Je, unaamini kuwa uchawi upo?

Je, unaamini kuwa uchawi upo?

Mzungu kua mungu ni katika muktadha wetu wa neno kutoholewa na kupata neno jipya, siyo katika imani. Kila nilichoandika ni kuhusu neno tu wala siyo juu ya imani ya uwepo wa mungu.

Ni ama umenielewa vibaya au haujataka kuelewa nilichoandika.

Swala la racial pride kwangu halina nafasi, ninang'ang'ana na facts.
Kama lexicology inasema 'mzungu' inaweza kua 'mungu' huna budi kukubali kua 'mzunguka' inaweza kua 'mzungu'

Samahani kama unahisi tunajibizana lakini kama tutafunga mawazo yetu kwenye sources tutakua tunakataa baadhi ya facts.
Mfano Afrika tulikua/ tuko nyuma katika kutunza rekodi ni wazi kua hatutapata source ya hili neno kutokea Afrika.

Na ndiyo maana mimi sikujikita katika kukataa au kukubali ila nilionyesha jinsi utohoaji unavyoweza kuleta neno jingine.

Siku njema

Unasema unang'ang'ania facts. Hauko katika racial pride.

Unasema hutaki kufunga mawazo yako kuhusu source, kwa kuwa utakataa baadhi ya facts.

Unasema yote hayo baada ya ku discredit source yoyote kwa sababu source yoyote inaweza kuwa famba.

Unasema hutaki kufunga mawazo yako kuhusu source, baada ya kufunga mawazo yako kuhusu source.

Una ji contradict.

Sent from my Kimulimuli
 
mkuu nilipoona to hii thread nikasemaa hii lazma itakua kwetu kusini, kiukweli huko kwetu kuna uchawi sana yan, yan hata mm kiukweli nimejenga tabia ya kufananisha tukio lolote linalotokea katika hali ya kawaida na uchawii,, watu wanalogana sana songea, watu wanatajrika sana kwa uchawii, watu wengi wanautajiri wa nyoka kama unakumbuka miez c mingi watu waliua nyoka na mtu wake huko kwetu songea, so uchawii upo na ni kawaida sana kwa cc wakaz wa uko. Over
Wewe ni mkazi wa songea eneo gani mkuu

Sent from my TECNO-C9 using JamiiForums mobile app
 
Uchawi ni elimu ya nguvu za giza mkuu

critical thinker
Unaposema "elimu ya nguvu za giza" una maana gani? That is a vague statement.

Ushawahi kufanya uchawi wewe?

Sent from my Kimulimuli
 
Mtoa mada hapa utabishana na hawa jamaa mpaka basi. Wewe cha umuhimu ni bora ungeukamata huo uchawi ukauleta hapa Jf wasio amini waone!!!
 
Nimetoa link yenye etymology hapo juu.

Habari ya kuzunguka imekuwa treated as a joke, mwisho, baada ya mazungumzo ya mizungu.

Sent from my Kimulimuli

Wewe amini unachoamini.

Kwangu 'mzungukaji' ndo nadharia inayokubalika zaidi kwa sababu inaingia akilini.

Hiyo ya 'mizungu' hai make sense kabisa.
 
Sitaki kuamini, nataka kujua.

Kwenye hili kujua kwa uhakika ni vigumu na ndo maana unaona kuna maelezo tofauti kuhusu asili ya hilo neno.

Na hiyo hali ni ya kawaida sana katika lugha.

Hata kwenye lugha zingine maelezo kuhusu chanzo cha maneno flani flani huwa yapo kadhaa.

Kwa hiyo sishangai kuona neno 'mzungu' lina maelezo tofauti kuhusu chanzo chake.

Katika hali kama hiyo ni juu yako kukubali unachotaka kukubali.

Wewe umeyakubali maelezo ya 'mungu' na mimi nimeyakubali maelezo ya 'mzungukaji'.
 
Ngaja nimsomee babu

Sent from my TECNO-L8 using JamiiForums mobile app
 
Kwenye hili kujua kwa uhakika ni vigumu na ndo maana unaona kuna maelezo tofauti kuhusu asili ya hilo neno.

Na hiyo hali ni ya kawaida sana katika lugha.

Hata kwenye lugha zingine maelezo kuhusu chanzo cha maneno flani flani huwa yapo kadhaa.

Kwa hiyo sishangai kuona neno 'mzungu' lina maelezo tofauti kuhusu chanzo chake.

Katika hali kama hiyo ni juu yako kukubali unachotaka kukubali.

