ubongokid
JF-Expert Member
- Apr 30, 2017
- 2,154
- 4,184
Habari za sikukuu?
Natambua kwamba kwa watanzania wengi hii ni siku kama siku nyingine na kwamba maisha yanaendelea kama kawaida. Natambua pia kwamba kuna ambao wako katika huzuni na pia wapo ambao wako katika furaha. Hayo ndio maisha na inabidi tukubaliane na hali halisi kabla ya kuanza kukabiliana nayo.
Leo nataka nizungumzie kwa uchache kuhusu jambo nyeti sana liitwalo UGAIDI-ambo kwa mujibu wa maelezo anuai ni Vitisho na mashambulizi yanayolenga kutia hofu, wasiwasi pamoja na kuleta taharuki. UGAIDI ni uhalifu unaofanywa na mtu au watu ukiwa na lengo la kuleta hofu kwa watu fulani au jamii nzima. Lengo la ugaidi ni kuleta hofu na taharuki.
Kwa wengi wetu unauchukulia ugaidi kama matendo ambayo yanafanywa na watu wanaopinga mamlaka fulani na wenye maslahi yao binafsi. Na hii ni kutokana na ukweli kwamba vyombo vingi vya habari vimekuwa vikitoa kipaumbele zaidi katika upande mmoja tu wa maelezo bila kuonesha au kutafiti iwapo kuna upande wa pili ambao nao unaweza kuwa na madai ya msingi ambayo yanapaswa kupewa kipaumbele. Hili linaweza kuwa linafanyika kutokana hofu kwa kujua au kutokujua na wakati mwingine vyomba vya habari vinaweza kuwa sehemu ya mpango mzima wa kuleta hofu.
Kwa kawaida UGAIDI wowote ule ni matokeo ya watu kuto kuridhika na hali ya mambo au kutokana na kuwa na ajenda au mipango binafsi ambayo inawez akufanikiwa kwa kuleta taharuki. Pamoja na hayo huwa kuna aina ya ugaidi ambao huwa unafanywa na taasisi za kiserikali au vikundi vinavyoafadhiliwa nwa serikali au watumishi fulani wa serikali wenye maslahi katika jambo fulani. Huu ni ugaidi unaoitwa STATE SANCTIONED TERRROR ambao huwa ni maarufu sana katika nchi za kibabe ni kidiktea ingawa piwa unaweza kuwepo katika nchi za kidemokrasia.
Katika aina hii ya ugaidi,serikali inaweza kutumia idara za serikali kutishia watu kwa kuwashambulia,kuwaua,kuwateka na hata kutaka mifumo ya kikatiba na kisheria katika namna ambayo itawakandamiza wale ambao wanatofautiana kiitikadi,kimsimamo na kimtizamo dhidi ya serikali. Aina hii ya ugaidi mara nyingi utakuta kuna mgawanyiko wa mtazamo katika jamii kuokana na ukweli kwamba unafanywa na mamlaka halali za nchi na wakati mwingine ni kwa ni ambayo inaonekana ni njema machoni kwa wengi.
UGAIDI huu huweza kuwa wa kutumia mfumo wa kisheria kwa ama kutunga sheria kandamizi na onevu na kisha kuwalenga aina fulani ya watu kwa lengo la kuwafanya washindwe kukosoa na kutoa maoni dhidi ya serikali.Wakati mwingine sheria kandamizi zinaweza kutungwa kwa lengo la kuwatia hofu watu hao na kuweza kuwafuatilia. Mfano wa sheria hizo unaweza kuwa sheria zinazopinga faragha(Anti Privacy Laws) Sheria zinazoruhusu detention without trial,Sheria zinazoruhusu bail denial, sheria zinazo criminize maswala halali na ya kawaida kama vile, haki ya kushirikiana,haki ya kufanya shughuliza za kuingiza kipato, haki ya kupata taarifa n.k..Sheria zote zinawekwa si kwa lengo la kuweka mazingira mazuri ya kibiashara na kijamii bilahuwa zinawalenga watu fulani au makundi fulani katika jamii.
AINA hii ya UGAIDI ndio hupelekea kuzaliwa kwa vikundi vya kigaidi vya nje ya MFUMO ambavyo huwa vinazaliwa kama matokea ya kukosa njia halali za kudai na kupata haki zao na hivyo kujikuta wakilazimika kutumia njia zisizokuwa halali.Kwa lugha nyingine ni kwamba Pale serikali inapozima njia zote halali za kuweza kupata haki basi jamii hulazimika kutafuta njia mbadala ya kupata haki na hapa ndipo vikundi vya KIGAIDI huzaliwa.
Hivyo basi ugaidi ni matokea ya kushindwa serikali katika utawala.Ni ishara ya kwamba serikali imeshindwa kuelewa kila Jamii inataka na hivyo kuamua kutumia nguvu katika kuhakikisha inathibitisha uhalali wake.Pale jamii inapoamua kujizatiti ndipo basi huzaliwa vikundi vinavyoitwa vya kigaidi ambavyo mara nyingi huundwa na watu ambao ni VICTIMS wa UGAIDI wa SERIKALI.
Ninchotaka kusisitiza hapa ni kwamba UGAIDI mwingi huanza na kutokuridhika kwa watu na mfumo wa haki wa nchi na ni matokea ya STATE SANCTIONED TERROR.Vikundi hivi hujikuta vikilazimika kutumia UGAIDI kama namna pekee ya kuhakikisha madhila yao yanasikika.
Itoshe tu kusema kwamba, tusikae kimya tunapoona Jamii yetu na serikali yetu inavunja haki kwa uwazi kabisa kwani matokeo yake yanaweza kuwa mabaya hasa kutokana ukweli kwamba kila mwanadamu anataka kutendewa HAKI.
