Je, Tanzania kwa sasa haina Baba au Mama wa Taifa hususani Wastaafu ambao kwa nia njema wanaweza kusema neno la dhati bila hofu na bila hila?

Pang Fung Mi

JF-Expert Member
Joined
Nov 10, 2022
Posts
6,653
Reaction score
13,919
Je, Taifa halina wenyewe kiasi kwamba Rais wa nchi ndivyo anakuwa final, na nchi imekosa Wastaafu wa dhati kabisa kusema kauli njema zenye kuakisi tunu ya hekima na busara za Taifa hili, seriously?

Are we in a dead state? Like serious? The state is torn to that extent?

Uhuru wa maoni ya kushauri ulikufa, kukemea maovu kumekufa?

Maskini, Mstaafu, Asiye na Cheo hana haki ya kusema, are we serious?

Masikitiko makubwa, ni aibu sana, watu wanakaa kimya kwenye mambo ya msingi?

Annoyed 😠😠😠

Wadiz
 
Wakijaribu kunyanyua midomo wapo vijana wa chama wanawachamba
 
Wakati watu wanataka katiba mpya si uliwaona viazi?
 
Ni Baba wa Taifa aliyekuwa na Ujasiri huo! Baada ya kufa sidhani kama kuna mzee mwingine aliyeweza au ambaye anaweza kulikemea Taifa kwa yale yasiyopendeza!
Mzee Sinde na Mzee Butiku ndiyo angalau tena kwa tahadhari wanajaribu kusema maovu wanayoyaona.
Lakini hawasikilizwi!
Mkuu waliopo hawawezi maana Kula yao iko mikononi mwa Serikali.
 
Mabadiliko ya tabia nchi yamesababisha chawa kuwa wengi na kuwasilimisha.
 
Sio kweli mkuu, Butiku na Warioba hujitokeza waziwazi kukemea mambo yanayofanyika ya ovyo,mpaka waliwahi ambiwa na utawala fulani eti, Wanawashwa washwa!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…