Je, upo tayari kujua tarehe yako ya kifo? AI death calculator inalo jibu

Bora usijue aise.
Kuna memba aliitwa Mpauko alileta thread ya kuonesha kuwa miezi mitatu baadaye angefariki kwa mujibu wa maelezo ya daktari wake. Ile thread ilituumiza sana maana hakuonekana tena.
Kujua kuna uzuri wake hususani katika kupangilia mambo yako muhimu.
 
Hata bure situmii fikiria kikabashili utakufa kesho itakuwaje yaanze mawazo tena bora nisijue kabisaa
 
Hiyo AI iboreshwe iwe na uwezo pia wa kutuambiwa kama ukisali kwa
Mwamposa ukanunua maji na kutoa sadaka kwa njia ya mtandao wake upata ticket ya kuingia peponi
 

Kwa wale wanaofuata mafundisho ya dini wanajua kabisa kuwa
Moja ya vitu Mungu hakutaka Kabisa Binadam wavifahamu ni siku ya Kufa.
 
Inatisha sana japo hata sasa ukitaka kujua umebakiza miaka mingapi ya kuishi inawezekana...

Ni wewe tu kuhitaji kujua.!
 
Hata bure situmii fikiria kikabashili utakufa kesho itakuwaje yaanze mawazo tena bora nisijue kabisaa
Mi mwenyewe siwez kukubali kukitumia. Kifo cha kutarajia kinatesa sn ndio maana wengine wakiambiwa wana ukimwi wanakufa siku sio zao.
 
Anajua mtu atakufa lini ni Mungu pekee yake si vinginevyo, hicho kifaa limebuniwa majini na maproo. Ukitoa tu detail zako wanaoingiza kwenye ulimwengu wa kishetani unaanza kupata matatizo
 
Haijaweza kubashiri kuwa Mtu akifa anakwenda wapi?🤣
 
Mmh teknolojia ni jitu la kuogofya sana wakati mwingine.
 
Bora walete kwasababu itatupa muda wa kujiandaa vyema kwenye mambo mengi.
 
Hicho kifaa kitajuaje kama mtu atakufa kesho kwa ajali ya Bodaboda?

Calculation zinaweza kufanyika kwa wagonjwa tu hasa wagonjwa wa Cancer coz inapigwa hesabu jinsi ugonjwa huo unavyo sambaa mwilini.
 
Hicho kifaa kitajuaje kama mtu atakufa kesho kwa ajali ya Bodaboda?

Calculation zinaweza kufanyika kwa wagonjwa tu hasa wagonjwa wa Cancer coz inapigwa hesabu jinsi ugonjwa huo unavyo sambaa mwilini.
Soma bandiko vizuri uelewe jibu lako lipo hapo.
 
Bora usijue aise.
Kuna memba aliitwa Mpauko alileta thread ya kuonesha kuwa miezi mitatu baadaye angefariki kwa mujibu wa maelezo ya daktari wake. Ile thread ilituumiza sana maana hakuonekana tena.
Mimi bila hata mujibu wa daktari siku nikijisikia kufariki lazima nitaaga humu ,sio kila mtu hajui atakufa lini.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…