Je, umemaliza chuo na unataka ujiajiri?

Je, umemaliza chuo na unataka ujiajiri?

David M Mrope

Senior Member
Joined
Jul 13, 2021
Posts
115
Reaction score
74
Mhitimu wa chuo kikuu ni mtu mwenye elimu ya juu kulinganisha na sehemu kubwa ya jamii. Hawa watu wanakitu cha kipekee japo wengi wao wamefumba.

Sasa haya ndio mambo makuu,ya kukusaidia ujitambue na ujiajiri.

👉TENGENEZA NJIA YA ZIADA KATIKA MAISHA.
Hii ni hatua ya kwanza kabisa,jaribu kuwaza ukiacha elimu uliyonayo kipi kingine unaweza ukakifanya?. Hapa ondoa wazo la biashara kwanza.

👉TAFUTA UJUZI KATIKA NJIA YA ZIADA ULIYOICHAGUA.
Hiki ni kitu cha lazima. Kabla hujaanza kuvamia hiyo njia ya ziada basi tafuta ujuzi. Kama ni umeme nenda vyuo vya umeme ukapate hata cheti cha mafunzo ya muda mfupi.

👉JIAJIRI KATIKA HIYO NJIA YA ZIADA.
Sasa baada ya kujipatia ujuzi wako vizuri,basi sasa unaweza ukajiajiri. Mfano kama umepata ujuzi wa muda mfupi wa umeme basi utaendelea na ufundi huo muda wowote na mahari popote.

🌺🌺🌺
Usikimbilie kuanzisha biashara wakati hauna ujuzi wowote katika maisha yako.

DAVID M MROPE.
SUA.
 
Kwa kawaida tumezoea mwanafunzi wa chuo anapohitimu ni kusubiri ajira, lahasha!

Ukiachilia mbali kuajiriwa, suala la kujiajiri ndilo limewainua watu wengi na kupiga hatua kubwa kwa mfano, katika historia ya mabilionea duniani wengi wamejiajiri
Kweli kabisa,uko sahihi sana.
 
Back
Top Bottom