Je, Uhaini unaweza fanywa na muomba Mungu?

Je, Uhaini unaweza fanywa na muomba Mungu?

Magufuli 05

JF-Expert Member
Joined
May 7, 2023
Posts
1,433
Reaction score
2,791
Uhaini( treason)the offense of attempting by overt acts to overthrow the government of the state to which the offender owes allegiance or to kill or personally injure the sovereign or the sovereign's family.

Nimejaribu kufikiri kidogo, na nimekumbuka baadhi ya vitabu nilivyosoma vile mwl. J.k. Nyerere alivyohangaika na wahaini. Kisha nikaangalia Hawa wanaotuhumiwa kwa uhaini hivi sasa. Nikajiuliza je ni kweli kwa hadhi Yao wanaweza kufanya uhaini? Nikajijibu " hapana"

Nasadiki kusema kwamba toka nianze kujitambua na kufuatilia siasa toka awamu ya pili ya mkapa mpaka sa100 sikuwahi kusikia Mtanzania akifunguliwa kesi ya uhaini zaidi ya Hawa Wenzetu waliofunguliwa hivi sasa.

Nimezoea kusikia Watanzania wakifunguliwa kesi za UGAIDI lakini si uhaini. Uhaini kosa la juu mno ambalo kwa akili yangu halipangwi wala kutekelezwa na waomba mungu Bali hufanywa na

1. Top government officials
2. senior or top military officers
3. Business tycoon but in coordination with others.

Mwl.nyerere aliwahi kumbana na watu wa namna hiyo wakiwemo akina marehemu Zacharia Hanspope na wengineo kama Bibi Titi.

Leo hii mdude na mwabukusi. Hawa ni raia waomba Mungu tu. Kweli wanaweza kufanya uhaini? Odinga na Martha pale Kenya wameendesha maandamano ya watu maelfu lakini hawajafunguliwa mashtaka kama hayo. Sisi huku tunaziba vijana midomo kwa vitisho vya uhaini. Kweli?

Wakae gerezani mwaka Kisha watolewe kwa jamhuri kukosa ushahidi au mwendesha mashtaka Hana Nia ya kuendelea na kesi hii.

Je Nini faida yake? Wewe unayefanya hivyo ama kwa makusudi au kwa maelekezo toka juu mwisho wako ni upo?

Kwanini serikali inahofu na wakosoaji.? Si mliridhia demokrsia Tena kwa mikataba lukuki?

Je mnataka tuwe na taifa la mazuzu ambao kila kitu kinafanywa waseme mama anaupiga mwingi?? Hapana.

Mimi nasema hapana. Mtawanyamazisha midomo Yao lakini hamtanyamazisha fikra zao.

Hiki mnakifanya leo siyo cha kwanza na walishafanya wengi lakini mwisho wao ulifika.

Nani anamkumbuka Mobutu,Idd Amin na Bokasa?

Nchi yangu, " unaweza kuwadanganya watu kwa nyakati tofauti lakini huwezi kuwadanganya watu wote kwa wakati mmoja"
 
Uhaini( treason)the offense of attempting by overt acts to overthrow the government of the state to which the offender owes allegiance or to kill or personally injure the sovereign or the sovereign's family.

Nimejaribu kufikiri kidogo, na nimekumbuka baadhi ya vitabu nilivyosoma vile mwl. J.k. Nyerere alivyohangaika na wahaini. Kisha nikaangalia Hawa wanaotuhumiwa kwa uhaini hivi sasa. Nikajiuliza je ni kweli kwa hadhi Yao wanaweza kufanya uhaini? Nikajijibu " hapana"

Nasadiki kusema kwamba toka nianze kujitambua na kufuatilia siasa toka awamu ya pili ya mkapa mpaka sa100 sikuwahi kusikia Mtanzania akifunguliwa kesi ya uhaini zaidi ya Hawa Wenzetu waliofunguliwa hivi sasa.

