Je, unamfahamu Aziz Ally, aliyechochea kuwepo kwa eneo la Mtoni kwa Aziz Ally?

Mnataka kila mtu atambuliwe katika harakati za kudai uhuru si inabidi pia muweke mchango wa wakoloni kutuwekea barabara maana nyerere kukosa hizo barabara walizojenga wakoloni asingeweza kufika dar.

Ni kama kipindi hiki kila kitu tunasema chini ya uongozi wa magufuli,ndege ,barabara ni chini ya chuma anko magu kwani ina maana ni yeye peke yake ndio anafanya kila kitu? Kwani baraza la mawaziri hawafanyi chochote?
 
Jibu nililopokea kutoka kwa mpashaji wangu kutoka kwa Mwenyekiti wa Medali lilinishangaza sana

Mohamed Said kama haoutojali tuambie ulipewa jibu gani?
 
In shaAllah ipo siku tutatembea wote mjinii.
 
Historia ya Tanganyika ni tamu sana
 
Tatizo la matajiri wengi wa kiafrika, utajiri wao unahusishwa na majini.....mwenye mali akifa tu na kila kitu kinakwenda naye.
Sio majini bali hao wanaomiliki utajiri hawawafundishi watoto wao jinsi wao wanavyofanya.
Ndo maana mwenye utajiri akiondoka utajiri unaisha.
 
Sio majini bali hao wanaomiliki utajiri hawawafundishi watoto wao jinsi wao wanavyofanya.
Ndo maana mwenye utajiri akiondoka utajiri unaisha.
Wanakuwa wanaogopa kuwafundisha watoto wao kuuana wenyewe kwa wenyewe au kushikwa uchawi na watoto wao
 
Dooohh bahati mbaya original history ya Tanganyika na Tanzania yetu haipo kabisa kwnye maktaba zetu.....sijui kwa nn
 
Swali zuri sana hili mkuu
 
Rafiki zake wanasema walikuwa wakimuona Dossa ameingia kila mtu anapumua kwani watakula na kunywa kwa furaha. Dossa alikuwa mtu karimu sana. Rafiki zake wa karibu sana walimpa jina la utani, ‘’The Bank.’’
Ukarimu kama huu mimi siutaki kabisa katika maisha yangu. Yaaani wao wanafurahi kula na kunywa kwa pesa zangu alafu pesa zao wanapeleka katika shughuli za ujenzi na maendeleo
 
Mwalimu Nyerere alipokuwa anastaafu alitoa medali 3979 kwa Watanzania walioitumikia nchi hii. Jina la Dossa halikuwapo katika orodha ile…''
Ninatamani sana kama tungepata pia fursa ya kusikiliza upande wa pili wa story kutoka kwa mwalimu JK Nyerere binafsi (a well-balanced story), basi tungeweza kufahamu kwanini mzee Dossa hakuwa katika orodha ile ya wapewa medani.

Si sahihi kufanya hitimisho la maamuzi kwa kuegemea maelezo ya mtu mmoja pekee.
 
Ukwasi umekwenda na Marehemu hao.Nadhani limebakia jina tu pale kwa Azizi Ally.
Mana kwa Utajiri huo uliotajwa hapo kwa miaka hiyo Labda kwasasa familia hii ingekuwa moja ya Matajiri wakubwa Tanzania na Africa Mashariki.
Naam
 
Umeandika vizuri sana na katika mtiririko mzuri ila umemalizia na kachuki kidogo.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…