Ndo maana JF tunaiita jungu kuu, mmenikumbusha mengi na mbali sana. Kwa wale wa Oljoro mnaikumbuka ROSHEROOO umasaini?
Afande Dauda keshatajwa, je, Mnamkumbuka Afande John Matondo?, yeye akiamsha watu kwa kurusha changarawe au kijiwe kidogo juu ya bati!, sasa ole wako usiamke! Wakati mwingine anaingia hangani halafu anatoa kikohozi cha kebehi halafu anatoka anasuburi, dakika mbili baadaye anakata bogi la wachelewaji! Afande Bosco yeye sifa yake kubwa ilikuwa alishaua kuruta kwa kusulubu!-Akikutazama tu unaweza kuanguka!
Nawakumbuka na ningependa kuwasiliana na wengi kama akina Justin Majengo, Mbutolwe Kabeta (alinifundisha kusonga ugali wa kombania, kwani mara ya kwanza mwiko wa ugali nusura unirushilie mbali!), Erasto Mkumbo, Peter Mhina, Hadi Katunzi, Chausiku (Butote?), (Lindarose?) Mushi, Wallace Arthur-Hamisi Bakari (Dr), Kapinga, Davi Mwamakula, Abdul Tajiri, Costantine Mkama, Costa, Joseph Mbelwa, Sauka (Stanley?) Ndaro, Eva Nziku, (Mary?) Shule, (Grace?) Magoti, Joseph Masanja, Yohana Mgonja, na wengineo wengi tu ambao majina hayajanijia kichwani sasa hivi.
Nilijifunza mengi na nilifunguka macho kwa mengi niliyoona, nilipata marafiki na wengi wao tukawa kama ndugu.