Je, unakumbuka nini enzi zako za JKT? Ni mambo gani yalikufurahisha au kukukwaza?


Duuuh kweli jeshi si mchezo
 
Mafinga JKT operation 'Program ya Chama' 1988/89 Namkumbuka Afande Mlay kafupi ila sauti kaliii! Namkumbuka Afande 'Nusu Mungu' pale kombania D alikuwa ni nomaaa akimwangalia mtoto wa kike kwa macho ya ukali basi analia hadi anajikojolea! Nakumbuka UCHAKA ilikuwa balaa hadi watu walizimia!
 
Haaa mi niliingilia mafinga! yaani kila nikiangalia magoti yangu yana michubuko! kubwa zaidi nakumbuka siku niliyotoka na afande Kiangazi kwenda kunywa ulanzi tukamix na viroba vya Malawi double panch aaah! nlizima mbayaa nikashindwa kuamka mwisho wa siku nikajisalimisha kwa mkufunzi ili paranja liniepuke sitaslsahauuuu! kubwa zaid ni mwendo wa kadet zile KILOMETER 180 MONDULI aaaah!
 
kwanza nakupongeza kwa ufafanuzi wako mzuri ila kwa upande wangu mimi nina diploma ya sheria, je nitapata kipaumbele hasa kwenye ajira?
 
Mkuu mm nina diploma ya uharibu nikabahatika kuingia jeshn je,naanza na cheo gan? Na n baada ya mafunzo au utakuwa unatambulka direct?

Nakushauri ww usiende jeshini kwa jinsi nilivyokusoma maswali unayouliza.
Uanajeshi haumo damuni mwako bali ni ajira ipo kwa damu yako morani.

Ukipiga mafunzo ya jkt afu uambiwe ulitumikie jeshi kwa miaka miwili free bila ya malipo najua utarusha ngumi navyokuona.

Na hapa kaeleza usiende kisa hauna ajira au kitaa kimekuwa kigumu.
 
I humbly thanks,for your lesson,i had no idea about jkt,but right now i'm aware of it ,but my question is,if am an advocate, and it happens i get a chance to join jkt,what privileges will i be entitled with!?
 
I humbly thanks,for your lesson,i had no idea about jkt,but right now i'm aware of it ,but my question is,if am an advocate, and it happens i get a chance to join jkt,what privileges will i be entitled with!?


Advocate? No privileges..utakuwa sawa sawa na recruits wengine,utazeeshwa kama kawaida

Labda ungekuwa medical doctor(ungekuwa unashinda hospitali kule unatibu kuruti wenzio) au basi hata fundi makenika
Mkuu,kimsingi kule hakuna kuruta mwenye haki kuliko mwenzie,muhimu kuliko mwenzie,nyie wote ni sawa.Sema hapo kwenye unyeti wa taaluma ndio panaweza kukupa nafasi ya kutegea kazi za watu,lakini sio kila mara

Lakini pia,katika taaluma wanazokimbilia jeshini,sheria na ualimu wamo aisee..Hautojikuta peke yako
 
Ok,ahsante sana,vip position ya mtu aliesoma sheria kwa ngazi ya degree,akimaliza jkt,possibility ya kwenda jwtz inakuwepo au la?
 
Sikushauri kwenda jkt kama unaelimu yako mkuu komaa kitaa ipo siku utadaka mishe
 

Umemjibu kwa busara sana, kazi ya jeshi ukitanguliza pesa na cheo mbele na mapenzi ya hiyo kazi ukayaweka nyuma, kwa kweli utajiona unaumia tu ukishaanza kazi.
 
Ok,ahsante sana,vip position ya mtu aliesoma sheria kwa ngazi ya degree,akimaliza jkt,possibility ya kwenda jwtz inakuwepo au la?


Possibility ipo,lakini itategemea na uhitaji wa jeshi kwa wakati huo.Nijuavyo mimi,kwa sasa jeshi linahitaji sana wataalamu wa afya,kilimo,uhandisi na wasanifu majengo na marubani na wapiganaji(wale darasa la saba na form four)

Kimsingi ,usiende jeshini kusaka ajira..Utateseka,utaumia na utajutia..Kamaa unalipenda jeshi kutoka moyoni,nenda,lakini kama unaenda kwa sababu kitaa hapasomi,utatoroka depo
 

Daaah hii thread bado inapeta?

Loong time saaana!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…