Je, unataka kulima mazao ya mbogamboga na matunda lakini unakosa maarifa sahihi? Karibu tushauriane hapa

Roving Journalist

JF Roving Journalist
Joined
Apr 18, 2017
Posts
3,984
Reaction score
13,760
Habari wanaJF wakulima,

Hii ni mada mahususi itakayotoa elimu na maarifa kuhusu kilimo cha mazao ya mbogamboga na matunda kwa ujumla.

Watu wengi wanatamani sana kulima ila wanakosa maarifa mbalimbali hivyo kupelekea kushindwa na kukata tamaa.

Kupitia mada hii nawakaribisha tushauriane.

Pia soma => Kilimo cha MbogaMboga - Kanuni za Kukuza Mboga

 
Ahsante,mie naomba unishauri juu ya kilimo cha giligilani,
juu ya magonjwa na namna ya kupata mbegu zake.
 
Naomba maelekezo ya nyumba kitalu. nilikuwa na mpango wa kujenga banda la makuti mfano wa namna bar zinavyojengwa ilihali nizuie jua na mvua. je wazolangu unalionaje?
 
Nashukuru. Naomba maelekezo ya nyumba kitalu. nilikuwa na mpango wa kujenga banda la makuti mfano wa namna bar zinavyojengwa ilihali nizuie jua na mvua. je wazolangu unalionaje
 

Shukrani sana
kama nahitaji majani tu nadhani sina haja ya kupiga dawa ya maua,
ngoja nilime nitaleta mrejesho.
 
Mkuu naomba kufahamishwa kuhusu kilimo cha mbaazi. Gharama zake hadi mavuno, maeneo inapostawi, msimu wa kilimo, muda inaochukua toka kupanda hadi kuvuna na makadirio ya mavuno kwa eka kwa gunia.
 
Mkuu naomba elimu kuhusu kilimo cha parachichi, apple, maeneo yanayokubali kulimwa..n.k
 
Natamani kujua kiimo cha tikiti na butternut
Jr naweza Luanda vyote kwa pamoja
 
Mkuu Ahsante Kwa Elimu Yako,mimi Naomba Kujua Au Kupewa Elimu Ya Zao La Nyanya Hybrid Kwenye Open Space.
 
ASANTE Sana Mkuu,Ntadesa kama ulivyoelekeza
Je Mbegu ipi/matikiti yapi yana uzika kwa bei ya juu, eg Dar shilingi ngapi kwa tikikiti
 
kilimomaarifa.tajiri kaka tunashukuru sana kwa elimu unayoitoa. Nina swali katika kilimo cha tikiti. Maelezo uliyoyatoa hapo juu ni kuhusu tikiti maji ila je unaweza kutumia hatua hizohizo katika matikiti ya aina nyingine kama honeydew na cantaloupe??
 
Last edited by a moderator:
Mkuu Ahsante Mimi Nalima Kipato F1 Tayari Nimeotesha Mbegu Bado Kupandikiza Shambani Nitapanda Wiki Ijayo,sasa Mbolea Ninazotaka Kutumia Ambazo Nimeandaa Ni Dap SA na CAN sasa nimepanga kuweka mbolea ya DAP siku tatu kabla ya kuweka mche nimwage maji kila siku na siku ya nne niweke miche je itakuwa sawa? na je baada ya hapo nipulize dawa gani? na je hiyo abamectine peke yake inatosha kukinga funza? naomba ushauri wako.
 
Mkuu Ahsante,mimi Niko Mtwara Na Maji Yana Chumvi Kidogo,lakini Labda Ungenipa Ushauri Wa Dawa Nzuri Maana Hapa Nina Dudu All,konto Na Ninja,pia Naomba Kujua Endapo Nitaweka Mbolea Ya Dap Wakati Wa Kupanda Nikae Siku Ngapi Niweke Mbolea Ya Kukuzia?(SA)
 
Ok,sijaelewa Unaponiambia Nisitumie CAN kama nitaweka SA kwasababu mimi niliplan nianze na DAP,then SA na mwisho nimalizie CAN matunda yakianza labda nipate ushauri wako,kwa upande wa wadudu huku kuna panzi wanakata sana nyanya kuanzia kitalu mpaka ukishapanda
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…