Je serikali kutokumlipa mshahara mwalimu mwenye masters ya ualimu ni sawa?

Je serikali kutokumlipa mshahara mwalimu mwenye masters ya ualimu ni sawa?

NJALI

JF-Expert Member
Joined
Jan 9, 2014
Posts
1,534
Reaction score
1,090
Jamani wanajanvi, sioni kama ni mantiki kumruhusu mtumishi akajiendeleze kwa kuchukua shahada ya pili ya ualimu kisha akirejea kazini serikali inashindwa kumlipa mshahara wa masters. Hii inawavunja moyo walimu wenye nia ya kujiendeleza kitaaluma. Hii ni kwa walimu wa s/msingi na s/sekondari. Vyuo vikuu hawahusiki, pia diploma na grade A teachers sijui ndio maana sijazungumzia. Nawasilisha.
 
Binafsi nnafaham kuwa mshahara umepangwa mwisho degree baada ya hapo ni malupulupu tu ndio utapata (i mean ukiwa na masters post nyingi sana zitakuhitaji)
 
Ni sawa,UALIMU ni wito.

Sent from my BlackBerry 9700 using JamiiForums
 
Tumekuwa tukilalamika kwamba walimu wa tz hawana motivation hata kidogo,hii si haki kwa walimu wetu.poor system utumishi wa umma.
 
Kwa Kawaida Kuna Kitu Ambacho Kinaitwa Cheo Na Kingine Wadhifa,unapoenda Kusoma Unaweza Ukapanda Vyote Au Kimoja Mara Unapofanyiwa Recategozization .ila Kwa Serikali Shahada Ya Kwanza Inakuwezesha Kushika Nafasi /Na Cheo Na Madaraka Yeyote Katika Utumishi Wa Umma Kasoro Vyuoni Hasa Vyuo Vikuu.unapoongeza Masta Unapata Bar Increment Ambayo Inapanda Hata Kwa Experience Pasipo Shule Kuongeza, We Wa Masta kitakochukusaidia Ni Madaraka (wadhifa) Km Utapata Na Inategemea Nafasi Km Iyo Ipo Ktk Sekta Yako,PIA WARAKA WA UTUMISHI UMESHAURI PIA INAWEZA IKAGOMBEWA NA PIA WA SHAHADA ya awali AKAPITA WE UKAKOsA myenye shahada ya uzamili MARA BAADA YA INTAVYUU Husika.
 
Ni sawa,UALIMU ni wito.

Sent from my BlackBerry 9700 using JamiiForums

hakuna cha wito wala nin wacha kuropoka kama umekunywa uji wa magimbi,,,,ualimu ni kazi kama kazi nyngne!!!!
 
Serikali waliangaliye hili la sivyo walimu wengi watashindwa kujiendeleza au wataacha ualimu na kwenda field zingine kwa sababu hivi kuna ugumu gani mwalimu wakijiendeleza na kupata masters kupewa bar moja ya mshahara? Kwa ukweli ina bore sana hakuna marupurupu yoyote ndo kwanza ukipata masters unatengeneza ugomvi na madeo wasiokuwa na elimu hiyo na unakuwa punished kwa kupelekwa maeneo ambayo yanakuwa tofauti na elimu yako. Wito chama cha walimu, TSD, na TAMISEMI muliangalie sana hili.
 
Jamani ifike mahala tuwe wamoja katika kudai haki zetu za msingi. Kwa kada zingine kama uhasibu, polisi,afya mambo yakoje kwa mtu mwenye masters? Inahesabika au hawaihesabu katika mshahara na marupurupu? Kama wanaitambua why not to teachers?
 
Binafsi nnafaham kuwa mshahara umepangwa mwisho degree baada ya hapo ni malupulupu tu ndio utapata (i mean ukiwa na masters post nyingi sana zitakuhitaji)

Hahahah labda kwa EDUCATION! Mfano mshahara wa HAKIMU MWENYE DEGREE ni 700,000/ ,kuna tena posho ya nyumba na mavazi, HAKIMU MWENYE MASTERS ni 1,500,000/=, na posho ya nyumba na mavazi , binafsi naunga mko kuwapa mshahara sawa MWENYE DEGREE MOJA NA MASTERS sababu hamna kipya alichoongeza kwenye masters yake
 
Jamani ifike mahala tuwe wamoja katika kudai haki zetu za msingi. Kwa kada zingine kama uhasibu, polisi,afya mambo yakoje kwa mtu mwenye masters? Inahesabika au hawaihesabu katika mshahara na marupurupu? Kama wanaitambua why not to teachers?

