Je, unaweza kutumia muda gani kurejea nyumbani baada ya kwenda kutafuta maisha?

Je, unaweza kutumia muda gani kurejea nyumbani baada ya kwenda kutafuta maisha?

Mr Lukwaro

JF-Expert Member
Joined
Jun 3, 2023
Posts
359
Reaction score
629
IMG_20230821_181803.jpg
Wanasema Mafanikio ni Mchakato. Ni mchakato unaochukuwa muda mrefu.

Now days imekuwa ni moja ya changamoto kwenye jamii na Familia zetu.

Watu wanapoenda kutafuta masha wanashindwa kurejea Nyumbani hata kwenye matukio ya ulazima kama vile "Misiba" "Sherehe" na hata mambo mengine kama vile Vikao vya familia.

Kwa utafiti wangu mdogo ,sababu kubwa imekuwa ni "Ugumu wa maisha, mipango haijakaa sawa kwa kuamini mpaka wapate hela ndo waweze kurudi Nyumbani" na n.k

Hii Ni tofauti na kipindi cha nyuma kwa babu zetu na Babu zetu.

Haya na wewe nambie, "Waweza tumia muda gani kurudi nyumbani baada ya kwenda kutafuta maisha?!"
 
Inaamuliwa na malengo yako, na unachorudi kukifuata ni kitu gani.

Mfano mimi nilienda USA, nikajenga Bongo, nikawa na mtaji.

Nikarudi maana nilikuwa na kwangu na ka balance ka Biashara.
 
Inaweza chukua hata miaka 7 au 10?

- Inafegeme na umri wako, uliowaacha na malengo. Mfano una miaka 25, hujaoa, na sio mtoto wa mwisho, kama kuna sababuhata miaka 20 ni sawa.

Mimi nilioa nina 30, nikaondoka, kurudi nikiwa na 45, ila mke alikuwa anakuja, akasoma, anarudi, anakuja, watoto wangu wote wana uraia wa Marekani.

Alikuwa akipata mimba, anakuja, anaielea mpaka anajifungua, alipomaliza kuzaa, akarudi, na wanawe, nikawa natuma hela, akajenga, then nikakaa tena kidogo, kukujikusanya.

Nikiwa na miaka 45 nikarudi, siwezi maliza maisha yangu nje ya Tanzania, huo ndo ulikuwa msimamo wangu thabiti.
 
Inaamuliwa na malengo yako, na unachorudi kukifuata ni kitu gani.

Mfano mimi nilienda USA, nikajenga Bongo, nikawa na mtaji.

Nikarudi maana nilikuwa na kwangu na ka balance ka Biashara.
Hongera
 
Kwangu ni Mwanza, nafanya kazi Arusha, ni miaka sasa, narejea kwangu kuona familia kila baada ya mwezi 1 au miezi miwili, swala la utafutaji kwa Dunia ya sasa tunaenda popote na tunarejea baada ya muda, kuhusu maswala ya familia kwa maana ya nyumbani kwetu kwenye uzao wa baba au mama, hua tunaangalia mazingira na nyakati ambazo matukio hutokea, kwamba unaweza kwenda au utaenda baadaye.

Dunia imekua na vifo, sherehe na matukio kadhaa, ukijajali yote eti kisa ni ndugu, hutoboi, utatumia pesa nyingi karibu kila mwezi huku maendeleo ya familia yako yanakukabili, binafsi hua sijali sana maana sometimes kipato chako ili kikidhinmaisha yako na familia yako, pia na ndugu ktk matukio yao,yakupasa kua na kipato kikubwa sana, na hiyo ni kwa watu wachache sana, ambao wakisikia msiba wa mjomba wa mjomba wake wanapanda ndege kwenda msibani kuzika na anarudi jioni.

Mwenzangu una mshahara wa laki8 una familia, ukisikia tukio unaanza kutafuta ticket ya bus, na ruhusa za kazini ambazo ni ngumu, maana kazi inatambua misiba ya Baba, Mama, mtoto, mke na mume, unashindwa kwenda kwa sababu unatumia bus siku nzima, ukae msibani siku mbili, uanze kurudi job siku nyingine nzima, siku ya nne ndo urejee ofisini, ni ngumu sana.

So sometimes mambo mengi kwa sasa kuhusu familia zetu hizi yapotezee na mengine yashiriki.
 
Back
Top Bottom