Je, ugaidi anaotuhumiwa nao Mbowe ni ugaidi wa serikali?

Je, ugaidi anaotuhumiwa nao Mbowe ni ugaidi wa serikali?

Nicholaus Kilunga

JF-Expert Member
Joined
Feb 15, 2014
Posts
1,188
Reaction score
570
Je Ugaidi anaotuhumiwa nao mh Mbowe ni ugaidi wa serikali?

Najaribu kutafakari kimyakimya kwa maandishi kuhusu mashataka aliyofunguliwa mwenyekiti wa CHADEMA mh Freeman Mbowe.

Nimejaribu kupitia rekodi mbalimbali za Mbowe tokea akiwa mwenyekiti wa vijana (BAVICHA) taifa, mpaka anakuwa mwenyekiti wa CHADEMA taifa, mbunge, mgombea urais na kiongozi wa kambi rasmi ya upinzani bungeni.

Kwa takribani miaka 15 mh Mbowe amefanya siasa za upinzani kwa mafanikio makubwa,mafanikio hayo ni ya jasho na damu,amepoteza mengi kuliko amevyopata kama angeamua kujitazama yeye binafsi na famila yake kuliko sisi watanzania, na kwa kupitia yeye wapo wanasiasa walioibuka na kukulia mikononi mwake na kupata mafanikio makubwa kisiasa hapa nchini ,hapa nawazungumzia wale wanasiasa ambao kwa namna moja ama nyingine walipitia mikononi mwake,wengine wakiwa wapo vyama vya upinzani mpaka sasa, na wengine walioamua kwenda CCM na wengine wapo serikalini mpaka napoandika tafakuri hii.

Kwa muda wote huo mh Mbowe amekuwa akifanya kazi na serikali kama mwanasiasa wa upinzani na mbunge,amekuwa pia akifanya kazi na taasisi za serikali,mashirika ya umma na ya le binafsi,makampuni ya serikali na binafsi pia,amekuwa akishirikiana na taasisi za ndani na nje ya nchi,dini na vyombo mbalimbali vya habari.

Ila kwa wakati wote huo serikali na vyombo vyake havikuwa na mtazamo wa kumwona Mbowe kama gaidi ila mwanasiasa wa upinzani na mfanyabiashara, na baba wa familia,mwenyekiti wa CHADEMA na kama ilikuwa inamtazama kama gaidi kwa kipindi chote hicho, je ilikuwa inamlea gaidi?

Ama ilikuwa inamchunguza na kumwacha azunguke nchi nzima akifanya shughuli zake, akijenga chama chake na kuwafunda viongozi na wananchama wake? Tutafakari tena, kama Mbowe anatuhumiwa kwa ugaidi vipi viongozi wa serikali waliopitia mikononi mwake?je na wao tunze kuwatazama kwa jicho la ugaidi?vipi wao hawakuwa magaidi wala kufundishwa ugaidi?

Je, kwa miaka yote serikali ilikuwa inamfumbia macho gaidi mpaka alipoanza kuongoza harakati za kudai katiba mpya na masuala mengine ya kidemokrasia?

Je, serikali inataka tuamini kwamba ilikuwa inamlinda gaidi?mpaka akawa kiongozi mkuu wa kambi rasmi ya upinzani? Kwa maslahi gani?

Je, serikali inafahamu athari za kutangaza kwamba imemshikilia Mbowe kwa tuhuma za ugaidi? Athari za kiuchumi, kidiplomasia na athari za kijamii?

Je, Serikali inajaribu kutuma ujumbe gani ndani na nje ya nchi?kwamba kwa sasa Tanzania tupo vitani tukiwindwa na magaidi na serikali ikipambana na magaidi?vp hao walipokuwa wanaandaa mpango huu wa kumshtaki mh Mbowe kwa tuhuma hizi,walitazama suala la utalii?walipima madhara ya shitaka hilo kimataifa na wageni wanataka kuja Tz kama watalii ama wawekezaji?