Kwa fani zetu wengine na hasa tulio katika sekta binafsi, mtu unasoma Masters ili ikusaidie kuongeza ufanisi katika kazi yako. Kitakachokuongezea masilahi ni ufanisi mkubwa wa utendaji na si Masters. Iwapo mwenye degree ya kwanza ana ufanisi zaidi yako mwenye Masters nafasi ya kumzidi masilahi inakuwa finyu. Hivyo isiwe kusoma tu, bali kutumia kisomo kwa kuongeza tija.
 
Serikali waliangaliye hili la sivyo walimu wengi watashindwa kujiendeleza au wataacha ualimu na kwenda field zingine kwa sababu hivi kuna ugumu gani mwalimu wakijiendeleza na kupata masters kupewa bar moja ya mshahara? Kwa ukweli ina bore sana hakuna marupurupu yoyote ndo kwanza ukipata masters unatengeneza ugomvi na madeo wasiokuwa na elimu hiyo na unakuwa punished kwa kupelekwa maeneo ambayo yanakuwa tofauti na elimu yako. Wito chama cha walimu, TSD, na TAMISEMI muliangalie sana hili.

Waalim maneno mengi, lini mtachukua hatua?hizi nyaraka kandamizi kila siku zinatolewa lakini mnaishia kulalamika tuuuuuu(mimi pia ni mwalim kitaaluma ila sifanyi kazi ya ualim)
 
Hahahah labda kwa EDUCATION! Mfano mshahara wa HAKIMU MWENYE DEGREE ni 700,000/ ,kuna tena posho ya nyumba na mavazi, HAKIMU MWENYE MASTERS ni 1,500,000/=, na posho ya nyumba na mavazi , binafsi naunga mko kuwapa mshahara sawa MWENYE DEGREE MOJA NA MASTERS sababu hamna kipya alichoongeza kwenye masters yake

tumia akili cyo unaropoka tu kama huna cha kuongea acha wanaume waongee
 
ni sawa,ualimu ni wito.

Sent from my blackberry 9700 using jamiiforums

ni wito kivipi? Kwani mwalimu akienda bucha kununua nyama anapunguziwa bei kwasababu ni mwalimu? U
 
Mwalimu anapasaswa azingatie anatoa matokeo gani na si kuja na vyeti akataka mshahara upande. Swali la kujiuliza mwalimu anasoma ili aongeze ujuzi au aongeze mshahara.
 
Yani ualimu ulishalaaniwa kwani km Waalimu wa sayansi wanalipwa sawa na walimu wa masomo ya sanaa hili ni janga
 
Pia Kusoma Ni Haki Ya Mtumishi Kwa Mujibu Wa Waraka Wa Utumish Ila Ukisoma(specialize) Eneo Ambalo Mwajili Haitaji Waraka Haumlazimishi Kukupandisha Ila Analazimishwa Kujua Kua Umerud Kazin !na Kutokana Na Mahitaji Anaweza Kukupangia Kazi Ile Ambayo Awali Ulikua Unafanya Au Kukubadilipia Mahakama Na Bunge Ni Mihimili Mengine Hivyo Si Lazima Kila Circular Inayotoka Iwahusu Na Wao!so Kabla Hujasoma Mtumishi Wa Uma Hasa Ambaye Anatoka Nje Ya Mihimili Ya Mahakama Na Bunge Pitia Nyaraka Muhim Km Miongozo, Kanuni ,Circular,gvt Notes,sheria Ilokuajili,standing Order,gvt Gazzete Nk Ili Ujue Unapoamua Kwenda Shule Km Lengo Upande Cheo Na Mshahara Ujue Mapemaaa Ila Km Unasoma Kwa Faida Yako Haina Haja Na Ndo Mana WANAPOKUA NA MAHITAJI WANASOMESHA Ila Km Unaiitaji Ww Unajisomesha
 
Mimi mtu mwenye DEGREE YA EDUCATION namuona kama mwanafunzi wa form6 wa mzumbe au ilboru tena anaweza akamzidi mwalimu mwenye DEGREE

ulisha isoma degree ya education? Au unaropoka kutafuta umaarufu? Kozi ambayo hujasoma huwezi jua inaugumu au faida gani.
 
Back
Top Bottom