Aaron Arsenal
JF-Expert Member
- Jul 24, 2014
- 24,501
- 28,711
Na Malisa GJ,
Leo Kenya imezindua ripoti ya BBI, ambayo ni kifupi cha maneno Building Bridge Initiatives, yani jitihada za kujenga daraja la maridhiano ya kitaifa.
Ripoti hiyo imezinduliwa katika ukumbi wa BOMAS jijini Nairobi na kuhudhuriwa na zaidi ya watu 5000, huku mamilioni wengine wakifuatilia kupitia runinga. Rais Rais Uhuru Kenyatta ndiye aliyeongoza shughuli hiyo, akisindikizwa na viongozi wa ndani na nje ya nchi.
Tanzania imewakilishwa na Waziri Palamaganda Kabudi ambaye ametoa hotuba nzuri na ya kusisimua. Ameongea kwa weledi mkubwa akisistiza mshikamano na maridhiano kitaifa. Amelaani vyama tawala kukumbatia madaraka na kupuuza wenye mawazo mbadala.
Ameshauri kuwepo kwa serikali zinazokaribisha mawazo mbadala, na kushirikisha vyama vya upinzani katika kuunda serikali. Hutaamini kama ni yule mzee mwenye "tashwishwi" anayeongea kwa "kujibagaza" akiwa hapa chini.
Ripoti ya BBI ni kilele cha mchakato ulioanza mwezi Machi mwaka jana (2018). Ripoti imesheheni mambo mengi sana, lakini baadhi ya mapendekezo yaliyopo kwa kifupi ni kama ifuatavyo;
#KISIASA;
1. BBI inapendekeza demokrasia jumuishi (Consociationalism). Yani ukishindwa kwenye uchaguzi hupotezi kila kitu. Kwa mfano CCM iliyopata kura mil.8 haikupaswa kuunda serikali yenyewe na kupuuza vyama vya upinzani vilivyopata zaidi ya kura mil.6. Consociationalism inazuia mmoja kushinda na kubeba madaraka yote, na aliyeshindwa kupoteza kila kitu.
2. Wagombea wa nafasi ya urais watakaoweza kufikisha walau 5% ya kura watapata ubunge moja kwa moja.
3. Mgombea atakayeshindwa urais (aliyeshika nafasi ya pili) atakuwa ndiye Kiongozi wa kambi ya upinzani bungeni.
4. Kuwepo kwa Tume huru ya uchaguzi ambayo Mwenyekiti wake atakuwa na madaraka ya kitendaji (Executive Powers).
5. Kipengele cha sheria kinacholazimisha Mwenyekiti wa Tume ya uchaguzi kuwa Mwanasheria/Jaji kifutwe.
6. Tume ya uchaguzi iwe na wajumbe kutoka vyama vya siasa (vyenye wabunge), asasi za kiraia (NGOs) na sekta ya habari. Wanaamini 'composition' hiyo itakua mwarobaini wa Tume huru ya uchaguzi, na itakuwa ya kudumu.
7. Rais awe mkuu wa nchi na mkuu wa serikali, na achaguliwe kwa absolute majority ya kura zote (50% + 1). Kama hakuna mgombea atakayepata 50% + 1 basi wagombea wawili wa juu watapigiwa kura tena.
8. Kuwe na Waziri Mkuu ambaye atateuliwa na Rais kutoka chama chenye wabunge wengi. Atakuwa mtendaji mkuu wa serikali na kiongozi wa serikali bungeni.
#MAADILI_YA_UTUMISHI;
1. Watumishi wa umma wanaomiliki biashara zao binafsi wamezuiwa kufanya biashara na serikali au taasisi zake.
2. Ikitokea kashfa ya ufisadi, 5% ya fedha zilizokombolewa apewe aliyeibua ufisadi huo. Yani kwa mfano Kafulila alivyoibua ufisadi wa 400Bil za Escrow, angepewa 20Bil.
3. Kiongozi wa umma akiwa na mali zinazozidi thamani ya KSH 50M (kama Bil 1 za kitanzania) aeleze alivyozipata.
#KIUCHUMI;
1. Kiwango cha juu cha deni la taifa (debt ceiling) kiwe 45% ya GDP. Kwa sasa kiwango cha deni la Kenya ni 90% ya GDP yao, kwahiyo wameamua kuifunga mkanda serikali 'isikopekope hovyo'.
2. Mashirika ya umma yawe na mfuko maalumu wa kutoa mafunzo kwa vijana kwenye ubunifu wa biashara na ujasiriamali.
3. Kuondoa "madalali" kwenye sekta ya kilimo ili kuboresha ufanisi wa sekta hiyo, na kumuwezesha mkulima kuwasiliana na mteja moja kwa moja.
4. Kuondoa kodi kwa vijana wanaoanza biashara, mpaka pale biashara zao zitakapoanza kuimarika.
5. Kuongeza mapato yanayokwenda kwenye serikali za mikoa (kaunti) kutoka 15% ya sasa mpaka 35%.
6. Kuhakikisha magavana wanatenga 20% ya fedha za kaunti kwenda kwenye mifuko ya maendeleo ya kata.
Je na Tanzania nasi tunahitaji BBI?
Kwa hisani ya Malisa GJ
Pia soma
www.jamiiforums.com
Leo Kenya imezindua ripoti ya BBI, ambayo ni kifupi cha maneno Building Bridge Initiatives, yani jitihada za kujenga daraja la maridhiano ya kitaifa.
