bissaka amekua ni mzuri sana katika kukaba lakini akiwa na mpira anakosa ubunifu anashindwa kuwa beki wa kisasa kama alfonso davies au trent alexander anorld hivyo solkjaer anapaswa kuliangalia tatizo ili kwa namna tofauti.

Mwisho kabisa ni pale kwenye beki wa katikati baina ya Maghuire na Lindelof wamekuaa hawana muunganiko mzuri kiuchezaji kwa kufanya makosa mengi yanayogharimu timu ndio maana mpaka sasa katika mechi 2 wamesharuhusu mabao matano ,Eric Baily ni beki mzui sana pale united tatizo ni majeruhi tu ndo yanamsumbua kama akiwa fiti na maghuire basi safu ya ulinzi itakua bora sana .Haya ni maoni yangu tu wewe kama mwanamichezo una mawazo gani?

I stand to be corrected
 
Hiyo namba 7 mpe hata Bissaka, mbona anaweza shughuli za mawinga, 2 pale mpe Dalot ..hili gari bovu lakini lina matairi litaenda tuu😂
 
Hii timu hii, wameshapita waalimu wengi wenye falsafa tofauti tofauti, wengi wakijaribu kumkosoa Fergie au kutaka kuuaminisha ulimwengu wa soccer kuwa mfumo wa kiuchezaji unaweza kubadilika kwa vyovyote vile.

Martial, Rashford, Jesse, Greenwood, James, ni wachezaji lakini si wa kiwango cha Utd. Bruno, Pogba, Matic, Mata, Mctommnay, Maguire, Dalot, Shaw, Wanbissacka, Lindeleof, Van Beek, Fred hawa wana kiwango cha UTD na wanafaa wakichezeshwa kwa nafasi wanazoziweza vyema.

Ila uwezo wa Ole pia unanitia shaka, kudhani Pogba anaweza kucheza dimbani kwa kuwa ni mrefu, naona anachemsha sana. Ulinzi ni Matic, Mctommnay, Maguire, hawa ndo walinzi pekee wa ndani Baily huwezi kumuhesabu, aachane na mpira tu, huwezi kucheza mechi 1 kisha unakaa majeruhi miezi 3, ukirudi tena mechi 1, majeruhi miezi 6.

Atafute goal getter, namba 6, 4, 5 wa nguvu, 7 na 11 wa uhakika, na hii ni shughuli ya angalau nusu msimu.
 
Hii timu hii, wameshapita waalimu wengi wenye falsafa tofauti tofauti, wengi wakijaribu kumkosoa Fergie au kutaka kuuaminisha ulimwengu wa soccer kuwa mfumo wa kiuchezaji unaweza kubadilika kwa vyovyote vile...
wachezaji wa kiwango cha united kwa huko mbele ni wepi? United ilikua na wachezaji wa kawaida tangu enzi na enzi, ni umoja tu wa kuifanya iwe timu ndo ulioiwezesha kushinda vikombe. Valencia na Young ndo walikua attacking wings wa Fergie kikombe chake cha mwisho.
 
wachezaji wa kiwango cha united kwa huko mbele ni wepi? United ilikua na wachezaji wa kawaida tangu enzi na enzi, ni umoja tu wa kuifanya iwe timu ndo ulioiwezesha kushinda vikombe. Valencia na Young ndo walikua attacking wings wa Fergie kikombe chake cha mwisho.
Ni kweli kabisaa, unaikumbuka falsafa ya mzee lakini? Wakati wakongwe walioizoea ligi, jua linapoanza kuzama, wanachukuliwa madogo kupewa uzoefu, wanaita succession plan. Kumbuka warithi wa akina Keane na Scholes walikuwa wakina nani na walianzaje kupewa nafasi. Usisahau Smalling na Jones walianzaje kupewa nafasi, usisahau Fletcher hakuwa na nafasi lakini mzee ndio alifanya yote.

Ila ukisema Scholes, Keane, CR7, Giggs, Cantona, Rooney, Rio, Evra, Wes, Nemanja, Ole, Yorke, Cole, Van Persie, Hargreaves, Owen, Chadwick, Chicharito, Tevez, Carrick n.k walikuwa ni wachezaji wa kawaida sana, basi wachezaji wazuri bado hawajazaliwa na hawatakaa watokee.

Kwa kikosi kile kile alichokiacha Mzee kikiwa kinapambania vikombe, walimu wangapi wameshindwa kukitumia? Leceister alipambana na vikosi vyenye thamani mara 3 zaidi yake, na wakabeba ndoo, Spurs je? Msimu huu, ziangalie Everton, Leeds, Crystal, wana jambo lao hao...halafu uje na hiyo dhana ya wachezaji wa kawaida mwishoni mwa msimu
 
Back
Top Bottom