kmbwembwe
JF-Expert Member
- Aug 16, 2012
- 10,892
- 7,780
Kwenye awamu ya nne elimu ilivurundwa sana hadi wahitimu wa form four kupangiwa chuo kikuu tena na kupewa mkopo kwa kisingizio cha kuandaa waalimu huku vigogo wakiwapangia jamaa zao ambao hata sifa hawana. Tulifikia mahali ambapo wahitimu form six walikua wanapangiwa vyuo vikuu binafsi kwanza hadi vijae wanafunzi wakati vyuo vikuu vya serikali vinakosa wanafunzi.
Chuo Kikuu cha Dodoma kwa mfano kilikua kinapata wanafunzi kama theluthi tu ya uwezo wake, wakati chuo kikuu cha Dar es Salaam nacho kilikua hakijai idadi ya wanafunzi. Yote hayo yalikua yanawezekana kutokana na viongozi vyuo binafsi kutoa rushwa kwa mamlaka za kupanga ambapo wanafunzi wakawa wanapangiwa vyuo binafsi japo maombi yao ni vvuo vya Serikali.
Katika awamu hii ya 6 yenye kushutumiwa kukubali kurejesha mafisadi serikalini na kukumbatia wafanyabiashara binafsi nimepata mshituko kuona binti wa ndugu yangu aliyefaulu vizuri masomo ya sayansi div 3 akiwa amepangiwa kwenda chuo cha uganga binafsi wakati hakuchagua chuo hicho. Ada kwa mwaka inastaajabisha kwa ukubwa kulinganisha na kama angepangiwa chuo cha serikali. Wazazi wa huyo jamaa yangu ni watu wenye uwezo mdogo kifedha na wanaona hawata mudu gharama hizo.
Kutokana na hiki nilichokijua inaelekea kile kilichodhibitiwa na awamu ya tano kimerejea tena.
Hapo nyuma kabla ya ufisadi kokomaa kwenye awamu ya nne vyuo binafsi vilikua na utaratibu wao binafsi wa kupata wanafunzi na sio kupangiwa na serikali.
Kwa maoni yangu naomba uongozi wa samia kujihadhari na vigogo kwenye serikali yake wanaojidai kuleta taratibu mpya kila nyanja kama ndio njia bora. Ukweli ni mafisadi tu wala rushwa wabaya na wataifarakanisha serikali ya CCM na wananchi.
Chuo Kikuu cha Dodoma kwa mfano kilikua kinapata wanafunzi kama theluthi tu ya uwezo wake, wakati chuo kikuu cha Dar es Salaam nacho kilikua hakijai idadi ya wanafunzi. Yote hayo yalikua yanawezekana kutokana na viongozi vyuo binafsi kutoa rushwa kwa mamlaka za kupanga ambapo wanafunzi wakawa wanapangiwa vyuo binafsi japo maombi yao ni vvuo vya Serikali.
Katika awamu hii ya 6 yenye kushutumiwa kukubali kurejesha mafisadi serikalini na kukumbatia wafanyabiashara binafsi nimepata mshituko kuona binti wa ndugu yangu aliyefaulu vizuri masomo ya sayansi div 3 akiwa amepangiwa kwenda chuo cha uganga binafsi wakati hakuchagua chuo hicho. Ada kwa mwaka inastaajabisha kwa ukubwa kulinganisha na kama angepangiwa chuo cha serikali. Wazazi wa huyo jamaa yangu ni watu wenye uwezo mdogo kifedha na wanaona hawata mudu gharama hizo.
Kutokana na hiki nilichokijua inaelekea kile kilichodhibitiwa na awamu ya tano kimerejea tena.
Hapo nyuma kabla ya ufisadi kokomaa kwenye awamu ya nne vyuo binafsi vilikua na utaratibu wao binafsi wa kupata wanafunzi na sio kupangiwa na serikali.
Kwa maoni yangu naomba uongozi wa samia kujihadhari na vigogo kwenye serikali yake wanaojidai kuleta taratibu mpya kila nyanja kama ndio njia bora. Ukweli ni mafisadi tu wala rushwa wabaya na wataifarakanisha serikali ya CCM na wananchi.