Maana kwa wenzetu huko ughaibuni neno ugaidi linamaana kubwa sana na ni neno lenye kuogofya sana ,tofauti na tawala nyingi za kiafrika zinazotumia neno hilo ama shitaka hilo kuwashinda wapinzani wao kisiasa na kuwajengea picha mbaya,jamii inaamini kesi hyo imechochewa zaidi kisiasa,hasa ikichochewa na siasa za maji taka alizokuwa ameziasisi mwendazake na ccm yake mpya,wakilenga kutaka kukifta chama kikuu cha upinzani CDM,ni bahati tu binadamu wanapanga na Mungu anaamua,.

siku hizi madai ya katiba mpya na demokrasia yamekuwa sehemu ya ugaidi? Je, tuziiteje serikali zilipita ambazo hazikuwahi kumwona Mbowe kama gaidi?je serikali imesahau maonyo waliyopewa na jaji kuhusu kesi za ugaidi wakati ule Wilfred Rwakatale kiongozi na mwanachama wa CDM wakati alipofunguliwa mashtaka ya ugaidi?kama wamesahau walejee kumbukumbu ya hukumu ile.

Huku Kwetu Kibondo Kigoma tunamsemo wetu unaosema(wuhagalikiwe ni ngona alavoma amazi, yaani aliesimamiwa na mamba mtoni ndo anaechota maji).

By Nick Kilunga
 
We mwenyewe unajua kuwa sababu ni katiba na hamna la zaidi lakini bado nawalaumu chadema ingebidi Mbowe Freeman Aikael alivyokamatwa na kuitwa gaidi watu kama mr Mbilinyi, Lema Godbless, Msigwa na wengine wengi akina chadema damu wangeendeleza kile Mbowe alitaka kufanya ili tu price kwamba Mbowe alikamatwa kwa ugaidi na siyo katiba lakini kusubiri Mbowe atoke ndiyo harakati ziendelee ni udhaifu tu

Sent from my TECNO KC8 using JamiiForums mobile app
 
Mkuu unapambana na Mtu mwenye Bunduki na wala hatishiki kuua?? Mtu mjinga unaachana naye. Fikiria kama.

Mtu angesema anasimama kidede mbele ya Jiwe angebaki salam? Uhai? Lakini wajanja waliachana naye wamebaki Hai Jiwe kafa.

Huwezi kucheza na kichaa mwenye Panga ukiwa mikono mitupu ukadhani kuwa ataogopa watu na wewe uonekane mwamba utapotea
 
We mwenyewe unajua kuwa sababu ni katiba na hamna la zaidi
Lakini bado nawalaumu chadema ingebidi Mbowe Freeman Aikael alivyokamatwa na kuitwa gaidi watu kama mr Mbilinyi, Lema Godbless, Msigwa na wengine wengi akina chadema damu wangeendeleza kile Mbowe alitaka kufanya ili tu price kwamba Mbowe alikamatwa kwa ugaidi na siyo katiba lakini kusubiri Mbowe atoke ndiyo harakati ziendelee ni udhaifu tu

Sent from my TECNO KC8 using JamiiForums mobile app
Easy said than Done
 
Mkuu unapambana na Mtu mwenye Bunduki na wala hatishiki kuua?? Mtu mjinga unaachana naye. Fikiria kama.mtu angesema anasimama kidede mbele ya Jiwe angebaki salam? Uhai? Lakini wajanja waliachana naye wamebaki Hai Jiwe kafa.

Huwezi kucheza na kichaa mwenye Panga ukiwa mikono mitupu ukadhani kuwa ataogopa watu na wewe uonekane mwamba utapotea
Harakati za kisiasa na za kudai mabadiliko uyatakayo huwezekana tu pindi mtu akiwa hai,na si vinginevyo,so ni muhimu kupambana na adui kwa akili zaidi ya nguvu
 
