Je, unafanyaje ukiwa umepigiwa full light barabarani?

Je, unafanyaje ukiwa umepigiwa full light barabarani?

Kweli aisee, Jamaa wa Abood ya Moro - Dar alisababisha nichane tairi pale Bwawani Morogoro, lami ilikuwa imetepeta na kutengeneza kamtaro hivi, sasa yeye ameovateki bila tahadhari anakuja kukutana na mimi kwenye lane yangu analazimisha nimpishe, kutii amri nikaamua kutanua kumbe ndio naichana tairi kwenye lami iliyojitengeneza kama kisu, hapo ni usiku nahangaika kubadili tairi wao wanaendelea na safari yao, nilisikitika sana. Hasara ya kununua tairi mpya sababu ya ubabe wa wenye basi.
Pole Sana mkubwa,Mi najipanga nichukue Mandolin kisha niitengeneze ngao nzito ya chuma ili niwe nakula Taa zao.
 
Rahisi sana, wewe unachokifanya unaangalia ule mstari mweupe unaowatenganisha na uhakikishe unakuongoza.....kitu kingine ukipigwa Full light hakikisha haungalii mwanga wa taa wa hizo gari.
 
Kimbembe ukutane na tractor au pawatila haina reflector halafu mwanga wako hafifu
 
Back
Top Bottom