Je tamaduni za wamasai na wahadzabe ziko juu ya sheria?

Je tamaduni za wamasai na wahadzabe ziko juu ya sheria?

Lyetu

JF-Expert Member
Joined
Feb 11, 2018
Posts
1,268
Reaction score
3,429
Mama wa watoto kadhaa anahukumiwa zaidi ya miaka 20 kwa kukutwa na nyamapori kilomoja, ila kuna kundi la watu linafanya uwindaji haramu kwa kuua mamia ya wanyamapori kwa kisingizio cha tamaduni.

Ufugaji wa ng'ombe wa kienyeji umekuwa kama uharifu nchini kwa asilimia kubwa ya wafugaji, mifugo yao inataifishwa na kupigwa mnada, ila kuna kundi limeachiwa pori lifuge mifugo kwa uhuru na wakitaka kuamishwa wanajengewa na nyumba kwa kisingizio cha tamaduni.

Mimi na wewe tukitembea na siraha kama sime au visu vikiwa hadharani bila kumdhuru yeyote, kuna uwezekano wa kukamatwa na kuchukuliwa hatua, ila kuna kundi linaruhusiwa kutembea na siraha kwa kisingizio cha tamaduni.

Nikwamba haya makundi mawili tamaduni zao ziko juu ya sheria?

Mbona tamaduni za wengine zinapingwa vikali na mamlaka ila za haya makundi mawili zinapewa kipaumbele?

Watanzania tumekubali baadhi ya wanachi wafungwe na wengine wafaidi matunda ya nchi kwa kisingizio cha tamaduni?

Sina uhakika sana ila wapokot walipewa umaalumu kama wanaopewa wale watembea na sime, leo wanamiliki siraha za moto na wamefikia hatua ya kutunishiana misuri na Jeshi.
 
sheria ilikuja ikawakuta wakiendelea na maisha na tamaduni zao, ndio maana kidogo kidogo wanapewa elimu ilio nje ya mfumo wao na kuwaingiza kwenye mfumo wa sheria japo ni ngumu kwao kuelewa lakini kuna wakati wataelewa huko mbeleni.
 
Na wale wanaovaa majambia kiunoni wakati wa harusi vipi??
 
Tokea lini masai aka affect Nature?? Awe na elimu au asiwe nayo ni watu wa misimamo...na wana tamaduni za kuheshimiana
 
Tokea lini masai aka affect Nature?? Awe na elimu au asiwe nayo ni watu wa misimamo...na wana tamaduni za kuheshimiana
Tamaduni zao ziko juu ya sheria? Kila kabila wakiamua kuziishi tamaduni zao tutakuwa tayari kukubaliana nao?

Sheria haziruhusu kutembea na siraha kinyume cha taratibu haijalishi huna lengo au unalengo la kudhuru.

Wasukuma ni utamaduni wao kufuga ng'ombe na mbuzi, mbona wao hawapewi kipaumbele kama wanavyopewa wamasai?
 
sheria ilikuja ikawakuta wakiendelea na maisha na tamaduni zao, ndio maana kidogo kidogo wanapewa elimu ilio nje ya mfumo wao na kuwaingiza kwenye mfumo wa sheria japo ni ngumu kwao kuelewa lakini kuna wakati wataelewa huko mbeleni.
Makabila yapi yamekuwepo baada ya sheria?

Makabila mengine yanatamaduni zao na haziko juu ya sheria, Kwanini wao?
 
Tamaduni zao ziko juu ya sheria? Kila kabila wakiamua kuziishi tamaduni zao tutakuwa tayari kukubaliana nao?

Sheria haziruhusu kutembea na siraha kinyume cha taratibu haijalishi huna lengo au unalengo la kudhuru.

Wasukuma ni utamaduni wao kufuga ng'ombe na mbuzi, mbona wao hawapewi kipaumbele kama wanavyopewa wamasai?
We ni kilaza haswa
 
utamaduni wa kushinda madrasa sio shuleni bado znz unasumbua ina maana wapo juu ya sheria
 
Yule mama aliyefungwa miaka 30 kisa nyama ya swala hakimu alaaniwe, majaji walioshindwa kumsimamia yule hakimu walaaniwe na Rais aliyeacha ile dhuluma itendeke alaaniwe
 
utamaduni wa kushinda madrasa sio shuleni bado znz unasumbua ina maana wapo juu ya sheria
Sio kweli,wanakwenda madrasa baada ya mda wa shule.Hakuna madrasa inayofundisha mda wa shule,ila kwa watuwazima na vijana waliomaliza shule na watoto wa chekekechea wanaotoka shule mapema saa 5.
 
We ni kilaza haswa
Ila wewe mwenye akili unafurahia mama kufungwa zaidi ya miaka 20 kwa nyama kilo moja, ila kuna kundi linafanya uwindaji haramu na wanaachwa Kwasababu wazungu wanafurahia kuwaona wakiishi hivyo.
 
Wahadzabe na wamasai ni mojawapo ya vivutio vya utalii. Kuna watu wanatoka ulaya na sehem nyingine duniani kuja kuwaona wamasai na wahadzabe. Makabila haya yakipotea utalii pia utayumba ndo mana serikali inawalinda kwa njia zote.
Ahaaa kwahiyo tumeamua kuwaacha watu wetu wasipate elimu, waendelee kuishi porini na kuua wanyama pori Kwasababu wazungu wanapenda.

Unaweza nisaidia ni sehemu gani uko kwa wazungu wameacha watu wao waishi maisha ya hovyo kama haya kwa kigezo cha utalii ili nasisi twende tukatalii?

Au ni sehemu gani ulaya tamaduni ziko juu ya sheria ili kulinda utalii?
 
utamaduni wa kushinda madrasa sio shuleni bado znz unasumbua ina maana wapo juu ya sheria
Kama tumeamua kuheshimu tamaduni za watu basi tuheshimu zote nasio kuwapa kipaumbele kundi la watu.

Hao watoto wakimasai wanaochunga ngo'mbe na hawasomi wako sawa sindio?
 
Back
Top Bottom