Je, umeshindwa kudhibiti matumizi yasiyo ya lazima?

Je, umeshindwa kudhibiti matumizi yasiyo ya lazima?

Pantosha

JF-Expert Member
Joined
Sep 22, 2022
Posts
640
Reaction score
958
Mimesikia mara nyingi tu watu wakisema hawawezi kutunza pesa zao au hawajui hata inaishaje. Wengine wanaweza kusema kuwa pesa ina majini ndiyo maana hawaelewi hata inavyoisha.

Njia moja nzuri ya kudhibiti matumizi yasiyo ya lazima na kujuwa vizuri namna unavyotumia pesa zako ni KUANDIKA KILA SENTI INAYOTOKA MFUKONI MWAKO. Unapofanya manunuzi yoyote, andika. Unapotoa sadaka, andika. Unaposaidia mtu, andika.

Nakuhakikishia siku ukianza kuandika matumizi tu, utaanza pia kujifunza namna ya kudhibiti pesa yako. Hii ni kutokana na ukweli kwamba, ukijua tu namna unavyotumia pesa yako, utaanza kujiona wewe ni mtumiaji wa pesa wa namna gani.

Nakutakieni siku njema.
 
Nakuhakikishia siku ukianza kuandika matumizi tu, utaanza pia kujifunza namna ya kudhibiti pesa yako. Hii ni kutokana na ukweli kwamba, ukijua tu namna unavyotumia pesa yako, utaanza kujiona wewe ni mtumiaji wa pesa wa namna gani.
Subutuu nimejaribu nimeshindwa aiseeee. Kuna apps nimejaribu kuzitumia bado nimeshindwa kabisa!
 
Mimesikia mara nyingi tu watu wakisema hawawezi kutunza pesa zao au hawajui hata inaishaje. Wengine wanaweza kusema kuwa pesa ina majini ndiyo maana hawaelewi hata inavyoisha.

Njia moja nzuri ya kudhibiti matumizi yasiyo ya lazima na kujuwa vizuri namna unavyotumia pesa zako ni KUANDIKA KILA SENTI INAYOTOKA MFUKONI MWAKO. Unapofanya manunuzi yoyote, andika. Unapotoa sadaka, andika. Unaposaidia mtu, andika.

Nakuhakikishia siku ukianza kuandika matumizi tu, utaanza pia kujifunza namna ya kudhibiti pesa yako. Hii ni kutokana na ukweli kwamba, ukijua tu namna unavyotumia pesa yako, utaanza kujiona wewe ni mtumiaji wa pesa wa namna gani.

Nakutakieni siku njema.
Kabisa.....siku pesa imekwisha....rudi soma ulichoandika....ndio utajojua u mtu wa aina gani😃😀😃
 
Pamoja na kuandika, wengi wetu Mipango ya kupata fedha huwa inakuja Tu. Yaani ukipata Tu fedha, Muda huohuo simu na SMS zinaanza. Utasikia wagonjwa, misiba na maombi Tele. Na ulisema utunze ndio itaisha yote kuisolve udiyopanga. Naamini zina ushetan flan hivi
 
Pamoja na kuandika, wengi wetu Mipango ya kupata fedha huwa inakuja Tu. Yaani ukipata Tu fedha, Muda huohuo simu na SMS zinaanza. Utasikia wagonjwa, misiba na maombi Tele. Na ulisema utunze ndio itaisha yote kuisolve udiyopanga. Naamini zina ushetan flan hivi
Hahaha 🤣
 
Pamoja na kuandika, wengi wetu Mipango ya kupata fedha huwa inakuja Tu. Yaani ukipata Tu fedha, Muda huohuo simu na SMS zinaanza. Utasikia wagonjwa, misiba na maombi Tele. Na ulisema utunze ndio itaisha yote kuisolve udiyopanga. Naamini zina ushetan flan hivi
Ni Jambo jema kusaidia. Ukianza kuandika hayo matumiza hata unaposaidia, mwisho wa siku utaanza ku control hata hiyo pesa inayoenda kwa ndugu na jamaa. Nasisitiza andika tu matumizi yako kila siku.
 
Ni kweli. Ila kwa leo nakumbusha tu umuhimu wa kuandika/kurekodi matumizi. Wew ni starehe fanya ila kumbuka kuandika umetumia kiasi gani. Kama unajiona maskini, sawa ila andika umetumia kiasi gani.
Misiwezi mkuu, nafikiri kuna vitu ambavyo watu wenye majukumu hatuwezi kufanya haki
 
Kwa kuwa moyo wako umekiri hauwezi, basi kweli huwezi.
 
Back
Top Bottom