Nimezoea kusikia Watanzania wakifunguliwa kesi za UGAIDI lakini si uhaini. Uhaini kosa la juu mno ambalo kwa akili yangu halipangwi wala kutekelezwa na waomba mungu Bali hufanywa na

1. Top government officials
2. senior or top military officers
3. Business tycoon but in coordination with others.

Mwl.nyerere aliwahi kumbana na watu wa namna hiyo wakiwemo akina marehemu Zacharia Hanspope na wengineo kama Bibi Titi.

Leo hii mdude na mwabukusi. Hawa ni raia waomba Mungu tu. Kweli wanaweza kufanya uhaini? Odinga na Martha pale Kenya wameendesha maandamano ya watu maelfu lakini hawajafunguliwa mashtaka kama hayo. Sisi huku tunaziba vijana midomo kwa vitisho vya uhaini. Kweli?

Wakae gerezani mwaka Kisha watolewe kwa jamhuri kukosa ushahidi au mwendesha mashtaka Hana Nia ya kuendelea na kesi hii.

Je Nini faida yake? Wewe unayefanya hivyo ama kwa makusudi au kwa maelekezo toka juu mwisho wako ni upo?

Kwanini serikali inahofu na wakosoaji.? Si mliridhia demokrsia Tena kwa mikataba lukuki?

Je mnataka tuwe na taifa la mazuzu ambao kila kitu kinafanywa waseme mama anaupiga mwingi?? Hapana.

Mimi nasema hapana. Mtawanyamazisha midomo Yao lakini hamtanyamazisha fikra zao.

Hiki mnakifanya leo siyo cha kwanza na walishafanya wengi lakini mwisho wao ulifika.

Nani anamkumbuka Mobutu,Idd Amin na Bokasa?

Nchi yangu, " unaweza kuwadanganya watu kwa nyakati tofauti lakini huwezi kuwadanganya watu wote kwa wakati mmoja"
ndugu naweza pata wapi hivyo vitabu vya nyerere vinavyohusu yaliyomkuta.
 
Kwanza tuanze kupata tafasiri ya neno uhaini.
Uhaini
ni pale mtu anapotenda jambo dhidi ya nchi yake. Kwa mfano, mtu anaweza kuisaidia nchi nyingine ipigane vita dhidi ya nchi yake kwa kutoa habari za siri.
Uhaini ni neno la kawaida, lakini nchi tofauti zina sheria na adhabu tofauti dhidi ya matendo ya kihaini, hata adhabu ya kifo.
Miongoni mwa wahaini maarufu duniani kuna Yuda Iskarioti, Benedict Arnold, Philippe Petain  na Vidkun Quisling.
Jibu ni:
Ndio muomba Mungu anweza akafanya uhaini pia.
 
Kwanza tuanze kupata tafasiri ya neno uhaini.
Uhaini
ni pale mtu anapotenda jambo dhidi ya nchi yake. Kwa mfano, mtu anaweza kuisaidia nchi nyingine ipigane vita dhidi ya nchi yake kwa kutoa habari za siri.
Uhaini ni neno la kawaida, lakini nchi tofauti zina sheria na adhabu tofauti dhidi ya matendo ya kihaini, hata adhabu ya kifo.
Miongoni mwa wahaini maarufu duniani kuna Yuda Iskarioti, Benedict Arnold, Philippe Petain  na Vidkun Quisling.
Jibu ni:
Ndio muomba Mungu anweza akafanya uhaini pia.
Kwenye sala ya toba tunaomba kusamehewa makosa yetu ya kuwaza na kutenda. Wakati fulani Bwana mmoja aliyekuwa mbunge wa Arumeru alimpiga mkwara Rais wa nchi kuwa aishie Pwani asifike Usa- River, ooh mama yangu aliponea chupuchupu kupata hiyo kesi mbaya, unapomtangazia Rais roadblock maana yake una intention ya kumdhuru , matamshi ambayo yanaunda treason offence. Lazima kuwa makini kuchagua maneno ya kuzungumza.
 
Back
Top Bottom