We mwenyewe unajua kuwa sababu ni katiba na hamna la zaidi
Lakini bado nawalaumu chadema ingebidi Mbowe Freeman Aikael alivyokamatwa na kuitwa gaidi watu kama mr Mbilinyi, Lema Godbless, Msigwa na wengine wengi akina chadema damu wangeendeleza kile Mbowe alitaka kufanya ili tu price kwamba Mbowe alikamatwa kwa ugaidi na siyo katiba lakini kusubiri Mbowe atoke ndiyo harakati ziendelee ni udhaifu tu

Sent from my TECNO KC8 using JamiiForums mobile app
Ulitaka waendeleze kipi ambacho hawakifanyi?mbona mengi tu yanaendelea kwa sasa ndani ya CDM?pengo la mwenyekiti lipo ila majukumu na ofisi yanaendelea kama kawaida mkuu
 
Easy said than Done
Moja ya tetezi mahakamani ingekuwa pomoja na hiyo yani kama kweli Mbowe alikamatwa kwa ugaidi mbona bado fulani na fulani wamekamatwa kwa kuendeleza alichokuwa anafanya Mbowe
Au wangeleta sababu gani nyingine

Sent from my TECNO KC8 using JamiiForums mobile app
 
Harakati za kisiasa na za kudai mabadiliko uyatakayo huwezekana tu pindi mtu akiwa hai,na si vinginevyo,so ni muhimu kupambana na adui kwa akili zaidi ya nguvu
That was my point. Ndio Maana Lissu alikuwa mwenye akili akamkimbia Jiwe. Leo Lissu yuko hai na ana fursa ya kuendeleza mapambano Jiwe hayupo. Sasa akili za uyo Lumumba sijui anataka kutushauri nini sisi wenye akili.
 
Mkuu unapambana na Mtu mwenye Bunduki na wala hatishiki kuua?? Mtu mjinga unaachana naye. Fikiria kama.mtu angesema anasimama kidede mbele ya Jiwe angebaki salam? Uhai? Lakini wajanja waliachana naye wamebaki Hai Jiwe kafa.

Huwezi kucheza na kichaa mwenye Panga ukiwa mikono mitupu ukadhani kuwa ataogopa watu na wewe uonekane mwamba utapotea
Nguvu hazijawahi kushinda maarifa
Lengo kuu ni kujibu hoja ya kwamba Mbowe siyo gaidi
Sisi tukija kama mbowe alivyokuja mtatupa kesi gani na mkitupa kesi kama ya Mbowe watakuja wengine na wengine na wengine hamtaweza kutumaliza mtaonekana wehu na watanzania na dunia nzima mwisho wa siku katiba itashinda na watu mia au mia mbili waliopo jela kwa ugaidi wa katiba watakuwa washindi tutakaa chini kuplani namna ya kuunda katiba mpya

Sent from my TECNO KC8 using JamiiForums mobile app
 
Freeman Mbowe ni Mtu wa Watu, mtu wa Mungu Yule.
Hakika

%E2%9C%8C%EF%B8%8F%E2%9C%8C%EF%B8%8F%E2%9C%8C%EF%B8%8F.jpg
 
Kina shilole, lopolopo manara wana walinzi lakini Mbowe anazuiwa kwa kila namna kuwa na walinzi
 
Me nilikuelewa na nilimwelewa hata Lissu,japo Mh Lisu alikuja kustukia hila za mwendazake huku tayari alikuwa ashapata madhara.
 
Nguvu hazijawahi kushinda maarifa
Lengo kuu ni kujibu hoja ya kwamba Mbowe siyo gaidi
Sisi tukija kama mbowe alivyokuja mtatupa kesi gani na mkitupa kesi kama ya Mbowe watakuja wengine na wengine na wengine hamtaweza kutumaliza mtaonekana wehu na watanzania na dunia nzima mwisho wa siku katiba itashinda na watu mia au mia mbili waliopo jela kwa ugaidi wa katiba watakuwa washindi tutakaa chini kuplani namna ya kuunda katiba mpya

Sent from my TECNO KC8 using JamiiForums mobile app
Ila pia kubadili mbinu haijawahi kuwa tatzo mkuu,unaweza hata kurudi nyuma ili kujipanga,siasa ni sayansi mkuu
 
Back
Top Bottom