Pre GE2025 Je, Uchawa unazorotesha Uwajibikaji? Ipi ni namna bora ya kuhakikisha Uwajibikaji unakuwa sehemu ya Utamaduni wa Kisiasa?

Pre GE2025 Je, Uchawa unazorotesha Uwajibikaji? Ipi ni namna bora ya kuhakikisha Uwajibikaji unakuwa sehemu ya Utamaduni wa Kisiasa?

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)

JamiiTalks

JF Advocacy Team
Joined
Aug 7, 2018
Posts
685
Reaction score
1,124
UCHAWA Space.jpg

Usikose kujiunga nasi katika Mjadala wa "Je, 'Uchawa' unakwamisha Uwajibikaji?" Alhamisi hii ya Februari 27, 2025, kuanzia Saa 12 jioni hadi 2 usiku, kupitia Xspaces ya JamiiForums

'Washtue' ndugu, jamaa au marafiki ili wawe sehemu ya Mjadala huu muhimu kwa 'kesho' ya Nchi yetu.

Washiriki watapata fursa ya kutoa maoni au mapendekezo na kuuliza maswali Wazungumzaji wetu

Kushiriki bofya https://jamii.app/KujipendekezaSpace

Khalifa Said (Mwandishi wa habari The Chanzo)

"Uchawa sidhani kama unazorotesha uwajibikaji, ninavyodhani mimi kitu kikubwa kinachodhorotesha uwajibikaji ni uimla, ukatili wa kidola, matumizi ya nguvu kwa polisi na mbinu nyingine za kihuni na za kishenzi zinazotumiwa na waliopa madarakani kuwanyamazisha watu ikiwemo kuwateka"

"Vijana wengi wanajikaribisha kwenye nafasi za Viongozi kwa kuwa wanaona hiyo ndio njia salama ya wao kufanikisha mambo yao mbalimbaliKama tunataka kuondoa hali hiyo tunatakiwa kuweka msingi ambao kila mchango wa Mtu unaweza kuheshimiwa tofauti na ilivyo sasa, mfano Msanii ukiimba nyimbo tofauti na wale waliopo Madarakani inakuwa ngumu kufanikiwa"

"Hautakiwi kushangaa kuona siku moja hata usiyemtegemea akajiunga kwenye timu ya hao wanaoitwa 'Machawa' kwa kuwa atakuwa anafanya hivyo ili kuweza kuishiKila Mtu anataka kuishi Maisha mazuri hivyo Uchawa sio sababu ya kukosekana kwa Uwajibikaji, matumizi mabaya ya Madaraka ndio chanzo"

"Vijana wengi wanajikaribisha kwenye nafasi za Viongozi kwa kuwa wanaona hiyo ndio njia salama ya wao kufanikisha mambo yao mbalimbaliKama tunataka kuondoa hali hiyo tunatakiwa kuweka msingi ambao kila mchango wa Mtu unaweza kuheshimiwa tofauti na ilivyo sasa, mfano Msanii ukiimba nyimbo tofauti na wale waliopo Madarakani inakuwa ngumu kufanikiwa"

"Tukiendelea kuwakandamiza Machawa tutakuwa hatusemi ukweli na hatuzungumzii tatizo la msingi ambalo ni la Dola kukandamiza Jamii"

Carlos Buto (Mkuu wa idara ya programu TCD)

Carlos amezungumzia kuhusu historia ya Uchawa, ameeleza uchawa haujanza leo katika nchi yetu, uchawa umekuwepo kuanzia kipidni cha mfumo wa chama kimoja lakini kwa hivi sasa unaonekana sana kutokana na uwepo wa mitandao ya kijamii. Ameeleza kuwa mifumo bora ya uchaguzi ndiyo inayoweza kuondoa kadhia hii ya uchawa.