Wewe umeyakubali maelezo ya 'mungu' na mimi nimeyakubali maelezo ya 'mzungukaji'.
Hakuna jambo lolote linaloweza kujulikana kwa uhakika kabisa.

Hata nikikwambia hakuna jambo lolote linaloweza kujulikana kwa uhakika kabisa, hili nalo sina uhakika nalo kabisa.

Hivyo, inabidi tuchague acceptable framework, margin of error, axioms, assumptions etc.

Katika fizikia, Heisenberg's Uncertainty Principle inatukataza kujua position na velocity ya particle kwa uhakika at any one moment.

Kwa hiyo, katika nadharia angalau, tunatakiwa tusiweze kuendesha magari, kurusha ndege au hata kutembea.Kwa sababu mahesabu yetu hayana uhakika kabisa.

Lakini katika ukweli wa mambo, effects zozote za Heisenberg's Uncertainty Priciple hatuzioni katika maisha ya kila siku kwa sababu zipokatika quantum level, tukichagua kutengeneza ndege, kuendesha gari au kutembea, tunazipotezea tu effects za Heisenberg's Uncertainty Principle kwa sababu hazitajitokeza katika maisha yetu, ni kama hazipo. In fact watu wengi wanaishi maisha yao yote bilakujua habari hizi kwa sababu hawajazisoma, na wanaishi vizuri tu.

Kwa hivyo basi, watu wameandikakwa kuangalia kamusiza Kiswahili za miakaya takriban 1900, wakaona neno mzungu limetokana na "mizungu" wakaweka online, nimeweka link.

Wameongelea sana kwamba "mzungu" limetokana na "mizungu". Halafu mwisho kabisa wakawekaanecdote kwamba kuna watu wamefanya utani kwamba mzungu limetokana na kuzunguka.

Nadharia unayosema ndiyo hasa imeonekana ni ya utani tu.

Neno nililosemamimindilo limeonekana hasa.

Sijui kama umeona hiyo link.
 
mimi binafsi niliamini uchawi upo kutoka kwa rafiki yangu wa karibu sana.rafiki yangu huyo alihamia shule yetu baada ya kushindwa juishi na bibi yake huko Mombo,mkasa ulikua hivi
kwanza alikua anashangaa hajawahi kumuona bibi yake akipika kufua wala kufanya usafi na alikua mzee sana na wanaishi wawili nyumbani lkn kila siku nguo zake ni safi na anakuta amepikiwa akaanza kua na mashaka lkn bibi alimdanganya hua anafanya yeye mwenyewe kumbe anawatu wanakuja kimiujiza wafanya kazi,

siku iliyofanya akakimbia na kurudi kwa baba yake ndo akaletwa shule yetu ni baada ya kuchapwa sana na mwalimu fulani shule, alivorudi bibi akamuaona kama amechapa viboko vingi na vya maumivu sana, akamwambia huyu mwalimu jitamkomesha shost alijua ataenda naye shule kesho yake, imefika usiku sana wa manane akamgongea mjuukuu amabaye ndo huyo rafiki yangu kwamba njoo nikuoneshe kitu, binti akaamka kumsikiliza bibi akampeleka mpaka nyuma ya nyumba akamfunulia gunia akamwambia mwalimu mwenyewe ndo huyu, rafiki yangu akapata shok akasema ndio bibi ni yeye bibi akamjibu sana mlipizie alivokupiga akampa mtwangio ule mkubwa, akamwambia mpige mpaka hamu yake iishe,
 
kesho yake alivokwenda shule mwalimu hakumsemesha kitu lkn aliwaambia waambia waalimu wenzake wakaanza kumchukia huyo rafiki yangu, then yule mwamlimu aliomba uhamisho na rafiki yangu ahamishiwa shule ndo kukakutana akanipa huo mkasa
 
Nasikia wamemfanyia hiyo Magufuli Ikulu mpaka anataka kuhamia Dodoma.

Ila mimi siamini uchawi. Inawezekana ni sayansi isiyojulikana tu.

Nikupe mfano.

Ukimchukua mtu wa miaka ya 1600 huko, ukamuonyesha jinsi ndege inavyopaa, jinsi mawasiliano ya internet na redio yanavyofanya kazi,etc, halafu ukamwambia huu uchawi, most probably atakubali ni uchawi.

Kwa sababu kwake ni vitu vya ajabu.

Kumbe ni vitu vinavyoweza kuelezeka naturally tu,huhitaji supernatural powers kuvielezea.

Kuna muandishimmoja nampenda sana wa science fiction, anaitwa Arthur C. Clarke, alisema "Any sufficiently advanced technology is indistiguishable from magic".