Ripoti hiyo imezinduliwa katika ukumbi wa BOMAS jijini Nairobi na kuhudhuriwa na zaidi ya watu 5000, huku mamilioni wengine wakifuatilia kupitia runinga. Rais Rais Uhuru Kenyatta ndiye aliyeongoza shughuli hiyo, akisindikizwa na viongozi wa ndani na nje ya nchi.
Tanzania imewakilishwa na Waziri Palamaganda Kabudi ambaye ametoa hotuba nzuri na ya kusisimua. Ameongea kwa weledi mkubwa akisistiza mshikamano na maridhiano kitaifa. Amelaani vyama tawala kukumbatia madaraka na kupuuza wenye mawazo mbadala.
Ameshauri kuwepo kwa serikali zinazokaribisha mawazo mbadala, na kushirikisha vyama vya upinzani katika kuunda serikali. Hutaamini kama ni yule mzee mwenye "tashwishwi" anayeongea kwa "kujibagaza" akiwa hapa chini.
Ripoti ya BBI ni kilele cha mchakato ulioanza mwezi Machi mwaka jana (2018). Ripoti imesheheni mambo mengi sana, lakini baadhi ya mapendekezo yaliyopo kwa kifupi ni kama ifuatavyo;
#KISIASA;
1. BBI inapendekeza demokrasia jumuishi (Consociationalism). Yani ukishindwa kwenye uchaguzi hupotezi kila kitu. Kwa mfano CCM iliyopata kura mil.8 haikupaswa kuunda serikali yenyewe na kupuuza vyama vya upinzani vilivyopata zaidi ya kura mil.6. Consociationalism inazuia mmoja kushinda na kubeba madaraka yote, na aliyeshindwa kupoteza kila kitu.
2. Wagombea wa nafasi ya urais watakaoweza kufikisha walau 5% ya kura watapata ubunge moja kwa moja.
3. Mgombea atakayeshindwa urais (aliyeshika nafasi ya pili) atakuwa ndiye Kiongozi wa kambi ya upinzani bungeni.
4. Kuwepo kwa Tume huru ya uchaguzi ambayo Mwenyekiti wake atakuwa na madaraka ya kitendaji (Executive Powers).
5. Kipengele cha sheria kinacholazimisha Mwenyekiti wa Tume ya uchaguzi kuwa Mwanasheria/Jaji kifutwe.
6. Tume ya uchaguzi iwe na wajumbe kutoka vyama vya siasa (vyenye wabunge), asasi za kiraia (NGOs) na sekta ya habari. Wanaamini 'composition' hiyo itakua mwarobaini wa Tume huru ya uchaguzi, na itakuwa ya kudumu.
7. Rais awe mkuu wa nchi na mkuu wa serikali, na achaguliwe kwa absolute majority ya kura zote (50% + 1). Kama hakuna mgombea atakayepata 50% + 1 basi wagombea wawili wa juu watapigiwa kura tena.
8. Kuwe na Waziri Mkuu ambaye atateuliwa na Rais kutoka chama chenye wabunge wengi. Atakuwa mtendaji mkuu wa serikali na kiongozi wa serikali bungeni.
#MAADILI_YA_UTUMISHI;
1. Watumishi wa umma wanaomiliki biashara zao binafsi wamezuiwa kufanya biashara na serikali au taasisi zake.
2. Ikitokea kashfa ya ufisadi, 5% ya fedha zilizokombolewa apewe aliyeibua ufisadi huo. Yani kwa mfano Kafulila alivyoibua ufisadi wa 400Bil za Escrow, angepewa 20Bil.
3. Kiongozi wa umma akiwa na mali zinazozidi thamani ya KSH 50M (kama Bil 1 za kitanzania) aeleze alivyozipata.
#KIUCHUMI;
1. Kiwango cha juu cha deni la taifa (debt ceiling) kiwe 45% ya GDP. Kwa sasa kiwango cha deni la Kenya ni 90% ya GDP yao, kwahiyo wameamua kuifunga mkanda serikali 'isikopekope hovyo'.
2. Mashirika ya umma yawe na mfuko maalumu wa kutoa mafunzo kwa vijana kwenye ubunifu wa biashara na ujasiriamali.
3. Kuondoa "madalali" kwenye sekta ya kilimo ili kuboresha ufanisi wa sekta hiyo, na kumuwezesha mkulima kuwasiliana na mteja moja kwa moja.
4. Kuondoa kodi kwa vijana wanaoanza biashara, mpaka pale biashara zao zitakapoanza kuimarika.
5. Kuongeza mapato yanayokwenda kwenye serikali za mikoa (kaunti) kutoka 15% ya sasa mpaka 35%.
6. Kuhakikisha magavana wanatenga 20% ya fedha za kaunti kwenda kwenye mifuko ya maendeleo ya kata.
Je na Tanzania nasi tunahitaji BBI?
Kwa hisani ya Malisa GJ
Pia soma
Prof. Kabudi ahudhuria hafla ya uzinduzi ripoti ya BBI nchini Kenya inayopendekeza uwepo wa cheo cha Waziri Mkuu na Kiongozi wa Upinzani Bungeni
Waziri wa mambo ya nje Prof. Kabudi amehudhuria hafla ya uzinduzi wa ripoti ya Building Bridge Initiatives (BBI) nchini Kenya ambayo imehudhuriwa na viongozi wote wakuu wa Jamhuri ya Kenya. Miongoni mwa mapendekezo ya BBI ni haya: 1. Uwepo wa cheo cha Waziri mkuu ambaye ni lazima awe Mbunge wa...