mkuu usicomment tu bila kuwa na elimu ya kutosha juu ya unachokicomment, infact uchawi upo uwe na imani ya kikiristo au kiislamu hzo dini zote zmethbitixa kT
uwepo kwa uchaw
cc Free ideassiku nyingi nimekuwa siamini kama kweli kuna uchawi katika tanzania hii, achilia mbali huko kwa wengine. Nimekuwa siamini kwa sababu makosa yote hapa nchini yana adhabu zake isipokuwa la uchawi hii ikimaanisha kuwa serikali inaamini kuwa hakuna uchawi. Hatahivyo, siku za hivi karibuni imani yangu imeanza kupungua baada ya kiongozi mmoja katika serikali hiyo hiyo inayoamini kuwa hakuna uchawi kudai kuwa amegundaua mbinu kuwa anarogwa ili awe zoba auwawe kirahisi. Sasa nikajiuliza, huyu mtu yumo ndani ya serikalini inayoamini kuwa hakuna uchawi, akiwa pekee yake kuna uchawi, inakuwaje hapa?
aidha, jana tarehe 28/03/2011 nilikuwa nasikiliza redio wapo fm kuanzia saa 1.30 jioni kipindi cha yaliyotufikia nikasika kuwa kuna fisi ameshambulia watu huko mto wa mbu, akauawa na askari wa wanyama pori, baada ya kuuawa, wakakuta ametobolewa masikio kama alikuwa anawekewa hereni.
je, huyu fisi alikuwa anashiriki mashindano ya miss mto wa mbu au ni fisi wa wachawi?
sasa wana jf wenzangu ni kweli kuna uchawi? au ni njama za wajanja kutishia wenzao.
kama upo tunashindwa kutumia fursa ya uchawi kujiendeleaze??!Uchawi upo....vitabu vya dini vinatambua hlo....
ni vitu vingi tu havipo lakini misamiati yake ipo,,,,kwa mfano neno sifuri au zeroUsingekuwepo hata huo msamiati (uchawi) usingeusikia
Asili ya uchawi ni shetani mwenyewe ......Shetani hawezi kujifitini ......umeona wapi ufalme ukijifitini?.....Hivyo Kuroga Boko Haram ambao ni kazi ya shetani pia ni sawa na shetani kujifitini ......Umewahi kusikia mchawi akimroga chizi ? Kwa faida ipi kwa shetani?
Mtu anakurupuka na kudai uchawi haupo kwa sababu sayansi imeshindwa kuthibitisha wakati anajua kabisa sayansi hiyo hiyo inakiri kuna isiyoweza kuyajua
Watu wengine wa ajabu sana!
uchawi upo tena sana, lakini kufanikiwa kuleta madhara hutegemea imani na hofu ya mlengwa. Usipokuwa na imani ya kudhurika nao hutalogeka abadan.
Uchawi ni imani muflis kuwa watu fulani wana nguvu fulani yenye uwezo wa kudhuru wengine. Hili jambo ni imani tu na imani hizo zimejikita katika jamii kweli kweli. Hao waliokuwa wakiitwa au wanaoitwa wachawi katika jamii huwa ni watu dhaifu sana, maskini na waoga wanaodharauliwa sana na jamii. Mara nyingi watu hao wakiitwa wachawi, hawakatai wala kukubali, kwani wengine hufikiria kuwa watu wakimuona ana nguvu hiyo ya ajabu (yaani uchawi) itakuwa ni sababu ya kuheshimiwa na kuogopwa.
Wengi wao hujiingiza katika matendo ya kufanya viinimacho au mazingaombwe ya kuwasadikisha watu kuwa wao kweli wanazo hizo nguvu na wana uwezo wa kudhuru. Kutokana na hilo, wakazaliwa watu wanaoitwa wachawi au walozi. Hawa watu wameanzisha utamaduni wao, kama zilivyo dini. Tofauti yao ni kuwa wao mambo yao hufanyika kwa siri, kwani lengo ni kuwadanganya watu waamini kuwa kweli wanazo nguvu za ajabu.
Hizi jamii za kichawi, kama secrete societies zingine hutoa sadaka na kufanya vitimbi vya hapa na pale vyenye lengo la kuwaaminisha watu kuwa wao wana nguvu zisizoonekana.
Lakini ukweli ni kuwa kama zilivyo jamii zote za siri, mambo haya yanagundulika na walio wengi kuwa si kweli. Wale wanaodanganyika wanabaki kuishi kwa hofu na wakati mwingine enzi hizo watu walilazimika kutoa kitu kidogo kwa wachawi ili wasirogwe. Huo ndo uchawi.
Ukiogopa vitimbi vyao, utajisalimisha kwao na kuwapa kitu kidogo ili wakulinde na uchawi.
Jamii ya wachawi ina umri mrefu kuliko hata dini zetu nyingi, ambazo nazo zimetumia mbinu kama zile zile wanazotumia wachawi kupambana nao. Mbinu wanayotumia wachawi ni kutangaza uwezo wa kudhuru watu kwa kutumia "magic". Dini zinatumia "nguvu za kimungu" kupambana na wachawi. Nguvu zote hizo ni 'supernatural'.
Kwa mtu mwenye scientific knowledge ya mwili wa binadamu na mazingira yake, uchawi ni kama hadithi za riwaya kwake na hauna madhara yoyote!
Huo ndo uchawi!
Basi fanya hivi;Mtu anakurupuka na kudai uchawi haupo kwa sababu sayansi imeshindwa kuthibitisha wakati anajua kabisa sayansi hiyo hiyo inakiri kuna isiyoweza kuyajua
Watu wengine wa ajabu sana!
ni vitu vingi tu havipo lakini misamiati yake ipo,,,,kwa mfano neno sifuri au zero
Sifuri ipo... (mfano kwenye sh. 100,000,000 zipo sifuri 8)
Basi fanya hivi;
Anza kuamini tafiti tu za kawaida ambazo ni wazi kuwa wafanya tafiti hawana sababu za kudanganya.
Hivyo basi tafiti hizo zinaweza kuaminiwa.
CNN wamefanya utafiti na kugundua kuwa asilimia 97 ya watanzania wanaamini ushirikina, nchi zingine za Afrika mashariki zikiwemo Rwanda na Burundi ni chini ya 50% ndiyo wanaamini mssuala ya uchawi.
Utafiti pia ukaonyesha kuwa ni 20% tu ya watanzania ndio wamefikia elimu ya sekondari, Kenya ni 70% ambapo uganda ni 50%, Rwanda ni 40%.
Nakupa tafiti hizi ili ugundue kitu, imani za ushirikina zinaenda sambamba na ukosefu wa elimu.
Asilimia kubwa ya watu wadio na elimu hawaezi kureason, hawawezi kujua sayansi, saikolojia, baiolojia, viini macho na kadhalika.
Ulishawahi kujiuliza ni kwa nini Ulaya na Marekani hakuna imani za ushirikina?, Albino hawakatwi mikono?
Ni kwa sababu asilimia kubwa ya watu wamepata walau elimu ya sekondari.