Mpaka sasa ambao hatuchepuki 7 - 0 wanaochepuka kwa faida zifuatazo:
1. Afya ya kimwili kwa kuepushwa na magonjwa ya zinaa na HIV.
2. Kuimarika kiuchumi sababu hakuna cha bure popote pale duniani.
3. Nguvu za kiroho za kutosha kwa kutovamiwa na mapepo kama "jini mahaba"
4. Amani ya ndoa iliyoshibishwa na furaha, upendo, kuaminiana na kuthaminiana na Mke mmoja.
5. Kutozeeka mapema kwa sababu ikiwa goli 1 la Me aliyefika kileleni ni sawa na Mtu aliyekimbia KM 7, kwa Mke mmoja 3 × 2 = 6 kwa wiki 1.
6 × 4 wiki (mwezi) mmoja = 24 KM × 12 miezi = KM 288(Mwaka mmoja) kwa Ke mmoja, je wewe mwenye Ke wawili (Ke halali na Mchepuko) = KM 576, kwa chakula kipi utumiacho kinachojenga mwili kiafya wala si kujaza tu tumbo?
Sababu spermatogenesises (gametiume) za kutungisha ujauzito zatakiwa zizalishwe mwilini kwa wiki 7.
6. Kuepukana na mawazo yasiyo na ulazima, ikiwa Ke wote wawili wakikuzingua kwa nyakati tofauti kwa mwezi mmoja, je utakuwa unatatua vipi matatizo ilihali hapo hapo una changamoto za kikazi, kibiashara, Ndugu, Rafiki au Jamaa na matatizo yako binafsi.
7. Ulinzi wa baraka za Mungu kimwili, kiafya, kiakili na hata kiroho kwa sababu imeandikwa;
1 WAKORINTHO 6:18.
"Ikimbieni zinaa. Kila dhambi aitendayo mwanadamu ni nje ya mwili wake; ila yeye afanyaye zinaa hutenda dhambi juu ya mwili wake mwenyewe.
METHALI 6:32-33.
Mtu aziniye na mwanamke hana akili kabisa;
Afanya jambo litakalomwangamiza nafsi yake.
Atapata jeraha na kuvunjiwa heshima;
Wala fedheha yake haitafutika.
Sent from my CPH2185 using
JamiiForums mobile app