"Ipo mifano ya Nchi kadhaa, mfano Nchi za Magharibi kama Norway, Ujerumani, Canada ukiangalia siasa zao sio za kubebana kwa mambo ya kusifiana, yanazingatia hoja na Utendaji wa TaasisiBoksi la Kura linaamua namna gani unamwajibisha Kiongozi, hivyo kama Kiongozi hana mwenendo mzuri wa utendaji, Kura yako ndio itakayomuwajibisha"

"Uchawa unaanzia katika ngazi ya Familia zetu, mfano ni kawaida kupokea simu na kuitwa majina kama “Mkuu” n.k. Ukishaujenga kuanzia ngazi hiyo ni ngumu kuuondoa katika Ngazi ya Taifa"

Amependekeza mabadiliko ya mifumo ya kimaisha, mfumo wa kishera na mifumo ya kitaasisi ili vitu viongozwe kwa mifumo na siyo kwa matwaka ya mtu ili kuondokana na tatizo la uchawa

Annastazia Rugambwa (Mkurugenzi wa Uchechemuzi Twaweza)

Annastazia ameeleza na kukubali kuwa uchawa ni tatizo kubwa sana na ili kuweza kutatua uongozi wa kiimla inabidi uchawa ukomeshwe. Ameleza pia kutokana na utafiti walioufanya watanzania zaidi ya 53% wanazungumzia kuhusu hali ngumu ya maisha, wengine wameelezea kuhusu ukosefu wa ajira. Ameeleza kuwa Chanzo cha uchawa ni hali ngumu ya maisha, kama wangekuwa na hali nzuri za maisha isingekuwa rahisi kwa wao kufanya uchawa kwani uchawa ni aibu.

"Wakati mwingine Uchawa unaharibu Viongozi, wapo wanaoingia wakiwa na nia ya kufanya mabadiliko kweli lakini kwa kuwa tunakuwa na tamaduni ya kuwasifia sana, wanazoea na inapotokea wanahojiwa wanakuwa wakali"

Ameeleza pia kuwa umasikini ndiyo mtaji wa viongozi na hiyo ndiyo sababu ya wao kutokupambana na umasikini kwa sababu ndiyo mtaji wao. Ameuliza kama umasikini ukiondoka machawa watatoka wapi?

"Uchawa una viwango, kuna viwango vya juu, kati na chini, hata Wanawake wapo Machawa, wanatumiwa kama ngazi ili wanaowatumia wafike wanapopataka"

Rubara (Mdau)

"Tunahitaji kupata Mifumo ya Elimu ya Uraia kama ambayo tulikuwa tunaipata Miaka ya 80Kuna uhitaji mkubwa wa kutoa Elimu ya Haki ya Mwananchi, hiyo inaanzia kwa Elimu ya Uraia"

Mwaura Robert (Mdau)

"Uchawa haupo tu kwenye Siasa kuna wakati ulifika hadi katika Mamlaka za Kisheria, uamuzi ulifanyika huku mhusika anayefanya maamuzi akilenga kupandishwa cheo"

"Kuwa na Watu ambao wanatokana na upendeleo, wanapofanya kazi duni hawawezi kuwajibishwaKwa ufupi Uchawa unaletwa na Umasikini"

Francis Nyonzo (Mdau)

"Uchawa ni kusifia tu hata kama jambo sio la kusifia, mfano tabia ya Watoto kuwa na utii bila kutoa hoja imekuwa ikitengenezwa na Wazazi na Walezi, kadiri inavyokuwa inamtengeneza Mtoto ambaye hawezi kubishana kwa hoja"

"Inatakiwa Watu wafundishwe kuwa na msimamo wa kusimamia kile wanachokiamini, hilo linatakiwa kwenda pamoja na Utawala wa Sheria"

Nkindikwa (Mdau)

"Wakati tunapata Uhuru tulikuwa na Vijana wanaoweza kuhoji Viongozi, lakini leo hawapo Vijana wa aina hiyo, sababu ni kwa kuwa wengi wao wanazingatia maslahi binafsi"

Singularity (Mdau)

"Ikitokea kikundi ambacho kinataka kuishi chenyewe bila kujali maslahi ya Watu wengine, hicho kikundi hakifai kwenye Jamii"

"Inapotokea katika Kundi la Watu Milioni moja, kati yao Watu Laki tisa wakiwa wanatoa kilio cha uhitaji Maji, wakati huohuo kundi la Watu 100 wao wanasema kila kitu kipo sawa, huo ndio Uchawa ambao hauna faida, hiyo ni kama Saratani na inatakiwa kuondolewa"
 
Maoni yangu
Tuipunguzie siasa thamani kubwa tuliyoipa kwasasa na tuipe taaluma thamani inayostahili uchawa utatoweka automatically kwakuwa kwenye taaluma kinachoongea ni weledi na ujuzi lakini kwenye siasa hasa kwa viongozi wenye maono kimo cha mbilikimo uchawa ndio think tank wanayoitegemea

Yakub Talib (Mdau)

