Elections 2010 Je, unawajua wanaoleta uchochezi kwenye uchaguzi mkuu?

Elections 2010 Je, unawajua wanaoleta uchochezi kwenye uchaguzi mkuu?

Mwanamayu

JF-Expert Member
Joined
May 7, 2010
Posts
11,662
Reaction score
6,888
Wanaoleta uchochezi kwenye uchaguzi mkuu wa kila mwaka kuanzia 1995 wengine walikwisha kufa na wengine bado wapo kwa kuweka kifungu na wengine kushindwa kukibadilisha katika katiba ya jamhuri ya muungano wa Tanzania ya 1977.

Ibara ya 41 (7) ya marekebisho ya mwaka 1995 na 2005 chini ya Mwanasheria Mkuu A. J. Chenge inasema "iwapo mgombea ametangazwa na Tume ya uchaguzi kwamba amechaguliwa kuwa Rais kwa mujibu wa ibara hii, basi hakuna mahakama yoyote itakayokuwa na mamlaka ya kuchunguza kuchaguliwa kwake".

Hivi kila mtu na mambo yote si yako chini ya sheria? Sasa hili mbona linakuwa juu ya sheria? Hivi wewe Obama unakijua kifungu hiki cha katiba yetu mpaka ututolee mfano wa utawala bora, utawala wa sheria?

Orodha ni hii hapa:
1. hayati Mwalimu Nyerere
2. Ali hassan Mwinyi
3. Ben Mkapa
4. Jakaya Mrisho Kikwete
5. wabunge wote waliopitisha kifungu hiki na kukihusudisha
6. .......
7. ......
 
Ndiyo maana chenge hutasikia anapelekwa mahakamani kwa kushiriki ufisadi wowote, kwani yeye ndiyo kafanikisha kupita kwa sheria kandamizi kwa hiyo serikali inamlipa fadhira kwa kufanikisha kutunga sheria kandamizi
 
This is very bad. we need a new president not only who cares the economy of the poor but who can lead people into total revolution including writing of the new constitution. we need Tanzania Constitution by 2011. :decision:
If we manage to do that, hata rais ataweza kushtakiwa pale ambapo atafanya utumbo. Hii ni muhimu kwa sababu ahata Rais atatekeleza kazi zake kwa uangalifu na kufuata sheria siyo kama Mkapa ambaye alikuwa anaamrisha piga risasi wazanzibari wakati walipoandamana.
:moony:
 
Mafisadi siyo hao mnaowataja pekee. Naamnini mafisadi wanajumuisha na hawa wafuatao:

1. Mahakimu na makarani wote wa mahakama ambao wamegeuza mahakama kuwa minada ya haki za watu.

2. Wafanyakazi wote wa maofisini ambao wanaishi kwa 10% na kuchakachua zabuni.

3. Madaktari wote na manesi ambao wamekuwa ni vibaka wa madawa yetu yanayosambazwa na MSD.

4. Waalimu wote ambao wametugeuza wazazi na walezi wa wanafunzi wao kuwa dili kupitia tuitions, remedials, karatasi za mitahani ya mwisho wa wiki, etc.

5. Polisi wote ambao tunaingia bure na kutoka kwa hela.

6. Wenye visima vya maji wote huko mtaani ambao huwahonga DAWASCO wasifungulie maji, ili wafanye biashara.

7. Viongozi wote wa CHADEMA ambao wanataka kutuingiza KINGI tuchague chama kinachonuka ukabila na udini. Na kabla hamjaanza LIGI nataka kusema kuwa chama ambacho BABA, MTOTO, NA MKWE wote ni wabunge, yaani NDESAPESA, LUCY OWINYO NA KIHWELU, ni chama KIBOVU na uwezo wa kufikiri wa wanachama wake unatia shaka sana!

8. KWA NCHI HII NDUGU ZANGU ORODHA HAINA MWISHO!
 
Mafisadi siyo hao mnaowataja pekee. Naamnini mafisadi wanajumuisha na hawa wafuatao:

1. Mahakimu na makarani wote wa mahakama ambao wamegeuza mahakama kuwa minada ya haki za watu.

2. Wafanyakazi wote wa maofisini ambao wanaishi kwa 10% na kuchakachua zabuni.

3. Madaktari wote na manesi ambao wamekuwa ni vibaka wa madawa yetu yanayosambazwa na MSD.

4. Waalimu wote ambao wametugeuza wazazi na walezi wa wanafunzi wao kuwa dili kupitia tuitions, remedials, karatasi za mitahani ya mwisho wa wiki, etc.

5. Polisi wote ambao tunaingia bure na kutoka kwa hela.

6. Wenye visima vya maji wote huko mtaani ambao huwahonga DAWASCO wasifungulie maji, ili wafanye biashara.

7. Viongozi wote wa CHADEMA ambao wanataka kutuingiza KINGI tuchague chama kinachonuka ukabila na udini. Na kabla hamjaanza LIGI nataka kusema kuwa chama ambacho BABA, MTOTO, NA MKWE wote ni wabunge, yaani NDESAPESA, LUCY OWINYO NA KIHWELU, ni chama KIBOVU na uwezo wa kufikiri wa wanachama wake unatia shaka sana!

