Je, Tanzania kwa sasa inao bodaboda wangapi? Au pikipiki zipo ngapi Tanzania

Kudhania tuu
Kwamba sabb bei chini basi watu wengi watakuwa nazo kuliko gari
Inawezekana lakin kumbuka pia watu wengi huangalia madhara yaletwao na uendeshaji wa pikipiki yakiwemo maradhi katika mfumo wa kupumua (Pneumonias), ajali, urahisi wa kuibiwa, vikwazo vya idadi ya abiria na aina ya watu unaoweza kubeba pamoja na umbali unaoweza kusafiri(Distance). Lakini sababu ya bei kuwa chini e.g. Tzs mil 2-3 sio wote wanaimudu. Ndo mana wengine hukopa au kutumia Mkataba.
 
Hapo kuna pikipiki bila Bajaj na sehemu ya pili pikipiki pamoja na Bajaj
 
2016-17 walianza kutumia number plate zao MC.

Kuna baadhi ya old number plate T123AAA hawakuenda ku-update.

Source: Trust me Bro.
Namba za MC zilianza kipindi Cha kikwete. Nakumbuka ilikua kwenye bajeti aliyoleta Saada Mkuya waziri wa fedha wa kikwete nadhani wa mwisho.
 
Kwa wastani kila kaya ina bodaboda 1.
Rejea sensa ya makazi utajua kuna kaya ngapi then angalia trend ya ongezeko la kaya kutoka 2022-2024.
Ni majanga kwa hakika
Uko vizuri. Kwa mujibu wa Takwimu ya idadi ya watu katika majimbo, SWM 2022
Tanzania ilikuwa na kaya 14,297,184. Endapo kila kaya itakuwa ina bodaboda 1, aisee! ni majanga. ie. Zipo pikipiki Takriban milioni 14+. Lakini Siamini bado.
 
Hapo kuna pikipiki bila Bajaj na sehemu ya pili pikipiki pamoja na Bajaj
Hoja hii 👆 👆 inaonekana kukinzana na pale uliposema walau kila kaya ina pikipiki. Mwaka 2022 Tz ilikuwa na kaya zaidi ya milioni 14. Kama tukisema walau Nusu ya kaya zote inamiliki pikipiki, tutakuwa na pkpk zaidi ya mil. 7. Hapo hilo unalisemeaje mkuu?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…