Je, unaamini kuwa uchawi upo?

Je, unaamini kuwa uchawi upo?

uwe na dini usiwe nayo uchawi upo hata kwenye kitabu kitakatifu umezungumziwa
 
Neno uchawi aslil yake ni Biblia, maana halisi ni kuufanyia mwili yale yaliyokinyume na kawaida na hatimaye yakauletea mwili maumivu, mauti, kuvuruga akili au ulemavu. Hivyo basi hata kama umewahi kutoa mimba, kuua mtu, kufamfamyia mtu operesheni (kwa madaktari), kumpa dawa yeyote ikamdhuru mtu huyo, kumfukuzisha kazi mtu kwa majungu, kutoa/ kupokea rushwa, kudanganya, na kama hayo, jihesabie wewe ni mchawi. Haijalishi unatumia gitaa chupa ya pombe, biblia au mazingira gani. GOOD DAY.
 
Wakati nafanya research moja niligundua kuna viongozi wengi wa serikali huwa wanakimbilia kwa watu wanaojiita waganga sijui huwa wanaenda kuchawia au kujikinga me do not no ?
Ili waweze kupita kwenye chaguzi mbali mbali ,
Mie nadhani upo ila inategemea na imani yako
 
Lakini dini inafahamika na ndio maana nikikashfu dini ya mwenzangu nitachukiliwa hatua za kisheria, lakini kama nikutishia kukuroga sichukuliwi hatua yoyete.

Uchawi nao ni imani kama zilivyo nyingine. Na muumini wa uchawi huwezi ukambadilisha imani yake hiyo kwa urahisi. Suala jingine ni kuwa kuna watu wanajitambulisha kuwa wakristo ama waislam lakini pia ni waumini wazuri sana wa uchawi. Mambo yanapoharibika kidogo tu hukimbilia kwa waganga (siyo kwa mungu) kupata majibu ya matatizo yao. Hivyo wanatumia hizi dini za kigeni kujitambulisha tu wasionekane ni watu wa ajabu kwenye jamii (for PR purposes) lakini ndani ya mioyo yao ni waumini sugu wa uchawi.
 
Uchawi hakuna,bali kuna imani za uchawi. Na ukizi puuza na kumuamini Mungu,hakuna cha kukutisha wala kukudhuru.
dah!mkuu mbonaa na sikiaa huwezi kumuona kwa macho ya kibinadamu mchawii..au na wewee umeangaa kwenu banaaa
 
Uchawi hakuna,bali kuna imani za uchawi. Na ukizi puuza na kumuamini Mungu,hakuna cha kukutisha wala kukudhuru.

Sawa kabisa Mkuu , na hili linaambatana na self confidence.Kama mtu hajiamini kwa lolote basi imani yake anaiweka sehemu nyingine kuiponyesha nafsi yake.
Imani yako iwe kwa Muumba wa yote.
 
kwani serikali ni nini? Inakuwaje serikali haiamini katika dini lakini viongozi wana dini? Haya yakipata majibu, hata la uchawi majibu yatapatikana

serkali ni collectivenrss ya watu waliopewa nyazifa na mamlaka ndio maana hata mawaziri/makatibu, wakuu wa mikoa na wilaya hua hawasemi "mimi" bali husema "serikali" kama wakiwa wana adres jambo fulani.sasa tunaposema kua serikali ni collectiveness ya hawa watu inamana hawa watu kuna wakati hua wao sio serikali pale wanapokua katka masuala binafsi.
Inapokuja sasa katika masuala kama haya ya dini na uchawi kila mmoja ana haki ya kuamua nini cha kuamini na nini sio.
la si hivi basi kungekua na sharti kua kila anaeunda serikali basi asiwe na dini wala asiamaini katika uchawi.
 
Siku nyingi nimekuwa siamini kama kweli kuna uchawi katika Tanzania hii, achilia mbali huko kwa wengine. Nimekuwa siamini kwa sababu makosa yote hapa nchini yana adhabu zake isipokuwa la uchawi hii ikimaanisha kuwa Serikali inaamini kuwa hakuna uchawi. Hatahivyo, siku za hivi karibuni imani yangu imeanza kupungua baada ya Kiongozi mmoja katika Serikali hiyo hiyo inayoamini kuwa hakuna uchawi kudai kuwa amegundaua mbinu kuwa anarogwa ili awe zoba auwawe kirahisi. Sasa nikajiuliza, huyu mtu yumo ndani ya Serikalini inayoamini kuwa hakuna uchawi, akiwa pekee yake kuna uchawi, inakuwaje hapa?

Aidha, jana tarehe 28/03/2011 nilikuwa nasikiliza Redio Wapo FM kuanzia saa 1.30 jioni kipindi cha “yaliyotufikia” nikasika kuwa kuna fisi ameshambulia watu huko Mto wa Mbu, akauawa na askari wa wanyama pori, baada ya kuuawa, wakakuta ametobolewa masikio kama alikuwa anawekewa hereni.

Je, huyu fisi alikuwa anashiriki mashindano ya “Miss Mto wa Mbu” au ni fisi wa wachawi?

Sasa wana JF wenzangu ni kweli kuna uchawi? Au ni njama za wajanja kutishia wenzao.