8. KWA NCHI HII NDUGU ZANGU ORODHA HAINA MWISHO!

"Viongozi wote wa CHADEMA ambao wanataka kutuingiza KINGI tuchague chama kinachonuka ukabila na udini. Na kabla hamjaanza LIGI nataka kusema kuwa chama ambacho BABA, MTOTO, NA MKWE wote ni wabunge, yaani NDESAPESA, LUCY OWINYO NA KIHWELU, ni chama KIBOVU na uwezo wa kufikiri wa wanachama wake unatia shaka sana!"


Lakini usisahau kuwa Mwinyi rais mstaafu mwanae waziri, Makamba mwanae msaidizi wa Raisi na amepita ubunge bila kupingwa, Kikwete and Family.
CHUNGUZA NJOMBA UTABAINI.Kasome kwanza mada ndipo anguka jamvini
 
Mafisadi siyo hao mnaowataja pekee. Naamnini mafisadi wanajumuisha na hawa wafuatao:

1. Mahakimu na makarani wote wa mahakama ambao wamegeuza mahakama kuwa minada ya haki za watu.

2. Wafanyakazi wote wa maofisini ambao wanaishi kwa 10% na kuchakachua zabuni.

3. Madaktari wote na manesi ambao wamekuwa ni vibaka wa madawa yetu yanayosambazwa na MSD.

4. Waalimu wote ambao wametugeuza wazazi na walezi wa wanafunzi wao kuwa dili kupitia tuitions, remedials, karatasi za mitahani ya mwisho wa wiki, etc.

5. Polisi wote ambao tunaingia bure na kutoka kwa hela.

6. Wenye visima vya maji wote huko mtaani ambao huwahonga DAWASCO wasifungulie maji, ili wafanye biashara.

7. Viongozi wote wa CHADEMA ambao wanataka kutuingiza KINGI tuchague chama kinachonuka ukabila na udini. Na kabla hamjaanza LIGI nataka kusema kuwa chama ambacho BABA, MTOTO, NA MKWE wote ni wabunge, yaani NDESAPESA, LUCY OWINYO NA KIHWELU, ni chama KIBOVU na uwezo wa kufikiri wa wanachama wake unatia shaka sana!

8. KWA NCHI HII NDUGU ZANGU ORODHA HAINA MWISHO!

Kweli Nyani haoni kundule:
JK, Salma, Rizonw, Miraji.........the list goes on!
 
This is very bad. we need a new president not only who cares the economy of the poor but who can lead people into total revolution including writing of the new constitution. we need Tanzania Constitution by 2011. :decision:
If we manage to do that, hata rais ataweza kushtakiwa pale ambapo atafanya utumbo. Hii ni muhimu kwa sababu ahata Rais atatekeleza kazi zake kwa uangalifu na kufuata sheria siyo kama Mkapa ambaye alikuwa anaamrisha piga risasi wazanzibari wakati walipoandamana.
:moony:

I dont think you need a new president, what you need is new constitution otherwise you will endup crying and with 1000 reasons including the one mentioned I doubt no one can take the country away from CCM. Tafakari na reflect yaliyotokea Kenya especial yaliyomkuta Raila Odinga au tafuteni si,u yake mumuuombe ushauri
 
Kweli Nyani haoni kundule:
JK, Salma, Rizonw, Miraji.........the list goes on!

Jibu hoya wewe ridhwan ni mbunge? na huyo miraji ni mbunge wa jimbo gani? Mnafanya JF inadharauliwa kwa ajili ya watu kama nyie hapa zimezungumziwa nafasi za ubunge ndani ya familia moja ndani ya chama kimoja cha upinzani! wewe sijui umejibu madudu gani halafu ndio mnataka nchi muongoze si bora hili zimwi tulijualo kuliko hilo tusilolijua? hofu yangu tusije kutawaliwa na watu wa kaskazini tu!
 
If you think changing the president ni tiba you are wrong kwa sababu for the same reason same people same external forces you will keep on changing presidents ad infinitum. Sokomo is right huenda tatizo lenye kichwa hapa ni katiba that makes sense for any open minded creature.
 
