Je, umri ulionao una tafsiri gani na maisha uliyonayo?

hapa umezungumzia mafanikio ya kiuchumi

sidhani kama kuwa na kiwanja ni mafanikio, kuwa na hela ya kununua kiwanja muda wowote ndo mafanikio

ukizeeka unaweza kufanikiwa ila ngumu kwasababu muda unao kidogo

hiyo ya kuandikiwa inategemea na imani, ila naona hata wanaoamini ni wanafki kwasababu wakipitia changamoto wanasema 'pambana na umtangulize mungu utatoboa' wakishindwa kutoboa utasikia 'kila mtu na riziki yake' au 'mungu anakupa unachostahili'
 
Hakuna billionaire hapa bongo mwenye umri chini ya miaka 40 katika ile Top 10 ..Mafanikio yanachukua muda ila haijalishi utayapata ukiwa na umri gani.

Kidunia pale kweny List labda Marck Zuckerberg ndio mdogo ,wapo wenye miaka mpaka 80's still wanapiga kazi.

Vijana wengi mnapagawa na hawa wapiga kelele ,bado watoto hao ndio maana hata Top ten pale bado ,
 
Haya mambo yapo Bongo na nchi za kusadikika tu.

Mungu alishatubariki wote tangu kuzaliwa, hata ukiona kichanga kinakufa hiyo si kazi ya Mungu, ni kazi ya shetani.

Inshort Kwa Bongo umri wa kujipata ni miaka 50, ukijipata mapema kabla ni network yako tu ni nzuri.

Halafu kujenga ni mawazo ya watu waoga, wahindi wanamiliki viwanda lakini hawana nyumba, ukifanikiwa kutoka nje ya bara la Giza ndio utagunduwa maana ya apartment ni nini, kimsingi unachotakiwa kuwa nacho ni uhakika wa kipato tu vingine vyote vinaletwa na pesa.
 
Yule founder wa KFC ametobowa uzeeni.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…