Je, Ulimwengu Umepoteza Mwelekeo? Au La.

Je, Ulimwengu Umepoteza Mwelekeo? Au La.

Mtayarishaji

JF-Expert Member
Joined
Jan 25, 2012
Posts
291
Reaction score
198
MWANZONI mwa mwaka wa 2017 wanasayansi walitoa tangazo lenye kuogopesha. Mwezi Januari, kikundi cha wanasayansi kilitangaza kwamba ulimwengu umekaribia kupatwa na janga kubwa zaidi kuwahi kutokea.

Wakitumia Saa ya mfano ya Maangamizi inayoonyesha jinsi wanadamu ulimwenguni pote wanavyokaribia kuangamia, wanasayansi walisogeza mbele mshale wa dakika wa saa hiyo kwa sekunde 30. Saa hiyo inaonesha kwamba sasa hivi bado dakika mbili na nusu tu kabla ya saa sita usiku, kumaanisha kwamba ulimwengu umekaribia sana kuangamia kuliko wakati mwingine wowote kwa zaidi ya miaka 60 iliyopita!

Mwaka wa 2018, wanasayansi wanapanga kufanya uchunguzi tena ili kuona tumekaribia kwa kadiri gani mwisho wa ulimwengu.

Je, Saa ya Maangamizi bado itaonyesha kwamba tumekaribia janga kubwa ambalo halijawahi kutokea?

Una maoni gani?

Je, ulimwengu umepoteza mwelekeo?

Huenda swali hilo likaonekana kuwa gumu kwa sababu hata wataalamu wenyewe hawakubaliani kuhusu jambo hilo. Si kila mtu anayeamini kwamba kuna siku isiyoepukika ya maangamizi.

Kwa kweli, mamilioni ya watu wanaamini kwamba kutakuwa na maisha mazuri wakati ujao. Wanasema kwamba wana uthibitisho unaoonyesha kuwa wanadamu na dunia yetu itadumu milele na kwamba maisha yetu yataboreka.

Je, uthibitisho huo unaaminika?

Je, ulimwengu umepoteza mwelekeo au la?



“Saa ya Maangamizi ni mchoro wa saa unaotambuliwa ulimwenguni pote ambao unaonyesha jinsi tunavyokaribia kuharibu kabisa mfumo wa maisha duniani kupitia vifaa hatari vya kisasa tulivyobuni sisi wenyewe. Silaha za nyuklia zinachukua nafasi ya kwanza, lakini vitu vingine hatari vinatia ndani vifaa vya kisasa vinavyoharibu hali ya hewa, teknolojia za kibiolojia, na teknolojia za intaneti ambazo zinaweza kuisababishia dunia na wanadamu madhara ya kudumu, iwe ni kwa kukusudia, au kimakosa.”— Bulletin of the Atomic Scientists.
 
Badili kichwa cha habari neno ulimwengu weka dunia.. maana ulimwengu ni mjumuiko wa kila kitu kwenye space.. ambavyo ni galaxies,stars,planets,pamoja na wewe n.k.
kupotea kwa mwelekeo wa dunia si kupotea kwa mwelekeo wa ulimwengu!,maana dunia kwenye ulimwengu ni kama tone kwenye bahari.
 
Tofautisha Dunia na Ulimwengu ili ionyeshe uelewa japo wa ulichokiandika
 
ungeweka ht link ili wengine wenye vchwa vzito tujisomee hio taarifa ya wanasayansi maana cjaelewa hayo mambo km silaha za nuclear na biolojia zilizopo ndani ya sayari moja tu ya dunia yana nguvu gani kiasi cha kusababisha mwsho wa ulimwengu huu ambao una mabilioni ya sayari na nyota
 
Back
Top Bottom