"Suala la Uchawa ni Mfumo, ilifikia hatua Watu wakaona huku tunapokwenda hakufai, kilichofanyika Watu walitesti wakaona inalipa"

"Niliwahi kufuatwa na Chama fulani kikinitaka niwe chawa, nilitafakari sana kabla ya kufanya maamuzi lakini baadaye nikaona hapanaPamoja na yote tunatakiwa kufahamu kuwa Uchawa wa sasa umekuwa sugu"
 
Mkuu mbona jibu unalo?
Ni kuondoa Uchawa tu! Changamoto unaondoaje Mbogamboga ambayo ndiyo source ya Uchawa?
 
Dawa ni Katiba Mpya inayowapa nguvu watendaji na mifumo kuliko Wanasiasa.

Kuwapa kipaumbele Wanasiasa kuliko wataalam na Watendaji ndo kumetufikisha huku.

Unakuwa na Sheria na Katiba ambayo kila nafasi inateuliwa na Rais na kutenguliwa na yeye alafu msiwe na uchawa?
 
Uchawa ni adui mkubwa sana wa maendeleo ya taifa letu kwa sasa na suala zima la uwajibikaji. kiongozi hata akikosea bado kuna watu watampamba kwa sababu tu wana maslahi yao binafsi
 
Maoni yangu
Tuipunguzie siasa thamani kubwa tuliyoipa kwasasa na tuipe taaluma thamani inayostahili uchawa utatoweka automatically kwakuwa kwenye taaluma kinachoongea ni weledi na ujuzi lakini kwenye siasa hasa kwa viongozi wenye maono kimo cha mbilikimo uchawa ndio think tank wanayoitegemea
Umemaliza yote Mkuu
 
Maoni yangu
Tuipunguzie siasa thamani kubwa tuliyoipa kwasasa na tuipe taaluma thamani inayostahili uchawa utatoweka automatically kwakuwa kwenye taaluma kinachoongea ni weledi na ujuzi lakini kwenye siasa hasa kwa viongozi wenye maono kimo cha mbilikimo uchawa ndio think tank wanayoitegemea
Kwa vile viongozi wanajua hawakubaliki wanatafuta chawa wanaodhani ni maarufu ili wawabebe, hata hivyo wananchi wamestuka
 
Chawa maana yake ni mpambe/mtu ambaye yupo na wewe bega kwa bega hadi utakapofilisika au ufakapopoteza mamlaka.
Kazi ya chawa ni kukushangilia kwa lolote hata ukinya madhabahuni mbele za waumini atatafuta maneno mazuri ya kukupamba kwamba umekunya vizuri
 
Obviously you know absolutely nothing about me!

Ungejua chochote kuhusu mimi wala usingeshangaa.

Ni ujinga wako tu [na sidhani unajua maana ya ujinga ni nini].
Ona ulivyopanic sasa Mkuu :KEKWlaugh::KEKWlaugh:... asante kwa kunijuza zaidi kuhusu wewe
 
Mwanasiasa anawajibika kwa nani au nani inabidi ndio amuwajibishe ?

Kama ni Mwananchi Je mwananchi atafanya hivyo bila kuwa na facts ukizingatia vyombo vya habari vimekuwa propaganda machines ?

Kwahio the only way sio kuwategemea wanasiasa kufichuana na Uchawa utapungua iwapo wananchi wataona ni uchafu na haufai (And why can we do That) ? Watu wanaotuhabarisha waache kutulisha Pumba....


NB: Chawa hana Gwanda wala Gamba....
 
Zamani waliwaita wapambe, leo ni machawa...they've been there miaka yote, ila wa sasa wamechangamka sana.
 
Mwanasiasa anawajibika kwa nani au nani inabidi ndio amuwajibishe ?

Kama ni Mwananchi Je mwananchi atafanya hivyo bila kuwa na facts ukizingatia vyombo vya habari vimekuwa propaganda machines ?

Kwahio the only way sio kuwategemea wanasiasa kufichuana na Uchawa utapungua iwapo wananchi wataona ni uchafu na haufai (And why can we do That) ? Watu wanaotuhabarisha waache kutulisha Pumba....


NB: Chawa hana Gwanda wala Gamba....
Vyombo vya habari vinafanya hivyo kwa sababu vingi havipo financially stable hivyo na wanao wanaendelea kuwalamba miguu viongozi
 
Back
Top Bottom