Lamar BlacAmerican
JF-Expert Member
- Aug 9, 2013
- 974
- 2,305
Oya ngaillo malizia hii1997 Vi-form 1 wenzangu wananitambia kuiona movie ya PREDATOR (Anorld ya jini) kwenye kibanda umiza,nikailaani sana mifugo (mbuzi)waliosababisha niwe malishoni wakati wenzangu wako wanafaidi mikwara ya akina BILLY DUKE...ikapita kama wiki hivi hiyo muvi ikawa inaoneshwa tena ila bahati mbaya inawekwa usiku kuanzia saa 4 mara tu baada ya trela la Alain Kounkou....
Home- ruhusa kama hiyo sahau kupewa (kutembea usiku?!)....nikajiapiza kutoikosa siku ya leo hata iweje,....Ili nifanikiwe lengo mzee nikalihujumu dirisha la chumbani kwangu kwa kung'oa nondo moja ili nipate pa kutokea pale familia nzima ikiwa imelala...
Saa 3 tayari raia wote wanakoroma,starling nikalinyatia dirisha nikajikuta niko nje,...ndani ya dk 5 nikawa nimejumuika na watu wazima holini tunamalizia album ya R.A.S (Alain) ili muvi lianze...muvi likaanza, muvi likaisha,nikaridhika...
Kutoka nje giza totoro....njia ya kwenda home mwendaji ni mimi tu,sina kampan coz tulikuwa tunakaa kwenye kota za shule alafu zimejengwa mbali na kijiji (Kunaitwanga Mahuta-Mtwara)...
Kijiji usiku huu kiko kimyaa,nyayo zangu tu ndo zinatoa sauti...kuna kipande cha msitu kinachotenganisha eneo la shule na hiki kijiji (hilo ndo eneo pekee nililolihofia kabla hata sijalifikia)....sasa wakati nazimalizia hizi nyumba za mwisho-mwisho ili niukabili huu msitu,mita kama 7 hivi kulia kwangu,kati ya nyumba moja na nyingine (zote zimeezekwa kwa nyasi) nikaona kundi la watu wako uchi,wako wima, wametengeneza kamduara hivi,wako kimya...BWANA BWANA wee...
Kuna kitu kama shoti ya umeme hivi iliyonifanya mwili,nywele visisimke kwa pamoja na nikauona mwili kama hauko na mimi vile...huku nikiwa nimesimama,moyo unataka utoke nje kwa mapigo ya KUDU-KUDU,nikiwa sijui la kufanya maana lile kundi nahisi lilikuwa bado halijaniona 'mwana mzurura usiku'... (vyote hivyo ni ndani ya kama sekunde 5 hivi)...
Mara kwa pamoja (utadhani waliambiana) kundi lote lile wakageuza vichwa vyao na kunitazama fwaaa......
Nakumbuka nikasema "Mawee" bila kutoa sauti (nikijua saasaa nyama ya mtoroka kwao inaenda liwa punde) na kufuatia na mbio za kukimbilia vidole/kama sio kucha pasipo kugeuka nyuma...nyumbani nikapitiliza,mbwa wa home akaanza kubweka na yeye akaniungia tela kimyakimya akijua tunacheza,nikajua hapa naenda chaka,nikageuza...mbio hadi dirishani...sikujali nani atasikia ninavyoingia au lah,...narukia dirishani,mbwa naye anavuta suruali kwa chini(huyu dog alikua best angu sana)baada ya zile kukuru-kakara za kuingia ndani...nikajikuta niko kitandani nahema kwelikweli, tena kwa nguvu,koo limekauka, huku mguu mmoja unaning'inia dirishani suruali inaendelea kuvutwa na mbwa nje......
Sent from my TECNO-C9 using JamiiForums mobile app