Habari wakuu!
Kama mada inavyosomeka hapo juu,wamiliki wa nyumba za biashara pamoja na watu walioko kwenye fani mbalimbali za ufundi wakiongozwa na mafundi ujenzi ni makundi yanayopata vipato vya uhakika zaidi ya 170,000 kwa wastani kwa mwezi lakini hawalipi kodi ya mapato
Kwani serikali wanakwama wapi kuwafanya hao watu wakate leseni ya biashara/kazi zao? Kuliko kusumbua wamama na vijana wauza karanga na mbogamboga kwa kukata kitambulisho cha mjasiriamali ilifaa makundi hayo hapo juu yawe na leseni za kazi zao
Viongozi wa mitaa wahakikishe kila nyumba ya kupangisha mmiliki ana leseni na ionekane kwenye mkataba wa wapangaji.Pili kila ujenzi unaofanywa ni lazima fundi awe na leseni ya kazi husika.
Nawasilisha