Je, unamfahamu Glenn Cunnigham? Kutoka kuwa mlemavu mpaka Mwanariadha maarufu

Je, unamfahamu Glenn Cunnigham? Kutoka kuwa mlemavu mpaka Mwanariadha maarufu

uvugizi

JF-Expert Member
Joined
Oct 13, 2012
Posts
1,278
Reaction score
956
Glenn cunnigham alipokuwa mwanafunzi , aliteuliwa kuwa mtu ambaye atakuwa anawasha moto katika kipindi cha baridi ili watoto wenzake waweze kupata joto. Siku moja katika harakati zake za kuwasha moto , kumbe dumu la mafuta ya taa mwenzake akaweka petroli . glenn cunnigham alipoenda kuwasha moto aliungua mwili mzima na hata ndugu yake aliyekuwa naye , huyo ndugu yeye aliungua mpaka kufa .

Glenn cunnigham alikimbizwa hospitali , akiwa ameharibika sana na kuonekana kwamba hataweza kutembea maisha yake yote , na kushauriwa mguu mmoja ukatwe , wazazi wa glenn walikubali lakini yeye mwenyewe alikataa kwani aliwaambia nina ndoto ya kuwa mwanariadha mkubwa licha ya hali hii . Madaktari walimshauri awe anatembelea wheel chair na kujitahidi kutia nguvu miguu kwa kuanza kutembea kwa support kama itawezekana .

Kwa takribani miaka kadhaa glenn alianza kupata nguvu na hatimaye siku moja glenn aliweza kusimama na kupiga hatua bila support. Baada ya kuweza kusimama akajiwekea bullet journal , kila siku anakimbia kidogo kidogo na hakuacha .

Baada ya kuwa fit na muendelezo wa mazoezi ya muda mrefu, mwaka 1934 madison square garden , ndiye mwanariadha pekee aliyeweza kumaliza mbio ndefu zaidi na kuweka record , na baada ya hapo alishiriki Olympic mara nyingi zaidi na zote kushinda kwa kuvunja record .
Kwa sasa anajulikana kama the greatest American miler of all time .

Glenn cunnigham hadithi yake ni chachu kwetu tukiwa katika kipindi cha matatizo . kama una shauku , dhamira ya dhati hakuna kinachoweza kukushinda .

Daima kumbuka kuwa when you are down or feel like you are stuck in a hopeless situation , remember the story of glenn cunnigham , all you have to do , is commit to doing it.

Biblia inatuambia Wakolosai 3:23 ….. lolote mfanyalo lifanyeni kwa moyo kama kwa bwana wala si kwa wanadamu .

GLENN.jpg

Lakini mtumishi wa Mungu ninaye muheshimu sana TD JAKES anasema NEVER GIVE UP HOPE , IT IS ALWAYS DARKEST BEFORE THE DAWN. Yaani kwa maana nyingine unapokaribia kukata tama ndipo upenyo ulipo.

Be inspired
kihiga@zoho.com
 
Duuh madini kama haya tuliyamiss kwa muda mrefu,huko Instagram kuta kuchwa wanajadili reality show ya wasafi
 
Back
Top Bottom