Je, tuendelee kustaafisha Jezi ya Mkude kama Legend, au tumuite Legend Msaliti?

G4rpolitics

JF-Expert Member
Joined
Jul 29, 2015
Posts
4,369
Reaction score
5,248
Sitaki kuandika uchambuzi wowote kuhusu Mkude, swali ni je, tustaafishe jezi yake au, tufute hilo swala kwa kuwa kaenda upande wa pili kutafuta masilahi?
 
Mlitaka Mkude astaafu kucheza soka? Au mlitaka aende penye riziki ndogo? Huu ni ujuha.

Mkude hajataka kuondoka Simba. Bali uongozi ndiyo uliona wampe mkono wa kheri akatafute changamoto kwingine. Ina maana walipaswa kumchagulia timu ya kwenda? La hasha!.

Mkude ataendelea kuwa 'Legend' kwenye klabu yetu. Ninyi mnaotafsiri vinginevyo ni Mashabiki Maandazi.
 
Mkudee anafanya kazi ni mwajiriwa kama waajiriwa wengine

Kama wewe unaweza kuhama kampuni moja kwenda nyingine , kumbuka Ibrahim ajibu alihama yanga kwenda simba wakati ambao yanga walikuwa wanamhitaji na walikuwa na hali tete.

Kuna muda inabidi tusiwalaumu kwakuwa inabidi wasifuate furaha yetu nao wanahitaji kufika malengo.
Note: ili ifanikiwe usifuate matakwa ya watu
 
Ila sasa Yanga waache maneno ya kejeli
 
Safi sana, jibu nimelipenda hili
Yaani watu hata huwa hawaeleweki.

Mchezaji huyo unayeng'ang'ania abaki kwenye timu akufurahishe, siku ukigundua hana mafanikio na maisha yake magumu, unashangaa pia, huku ukilaumu klabu na kwenda mbali zaidi kuwasingizia wachezaji kwa kupenda starehe.
 
Ila mi simwamini kabisa. mechi za derby tunaomba atupishe, atulie zake bench tu. atacheza mech nyingine.
 
Kaka nikushukuru Kwa mawazo mapana. Wasamehe uliowaita mashabiki maandazi ingawaje kiukweli ni Mabumunda wala si Maandazi.
 
Kabisa mkuu , ajabu akiondoka anavyoandamwa na kashfa ndipo unapogundua kubwa unatakiwa ufanye kwa manufaa yako sio kwa manufaa ya watu kuna muda watu hawana shukrani ukizeekea kwao na huna kitu wala hawatakukumbuka
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…