Teknolojia yoyote iliyoendelea sana haitofautiani na uchawi.

Sasa mtajuaje mnachoita uchawi ni uchawi (i.e, supernatural powers) au ni kitu kinachotumia sayansi na teknolojia ambayo hamjajijua tu (i.e natural powers but unknown at the time) ?

How do you tell the difference?

Wale mababu zetu walioona wazungu wanajua kutabiri kupatwa kwa jua waliwaona wazungu wachawi (ndiyomaana wakawaita wazungu,wazungu maana yake ni miungu - ukichukua mzungu ukatoa z unapata mungu -).

Sasa tutajuaje kwamba tunachofikiri ni uchawi si sayansi tofauti tu ambayo hatujaijua?

If at all the suspicion is authentic.

Zile siku za mwanzo nasikia hakulala kabisa kwenye ile nyumba nyeupe..kulikua na mauzauza hatari
 
Nadharia unayosema ndiyo hasa imeonekana ni ya utani tu.

Imeonekana ni ya utani kivipi?

Hujui kuwa baadhi ya maneno hutokana na mtu au kitu kuwa cha aina flani na hapo neno kuhusu huyo mtu au hicho kitu ndo hutokea?

Hilo la mzungu kuwa mzungukaji nimelijua tokea nikiwa dogo kabisa.

Katika maongezi yangu na wataalamu wa lugha [ Prof. Herman Batibo....Google him....Msukuma huyo] kutoka idara ya lugha za kigeni na isimu ya chuo kikuu cha Dar, nadharia waliyokuwa wanaikubali zaidi ni hiyo ya 'mzungukaji' kwa sababu ilikuwa inaakisi uhalisia wa hao wageni waliokuja.

Soma kidogo kuhusu Batibo hapo Herman Batibo, University of Botswana

Hili la mzungu kuwa mungu hali make sense kwa sababu ilikuwa na bado inadhaniwa kuwa mungu haishi duniani. Anaishi mbinguni.

Hivyo mzungu hawezi kuwa mungu. Mzungu ni mzungu kutokana hali yake ya kuzunguka huku na kule tofauti na ilivyokuwa kwa wenyeji wa maeneo hayo ambayo wazungu walifika.
 
Zile siku za mwanzo nasikia hakulala kabisa kwenye ile nyumba nyeupe..kulikua na mauzauza hatari
Duh,kumbe na wewe umesikia hizo habari eenh?

Nasikia wakilala huwa wanajikuta wameamka nje.Kuna dogo mmoja wa Kikwete alijikuta kaamka na matope miguuni.

Lakini mimi upande mmoja nashindwa kuamini hizi habari kwa sababu siamini uchawi. Upande mwingine hizi strories ziko so consistent kutoka watu wenye first hand knowledge na Ikulu. I mean first families wenyewe kutokakwa Nyerere mpaka Magufuli wanasema haya mambo.
 
Imeonekana ni ya utani kivipi?

Hujui kuwa baadhi ya maneno hutokana na mtu au kitu kuwa cha aina flani na hapo neno kuhusu huyo mtu au hicho kitu ndo hutokea?

Hilo la mzungu kuwa mzungukaji nimelijua tokea nikiwa dogo kabisa.

Katika maongezi yangu na wataalamu wa lugha [ Prof. Herman Batibo....Google him....Msukuma huyo] kutoka idara ya lugha za kigeni na isimu ya chuo kikuu cha Dar, nadharia waliyokuwa wanaikubali zaidi ni hiyo ya 'mzungukaji' kwa sababu ilikuwa inaakisi uhalisia wa hao wageni waliokuja.

Soma kidogo kuhusu Batibo hapo Herman Batibo, University of Botswana

Hili la mzungu kuwa mungu hali make sense kwa sababu ilikuwa na bado inadhaniwa kuwa mungu haishi duniani. Anaishi mbinguni.

Hivyo mzungu hawezi kuwa mungu. Mzungu ni mzungu kutokana hali yake ya kuzunguka huku na kule tofauti na ilivyokuwa kwa wenyeji wa maeneo hayo ambayo wazungu walifika.

Wasomi wa Kiafrika wana vested interest ya ku undermine habari ya mzungu kutokakatika mizungu.

Racial pride.

Umeiona hiyo link?

Unasema ilikuwa inaaminika Mungu haishi duniani katika jamii iliyoamini kwamba mpaka miti na wanyama ni miungu?

Halafu mbona Wakristo waliamini Mungu anaishi mbinguni, lakini Yesu alivyokuja duniani wakaamini ni Mungu?
 
Back
Top Bottom