Jibu hoya wewe ridhwan ni mbunge? na huyo miraji ni mbunge wa jimbo gani? Mnafanya JF inadharauliwa kwa ajili ya watu kama nyie hapa zimezungumziwa nafasi za ubunge ndani ya familia moja ndani ya chama kimoja cha upinzani! wewe sijui umejibu madudu gani halafu ndio mnataka nchi muongoze si bora hili zimwi tulijualo kuliko hilo tusilolijua? hofu yangu tusije kutawaliwa na watu wa kaskazini tu!
Kam hoja ni ndugu au familia moja kuwa katika nafasi fulani basi hapa hoja imejibiwa na haina haja tena ya kuijadili,lakini kama unamaanisha kuwaq mbunge ndio kuwa katika uongozi wa nchi hii basi mimi napingana nawe na namsapoti NYUMBU kwani aliyoyasema ni sawa kabisa,hata kama aliowataja hawapo katika serikali lakini kwa hali halisi ilivyo sasa ni dhahiri wapo serikalini maana wanapata hata taarifa za serikali ambazo wabunge uliowataja ni vigumu kuzipata.
Cha msingi tuangalie tu ni namna gani tunaweza kulipeleka taifa letu katika maendeleo bila kujali ni nani yupo na ana uhusiano gani na mtu fulani katika serikali,mfano mzuri ni Uganda ya Museveni mkewe anafanya kazi kama kawaida kwa kuwajibika kwa wananchi.
 
Waalimu, "usalama wa taifa" a.k.a Usalama wa CCM, watumishi wa almashauri na tume ya uchaguzi. Hii ni kudhihirisha kwamba wapumbavu wanajiamini kiasi cha kuwapa waelevu amri za kufanya upumbavu, na waelevu kwa hofu yao wanakubali upumbavu kama alivyosema Dilunga (Raia mwema of this week)
 
Mafisadi siyo hao mnaowataja pekee. Naamnini mafisadi wanajumuisha na hawa wafuatao:

1. Mahakimu na makarani wote wa mahakama ambao wamegeuza mahakama kuwa minada ya haki za watu.

2. Wafanyakazi wote wa maofisini ambao wanaishi kwa 10% na kuchakachua zabuni.

3. Madaktari wote na manesi ambao wamekuwa ni vibaka wa madawa yetu yanayosambazwa na MSD.

4. Waalimu wote ambao wametugeuza wazazi na walezi wa wanafunzi wao kuwa dili kupitia tuitions, remedials, karatasi za mitahani ya mwisho wa wiki, etc.

5. Polisi wote ambao tunaingia bure na kutoka kwa hela.

6. Wenye visima vya maji wote huko mtaani ambao huwahonga DAWASCO wasifungulie maji, ili wafanye biashara.

7. Viongozi wote wa CHADEMA ambao wanataka kutuingiza KINGI tuchague chama kinachonuka ukabila na udini. Na kabla hamjaanza LIGI nataka kusema kuwa chama ambacho BABA, MTOTO, NA MKWE wote ni wabunge, yaani NDESAPESA, LUCY OWINYO NA KIHWELU, ni chama KIBOVU na uwezo wa kufikiri wa wanachama wake unatia shaka sana!

8. KWA NCHI HII NDUGU ZANGU ORODHA HAINA MWISHO!
afadhali chama cha kikabila kuliko cha kifamilia, kwa kuwa kinaweza kurudisha usultani, ccm ni chama cha familia ya kikwete, yaani jakaya, salma, ridhiwani, na akina miraj, wengine mlioko huko ni wasindikizaji
 
..... kifungu na wengine kushindwa kukibadilisha katika katiba ya jamhuri ya muungano wa Tanzania ya 1977.

Ibara ya 41 (7) ya marekebisho ya mwaka 1995 na 2005 chini ya Mwanasheria Mkuu A. J. Chenge inasema "iwapo mgombea ametangazwa na Tume ya uchaguzi kwamba amechaguliwa kuwa Rais kwa mujibu wa ibara hii, basi hakuna mahakama yoyote itakayokuwa na mamlaka ya kuchunguza kuchaguliwa kwake".

Hivi kila mtu na mambo yote si yako chini ya sheria? Sasa hili mbona linakuwa juu ya sheria? Hivi wewe Obama unakijua kifungu hiki cha katiba yetu mpaka ututolee mfano wa utawala bora, utawala wa sheria?

Orodha ni hii hapa:
1. hayati Mwalimu Nyerere
2. Ali hassan Mwinyi
3. Ben Mkapa
4. Jakaya Mrisho Kikwete
5. wabunge wote waliopitisha kifungu hiki na kukihusudisha
6. .......
7. ......

Ndio nami nawashangaeni humu ndani twakalia kupiga porojo za kura kura weeeeeeeeeeee huku KATIBA YA JAMUHURI inatufunga kwanza katiba ibadirishwe then twendeni kwenye uchaguzi, hapa twatwanga maji kwa kinu,

Lini tuanze kuijadili KATIBA YA JUMUHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA ili tujue mapema na wanachi waanze kuijua na kujipanga 2015 na ndipo kutakuwa na mapinduzi halali kwanza kwa wanaCCM na TAIFA kwa ujumla amini nawambieni bila katiba mpya kila kukicha tutaendelea kushindwa kujibu kwanini Tanzania na mali zote haiendelei kenya mwakani na miaka ijayo hatuto washika tena

 
Back
Top Bottom