Je, wajua haramu isipoharimishwa inageuka halali? Na batili isipobatilishwa inageuka halali. Je, tuhalalishe ubatili huu kwa mhimili wetu wa Bunge?

Nimekuelewa Sana Mayala
Mkuu Kajabila, asante kwa kunielewa, pale ninapopandisha bandiko humu, hata kama watu 100 hawata nielewa, huwa nafarijika sana, pale anapotokea angalau mmmoja aliyenielewa, this means much to mě. Thanks.
P
 
Habari njema kwa watu wote, pendekezo No. 3 na No. 4 Katika bandiko hili, limetekelezwa kwa asilimia 100% kama lililopendekezwa.
Hivyo sasa ule ubatilifu katika barua ya Kujiuzulu kwa JYN umeondolewa kama nilivyo shauri, na kuwasilishwa barua halali,
Hivyo ile taarifa ya JYN kwa waandishi wa habari, kuwa ameandika barua kwa Katibu Mkuu CCM, sasa imebatilishwa na imefutwa kwenye website ya Bunge, barua rasmi ni kwa Katibu wa Bunge, na CCM kupewa nakala.
Hongera sana Bunge letu tukufu kuubatilisha ubatili huu. Sasa kwenye hili la Spika umebaki ubatili mmoja wa Naibu Spika, Dr. Tulia Akson kujiuzulu u Naibu Spika, kabla ya kugombea Uspika.
P
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…