Open school
JF-Expert Member
- Jul 13, 2015
- 1,158
- 1,746
Tatizo la kutokuona vitu vizuri halitokani na misuli ya macho kulegea, bali uchovu, hivyo unatakiwa u-relax .
Wakati uko kwenye msongo wa mawazo misuli inayozunguka mboni ya jicho hubanwa na kuikosesha utulivu, hii husababisha kupungua kwa uwezo wa jicho kuona/kuona vitu kama vina ukungu(blur vision) na kuwa unabadilika mahali ambapo uoni unakuwepo kwenye retina.
Matatizo ya kuona masafa ya karibu, mbali, mbali na karibu(astigmatism), mtoto wa jicho(catalact) na glaucoma yanaweza kutokomezwa kwa "Dr. Bates method).
Nyoosha kiganja chako vidole vikiwa vimefunga kisha tumia vitundu vidogo katikati ya vidole kutazama vitu utaona kwamba uwezo wako wa kuona unaweza kurejea kama awali.
"Dr. Bates method" ni mbinu ya kiakili inayokufundisha namna ya kuondoa uchovu kwenye misuli ya macho yako na kurejesha uoni wako uliopungua.
NI KWA NAMNA GANI BATES METHOD INAFANYA KAZI?
"Kwa kawaida jicho lako limezungukwa na misuli sita na inatembea kuzunguka jicho lako. Kwa kawaida mishipa hiyo huwa rahisi kufuata kile jicho lako linata kukiona. Tatizo linaweza kutokana na sababu za hisia za kimwili(hofu, msongo wa mawazo, hasira nk)".
Anasema Dr. Bates.
Kwahiyo una machaguo matatu...
1. Kufahamu tatizo linalokufanya uwe msongo wa mawazo. Unapoondokana na msongo wa mawazo na kuifanya akili itulie/relax mara uwezo wa kuona vizuri hurejea kama mwanzo.
2. Kufanya upasuaji(LASIK) ambao hubadili moja kwa moja uwezo wa macho ku-focus mbali.
3. Kuvaa miwani(contact lens). Kuvaa miwani hufanya tatizo liwe endelevu kwa sababu miwani haiondoi tatizo zaidi ya kukufanya uwe tegemezi.
Wakati watu wanaposhindwa kuona vitu vizuri hujikuta wakibinya macho ili kufanya vitu kuonekana vizuri. Kubinya macho ni tendo baya ambalo hufanya mhusika kuwa stressed na hivyo kubana misuli kuzunguka mboni ya jicho.
Moja ya mbinu iliyotumiwa na Dr. Bates kwa wagonjwa wake ni njia ya viganja(Palming). Tazama mahali kisha angalia uwezo wako wa kuona mwanzoni ulivyo. Taratibu weka viganja vyako juu ya macho yako kisha tulia(relax), regeza mabega yako. Unaweza kujiegemeza kwenye meza au juu ya mto ili kuongeza utulivu(relaxion). Tulia(relax) walau kwa muda wa dakika mbili kisha ondoa mikono yako juu ya macho kisha angalia kama kuna vitu vinaonekana vizuri tofauti na kabla huja-relax.
Chukua karatasi yenye maandishi kisha isogeze karibu kabisa na pua(kwa wenye mypoia& astigmatism)utakuwa unayaona maandishi vizuri kisha haraka sana isogeze mbali karatasi hiyo bila kupepesa macho pembeni, endelea kutazama hadi pale utakapoona mabadiliko kidogo kisha utoe karatasi. Kwa wenye presbyopia(kutokuona vitu vya karibu) chukua karatasi yenye maandishi yanayosomeka vizuri kisha iweke mbali mbele ya macho kwa muda kisha ghafla ihamishe karibu na uso. Fanya hivyo mara kwa mara hadi tatizo litakapoisha.
Dr. Bates anasema kwamba jicho haliwezi ku-focus kwenye vitu vinavyonekana bali, hutaka kuona vitu visivyoonekana hivyo unapotazama karatasi yenye maandishi au kitu chochote kwenye umbali usioweza kuona vizuri hufanya mishipa ya fahamu iliyounganika na jicho hupeleka taarifa kwenye ubongo na ubongo hurudisha jibu kwamba umeona kitu hicho hivyo baada ya muda vitu hivyo vitaanza kuzoeleka kwenye ubongo (rejea kwamba matatizo ya uwezo wa kuona hutokana na uchovu kwenye mishipa inayozunguka macho kuzuia kupeleka taarifa ya taswira kwenye ubongo), kwahiyo hata pale unapotumia miwani kurekebisha uoni wako, taarifa hupelekwa kwenye ubongo kwamba taswira imeonekana kwa msaada wa miwani na hivyo kufanya uendelee kuwa tegemezi kwa miwani huku tatizo likiendelea kuwepo.
NOTE
Njia ya Dr. Bates sio mbinu kitabibu bali ni mbinu ya kiakili, kwahiyo hakikisha unatambua tatizo lako kwa kuonana na daktari macho kupata vipimo. Zoezi hili linahitaji uvumilivu na baada ya muda matokeo yatakuwa mazuri.
Unaweza kuangalia video hizi namna ya kufanya mazoezi hatua kwa hatua hadi kupona kabisa tatizo lako.
