Je Wajua Ayam Cameni ni kuku Weusi mpaka nyama na kiini cha Yai?

Je Wajua Ayam Cameni ni kuku Weusi mpaka nyama na kiini cha Yai?

BigBaba

JF-Expert Member
Joined
Feb 7, 2017
Posts
1,908
Reaction score
9,040
341d5bc27fa44dfbe90fdd77ef2c1c06.jpg


1. Hao kuku wanaitwa Ayam Cameni , Ni Weusi kwa kila kitu mpaka nyama na kiini cha Yai,

2. Waligunduliwa nchini Indonesia Karne ya 17 na bado hawapatikani nchi nyingi Hadi sasa

3. Nchini Marekani waliingia mwaka 1998 na Yai moja la kuku Hawa nchini marekani linauzwa dola $130 Karibia Shilingi laki 3 za kitanzania

4. Kuku mzima nchini marekani anauzwa dola $2500 Takribani shilingi millioni 5.5 za kitanzania

5. Nyama yake inadaiwa Kuwa tofauti kidogo lakini inadaiwa Kuwa tamu zaidi kuliko kuku wa kawaida waliozoeleka

6. Wengine nchini Indonesia wanaamini kula nyama ya kuku hao inaongeza kinga ya mwili

7. Kula kiini kibichi cha Yai la kuku Hawa inadaiwa inasaidia Wanawake wajawazito wanaopata uchungu wa kuzaa muda mrefu kujifungua vizuri

Lakini mpaka sasa habari zinasema bado hakuna tafiti nyingi za kutosha wala kuridhisha ukweli wa mambo mbali mbali kuhusu kuku Hawa sababu bado hawajaenea nchi nyingi mpaka sasa
 
hao kuleni wenyewe,kuku anauzwa ghali kuliko farasi,what for?
 
Ukiwa unapika kipande cha mkaa kikadondokea kweny sufuria utakuja kugundua wakati Kiko mdomoni!
 
Wangekuwa na nguvu za kiume hapo sawaa
 
Hao kuku inabidi muwalete huku chugga tuwapelekee wakina Joh Makini wao si wanaitwa Weusi? kwa hiyo tunawaletea mweusi mwenzao!!
 
Back
Top Bottom