Uchawi upo ila hauna nafasi kwa mtu asiyeauamini, ni kama sumaki south na north, south kwa north kitu mwake ila south kwa south au north kwa north hata siku moja. Kwa hiyo ukianza tu kuogopa ukaambiwa katundike hii au vaa hiki, ujue umefunga bendera (antena) kuwaambia nipo hapa
 
Ushirikina (ambao ni dhana tu kama vile kuamini siasa ya "ujamaa na kujitegemea" (sic!)) upo.

Uchawi (ambao ni attempt ya ku-tangibilize ushirikina) haupo na haufanyi kazi.

Search me!
 
Wakati nafanya research moja niligundua kuna viongozi wengi wa serikali huwa wanakimbilia kwa watu wanaojiita waganga sijui huwa wanaenda kuchawia au kujikinga me do not no.
Ili waweze kupita kwenye chaguzi mbali mbali ,
Mie nadhani upo ila inategemea na imani yako


hapo kwenye nyekundu ulitaka kumaanisha nini?
 
uchawi pamoja na imani nyingine zote supernatural ni fix tupu.
 
Hiyo ni sehemu ya mazingaombwe na mauza uza ya kukufanya uamini kuwa kweli uchawi upo. Lakini mwenye akili ya ukweli ulivyo hawezi kutishika eti kwa sababu mtu kachukua viungo vya uzazi vya mnyama. Unaweza kweli kulitumia hili kama kithibitisho cha kuwepo kwa uchawi? Samahani, naona tuko kwenye viwango tofauti mno vya uelewa wa mambo na itakuwa vigumu kueleweshana ikiwa haya ndo madai ya kuthibitisha kuwepo kwa uchawi.

Uchawi ni dhana. Ni dhana inayoishi na watu. Ziko dhana nyingi sana zinazoishi na watu hadi leo. Hata mira nyingi na desturi ni dhana tu ambazo zimejijenga kwa muda mrefu. Nyingine zina sababu za msingi, nyingine hazina sababu yoyote..

Jamani nawakaribisha huku uswazi mjionee .Uchawi umekua kero kubwa huku ni kawaida watu kuona wazee waliofariki maeneo ya chooni,kelele za wanyama ambazo zinafanana na sauti ya binadamu,watu kukabwa usiku ,kuugua magonjwa ambayo hospitalini hayaonekani na kadhalika.
 
Uchawi upo japo umekaa kiimani zaidi. Na inategemeana na imani yako katika kuukabili. Ndio maana unatibika kutegemeana na imani yako. Wapo wanaotibu uchawi kwa uchawi. (Wakipatwa na kitu chochote kibaya, basi anajua amelogwa anachapa mbio kwa mganga wa kienyeji). Wapo wanaotibu kwa kumuomba Mungu wa Kwenye vitabu vya dini (Maana kuna mungu wengi ndio maana Mungu wa kwenye biblia aliwaambia watu wake kuwa "Mimi ni Mungu mwenye wivu, Usiabudu miungu wengine") kwa kuwa alisha waambia kuwa yeye ni tabibu vilevile, Wapo wanaotibu na sayansi (Wakiugua hata ngoma wanatoka nduki hospitali hata kama anajua hakuna dawa ya kutibu ugonjwa huo zaidi ya kupunguza maumivu na kununua visiku vichache, hata kama hospitali hawaoni kitu s/he will keep on changing hospitals. kwa sababu haamini kama kuna altenative nyingine. Wapo wanaochanganya approach zote tatu katika kupambana na uchawi. (Hawa ndio wengi sana katika jamii yetu ya leo). wanafanya trial and error itakayokubali ndio hiyo hiyo. Mfano mzuri ni samunge na matukio yanayofanana.

Hii inapelekea hata kuamini uchawi kuwa unaweza hata ukakufanya upate maisha mazuri kwa njia ya mkato. Mfano mzuri ni mauaji ya albino, kuchunana ngozi, watu kupotea katika mazingira ya ajabu ajabu, wengine waliokufa miaka mingi halafu wakaonekana wazima. kwa namna ya kinyume chake wapo wanaoamini kuwa wanafanyiwa uchai ili mambo yao yasiwanyookee, waharibikiwe katika maisha au hata waondolewe duniani kabisa. Hata hivyo (kwa maoni yangu) kuna uhusiano mkubwa sana kati ya uchawi na kinachoitwa NGUVU za Giza. Vile vile nashawishika kuamini kua uchawi yawezekana ni sayansi fulani ya ujanja ujanja kwa ajili ya kujipatia kitu: iwe ni umaarufu, nafuu ya maisha, nk. Mfano ni hii kitu ya Mazingaombwe, naona kama ni nadharia hiyo hiyo ya uchawi uliovishwa joho zuri.

Nawasilisha!!!
 
Agalia wakati mwingine spelling zaweza kuaribu maana ya kile ulichokusudia. Hebu hii " akawauwa na askari wa wanyama pori, baada ya kuauwa, wakakuta ametobolewa masikio kama alikuwa anawekewa hereini" Hii haijatulia.

Na wewe hapo penye red pia umepindisha neno sahihi ni kuuawa
 
Back
Top Bottom