Niwatakie Maisha Mema.
Natambua kwamba kwa watanzania wengi hii ni siku kama siku nyingine na kwamba maisha yanaendelea kama kawaida. Natambua pia kwamba kuna ambao wako katika huzuni na pia wapo ambao wako katika furaha. Hayo ndio maisha na inabidi tukubaliane na hali halisi kabla ya kuanza kukabiliana nayo.
Leo nataka nizungumzie kwa uchache kuhusu jambo nyeti sana liitwalo UGAIDI-ambo kwa mujibu wa maelezo anuai ni Vitisho na mashambulizi yanayolenga kutia hofu, wasiwasi pamoja na kuleta taharuki. UGAIDI ni uhalifu unaofanywa na mtu au watu ukiwa na lengo la kuleta hofu kwa watu fulani au jamii nzima. Lengo la ugaidi ni kuleta hofu na taharuki.
Kwa wengi wetu unauchukulia ugaidi kama matendo ambayo yanafanywa na watu wanaopinga mamlaka fulani na wenye maslahi yao binafsi. Na hii ni kutokana na ukweli kwamba vyombo vingi vya habari vimekuwa vikitoa kipaumbele zaidi katika upande mmoja tu wa maelezo bila kuonesha au kutafiti iwapo kuna upande wa pili ambao nao unaweza kuwa na madai ya msingi ambayo yanapaswa kupewa kipaumbele. Hili linaweza kuwa linafanyika kutokana hofu kwa kujua au kutokujua na wakati mwingine vyomba vya habari vinaweza kuwa sehemu ya mpango mzima wa kuleta hofu.
Kwa kawaida UGAIDI wowote ule ni matokeo ya watu kuto kuridhika na hali ya mambo au kutokana na kuwa na ajenda au mipango binafsi ambayo inawez akufanikiwa kwa kuleta taharuki. Pamoja na hayo huwa kuna aina ya ugaidi ambao huwa unafanywa na taasisi za kiserikali au vikundi vinavyoafadhiliwa nwa serikali au watumishi fulani wa serikali wenye maslahi katika jambo fulani. Huu ni ugaidi unaoitwa STATE SANCTIONED TERRROR ambao huwa ni maarufu sana katika nchi za kibabe ni kidiktea ingawa piwa unaweza kuwepo katika nchi za kidemokrasia.
Katika aina hii ya ugaidi,serikali inaweza kutumia idara za serikali kutishia watu kwa kuwashambulia,kuwaua,kuwateka na hata kutaka mifumo ya kikatiba na kisheria katika namna ambayo itawakandamiza wale ambao wanatofautiana kiitikadi,kimsimamo na kimtizamo dhidi ya serikali. Aina hii ya ugaidi mara nyingi utakuta kuna mgawanyiko wa mtazamo katika jamii kuokana na ukweli kwamba unafanywa na mamlaka halali za nchi na wakati mwingine ni kwa ni ambayo inaonekana ni njema machoni kwa wengi.
UGAIDI huu huweza kuwa wa kutumia mfumo wa kisheria kwa ama kutunga sheria kandamizi na onevu na kisha kuwalenga aina fulani ya watu kwa lengo la kuwafanya washindwe kukosoa na kutoa maoni dhidi ya serikali.Wakati mwingine sheria kandamizi zinaweza kutungwa kwa lengo la kuwatia hofu watu hao na kuweza kuwafuatilia. Mfano wa sheria hizo unaweza kuwa sheria zinazopinga faragha(Anti Privacy Laws) Sheria zinazoruhusu detention without trial,Sheria zinazoruhusu bail denial, sheria zinazo criminize maswala halali na ya kawaida kama vile, haki ya kushirikiana,haki ya kufanya shughuliza za kuingiza kipato, haki ya kupata taarifa n.k..Sheria zote zinawekwa si kwa lengo la kuweka mazingira mazuri ya kibiashara na kijamii bilahuwa zinawalenga watu fulani au makundi fulani katika jamii.
AINA hii ya UGAIDI ndio hupelekea kuzaliwa kwa vikundi vya kigaidi vya nje ya MFUMO ambavyo huwa vinazaliwa kama matokea ya kukosa njia halali za kudai na kupata haki zao na hivyo kujikuta wakilazimika kutumia njia zisizokuwa halali.Kwa lugha nyingine ni kwamba Pale serikali inapozima njia zote halali za kuweza kupata haki basi jamii hulazimika kutafuta njia mbadala ya kupata haki na hapa ndipo vikundi vya KIGAIDI huzaliwa.
Hivyo basi ugaidi ni matokea ya kushindwa serikali katika utawala.Ni ishara ya kwamba serikali imeshindwa kuelewa kila Jamii inataka na hivyo kuamua kutumia nguvu katika kuhakikisha inathibitisha uhalali wake.Pale jamii inapoamua kujizatiti ndipo basi huzaliwa vikundi vinavyoitwa vya kigaidi ambavyo mara nyingi huundwa na watu ambao ni VICTIMS wa UGAIDI wa SERIKALI.
Ninchotaka kusisitiza hapa ni kwamba UGAIDI mwingi huanza na kutokuridhika kwa watu na mfumo wa haki wa nchi na ni matokea ya STATE SANCTIONED TERROR.Vikundi hivi hujikuta vikilazimika kutumia UGAIDI kama namna pekee ya kuhakikisha madhila yao yanasikika.
Itoshe tu kusema kwamba, tusikae kimya tunapoona Jamii yetu na serikali yetu inavunja haki kwa uwazi kabisa kwani matokeo yake yanaweza kuwa mabaya hasa kutokana ukweli kwamba kila mwanadamu anataka kutendewa HAKI.
Niwatakie Maisha Mema.