Watakaoanza kutumia njia hii ya Dr. Bates ni vizuri wakawa wanaleta mrejesho hapa ili wengine wahamasike kutumia njia hiyo kurejesha uwezo wao wa kuona.
Wakati uko kwenye msongo wa mawazo misuli inayozunguka mboni ya jicho hubanwa na kuikosesha utulivu, hii husababisha kupungua kwa uwezo wa jicho kuona/kuona vitu kama vina ukungu(blur vision) na kuwa unabadilika mahali ambapo uoni unakuwepo kwenye retina.
Matatizo ya kuona masafa ya karibu, mbali, mbali na karibu(astigmatism), mtoto wa jicho(catalact) na glaucoma yanaweza kutokomezwa kwa "Dr. Bates method).
Nyoosha kiganja chako vidole vikiwa vimefunga kisha tumia vitundu vidogo katikati ya vidole kutazama vitu utaona kwamba uwezo wako wa kuona unaweza kurejea kama awali.
"Dr. Bates method" ni mbinu ya kiakili inayokufundisha namna ya kuondoa uchovu kwenye misuli ya macho yako na kurejesha uoni wako uliopungua.
NI KWA NAMNA GANI BATES METHOD INAFANYA KAZI?
"Kwa kawaida jicho lako limezungukwa na misuli sita na inatembea kuzunguka jicho lako. Kwa kawaida mishipa hiyo huwa rahisi kufuata kile jicho lako linata kukiona. Tatizo linaweza kutokana na sababu za hisia za kimwili(hofu, msongo wa mawazo, hasira nk)".
Anasema Dr. Bates.
Kwahiyo una machaguo matatu...
1. Kufahamu tatizo linalokufanya uwe msongo wa mawazo. Unapoondokana na msongo wa mawazo na kuifanya akili itulie/relax mara uwezo wa kuona vizuri hurejea kama mwanzo.
2. Kufanya upasuaji(LASIK) ambao hubadili moja kwa moja uwezo wa macho ku-focus mbali.
3. Kuvaa miwani(contact lens). Kuvaa miwani hufanya tatizo liwe endelevu kwa sababu miwani haiondoi tatizo zaidi ya kukufanya uwe tegemezi.
Wakati watu wanaposhindwa kuona vitu vizuri hujikuta wakibinya macho ili kufanya vitu kuonekana vizuri. Kubinya macho ni tendo baya ambalo hufanya mhusika kuwa stressed na hivyo kubana misuli kuzunguka mboni ya jicho.
Moja ya mbinu iliyotumiwa na Dr. Bates kwa wagonjwa wake ni njia ya viganja(Palming). Tazama mahali kisha angalia uwezo wako wa kuona mwanzoni ulivyo. Taratibu weka viganja vyako juu ya macho yako kisha tulia(relax), regeza mabega yako. Unaweza kujiegemeza kwenye meza au juu ya mto ili kuongeza utulivu(relaxion). Tulia(relax) walau kwa muda wa dakika mbili kisha ondoa mikono yako juu ya macho kisha angalia kama kuna vitu vinaonekana vizuri tofauti na kabla huja-relax.
Chukua karatasi yenye maandishi kisha isogeze karibu kabisa na pua(kwa wenye mypoia& astigmatism)utakuwa unayaona maandishi vizuri kisha haraka sana isogeze mbali karatasi hiyo bila kupepesa macho pembeni, endelea kutazama hadi pale utakapoona mabadiliko kidogo kisha utoe karatasi. Kwa wenye presbyopia(kutokuona vitu vya karibu) chukua karatasi yenye maandishi yanayosomeka vizuri kisha iweke mbali mbele ya macho kwa muda kisha ghafla ihamishe karibu na uso. Fanya hivyo mara kwa mara hadi tatizo litakapoisha.
Dr. Bates anasema kwamba jicho haliwezi ku-focus kwenye vitu vinavyonekana bali, hutaka kuona vitu visivyoonekana hivyo unapotazama karatasi yenye maandishi au kitu chochote kwenye umbali usioweza kuona vizuri hufanya mishipa ya fahamu iliyounganika na jicho hupeleka taarifa kwenye ubongo na ubongo hurudisha jibu kwamba umeona kitu hicho hivyo baada ya muda vitu hivyo vitaanza kuzoeleka kwenye ubongo (rejea kwamba matatizo ya uwezo wa kuona hutokana na uchovu kwenye mishipa inayozunguka macho kuzuia kupeleka taarifa ya taswira kwenye ubongo), kwahiyo hata pale unapotumia miwani kurekebisha uoni wako, taarifa hupelekwa kwenye ubongo kwamba taswira imeonekana kwa msaada wa miwani na hivyo kufanya uendelee kuwa tegemezi kwa miwani huku tatizo likiendelea kuwepo.
NOTE
Njia ya Dr. Bates sio mbinu kitabibu bali ni mbinu ya kiakili, kwahiyo hakikisha unatambua tatizo lako kwa kuonana na daktari macho kupata vipimo. Zoezi hili linahitaji uvumilivu na baada ya muda matokeo yatakuwa mazuri.
Unaweza kuangalia video hizi namna ya kufanya mazoezi hatua kwa hatua hadi kupona kabisa tatizo lako.
Watakaoanza kutumia njia hii ya Dr. Bates ni vizuri wakawa wanaleta mrejesho hapa ili wengine wahamasike kutumia njia hiyo kurejesha uwezo wao wa kuona.