Je uwezo wa kimaisha wa Tanzania (Purchasing Power) ni mkubwa kuliko Nigeria?

Je uwezo wa kimaisha wa Tanzania (Purchasing Power) ni mkubwa kuliko Nigeria?

The Assassin

JF-Expert Member
Joined
Oct 30, 2018
Posts
4,942
Reaction score
20,077
Naomba kuuliza wachumi, je uwezo wa kimaisha ama kiwango cha kimaisha cha watanzania ni kikubwa kuliko cha wanigeria?

Nauliza hivyo kwa sababu nilikua natumia YouTube Premium Service (You Tube ambayo haina matangazo, unaweza ku download video, unaweza kuangalia ama kusikiliza hata screen ya simu ikiwa off nk) kutoka Nigeria

Juzi You Tube wakanitumia email kwamba wananifungia kwa sababu nilijisajili kwa kudanganya naishi Nigeria kumbe naishi Tanzania. Hivyo wakanitaka kama nahitaji huduma ya premium nilipie gharama za Tanzania.

Ni kweli nilijiunga 2020 you tube premium kwa kutumia VPN nikidanganya naishi Abhu Dhabi, hapa nilikaa kisha nikahamia Lagos Nigeria kumbe niko Tandale kwa mfuga Mbwa. Hii ni kwa sababu kipindi hicho huduma ya premium haikua inapatikana Tanzania.

Gharama ya Abhu Dhabi ilikua Dolar za Marekani 8, nilipohamia Nigeria nikawa nalipia chini ya Dola moja ama Naira 1,100 sawa na shilingi 2,000 za kitanzania.

Ajabu You Tube wameniletea gharama za Tanzania zinaanzia 4,500 kwa mwanafunzi na 8,700 kwa mtu binafsi na kwa 15,400 kwa familia ya watu 15.

Swali, je Tanzania Purchasing Power ni kubwa kuliko Nigeria, kwa nini sisi tupate huduma kwa bei ya juu kuliko Nigeria?
Screenshot_20240620_180603_Gmail.jpg

Screenshot_20240620_180536_Gmail.jpg

 
Back
Top Bottom