Je, wajua kuwa Shetani naye ana amri zake? Ziko 11

Je, wajua kuwa Shetani naye ana amri zake? Ziko 11

Vitabu vimesema Mungu hataki watu wavuguvugu

Kama wamoto bakia wamoto, kama wabaridi bakia baridi ila usiwe vuguvugu

Kwanini unakua vuguvugu?
Hapana imeandikwa usihukumu usije uka hukumiwa!........ hiyo ni vile weye unaona ni hukumu sahihi dhidi yangu!! lkn mie ni moto! lakini pia ujue shetani anatumia watu kupotosha watu! uonavyo wewe sivyo nilivyo! ila umeniona kwa njia ya kipepo zaidi! ili upotoke!!

siku zote shetani atakuonyesha mapungufu tuu! mfano unaweza ona kabisaa mchungaji wako anaingia guest na kimwana, utabaki kuona kuumbe hkn uungu ndani yake! bila kujua kwamba wale wanajaribiwa mno na shetani!!..... mwenzako jioni anatubu wewe unateketea!

Mie kuwa Baridi sometimes ni sawa!! ili imani yangu ikomae!!! hata manabii walioongea na Mungu, live wali jaribiwa sana tu! tena binafsi napenda kuyashinda majaribu, na ukiona ivo!! ni shetani amenijaribu! siyo kwamba mie siwezi jaribiwa! naweza kujaribiwa sana km yesu alivyo jaribiwa na shweitani!!

bila shaka km ungemuona Yesu alivyo bebwa na shetani kumpeleka mnalani kumjaribu wewe ungekufa moyo, sababu ungesema kuumbe hawa wanaelewana mbona wamebebana wkt wa mfungo? tena bila vurugu! bila shaka ungejiuliza daa! jamaa anaenda kugonga msosi kwa siri!! anatudanganya sisi kuwa amefunga?
 
Kwasababu umesema umeumbwa na mungu, maana yake hujazaliwa na mama yako
Huku nielewa Mkuu! Binafsi sijaumbwa na mungu wako huyo! kabisaaa! kwanza kamwe hawezi! hata kujaribu! wala kufikiria.tena umetamka vizuri tu! huyu mmoja kaniumba, na huyu Mama kanizaa! sasa unashindwaje kuona tofauti ndogo km hii Mkuu!

Ndiyo! kwa maana nyingine tena umesema vizuri sana, binafsi yupo mwenyewe!! nimeumbwa nae haswaaaaaa! sijakosea!! na niko ivo! Mama yangu yule alitumika tu km gari la kunileta Duniani yaani kanizaa tu!

kumbuka siyo kila Binadamu unae muona mwenye mwili ni ameumbwa na Bwana, ninae mjua sisi tulio wake tuna jijua! ujue! tena ni rahisi sana kuwa jua wasio watoto wake, yaani wale wasio ndugu zetu!
 
Najua Haters mtapinga tu hizo Amri za Shetani lakini Mwamba kapiga mle mle!! Mtapinga kwa ubishi tu, na wivu dhidi ya nondo za maana kwavile tumeaminishwa Mwamba sio kabisa, ingawaje kiuhaliisa, tunampigia shangwe... tena za kibingwa!

Ukweli usemwe, Mwamba hakukurupuka kama Bwana Yuleee!! Amri zake zimesimama na practical kuzidi hata zile alizotuletea Bwana Yule ambazo ni Impractical... hazitekelezeki maabara wala kwenye karakana!

Just imagine! Hakuna aliyekutaka ushauri wala kukuuliza lakini from nowhere"...oh, najua uukitaka kutoboa usawa huu, wekeza kwenye kilimo Chifu! Maparachichi yanalipa big time! Amini usiamini Chifu, parachichi ni Green Gold"

Pumbaaavu! Kwani we mwenyewe hutaki kutoboa? Ina maana huzitaki hizo Green Gold?! Kwamba Njombe wanakochimbua hizo green gold hukujui, ama?!

Nenda kalime mwenyewe hayo maparachchi, kenge wewe... kwani nimekuomba ushauri? Unakuta mwingine hujamuuliza wala nini halafu eti anakushauri upande miti gani sijui ambayo kuivuna ni sawa na kifungo cha Sabaya! Hivi zimetimia kweli wewe? Yaani kosa la babako mwenyewe aliyeshindwa kukulipia ada ya kusoma kozi uitakayo, na matokeo yake ukaishia kusomea Misitu SUA, halafu umeona mi ndo wa kunidoshea jumba bovu? Unajifanya kutoa ushauri bila kuombwa ili upate sababu ya kupiga mizinga, sio?

Tena Wabongo kwa kupenda kutoa ushauri.... dah!!

Mnyonge mnyongeni, haki yake mpeni! Mwamba anajua! Unanipigia stori za matatizo yako kwani yananihusu nini wakati mwenyewe nina matatizo kibao?! Nenda kasimulie kanisani au msikitini huko, kama nako hawajakuona tapeli tu!
Haaaa eti miti umri wa kuvuna sawa inankifungo cha sabaya
 
Bonge la mada hii.

Huwa najiulizaga sana, shetani kabla ya kumuasi Mungu, ni siri gani za KiMungu alizoiba ambazo Mungu hakuweza kumnyang'anya? Lazima kuna siri kama hizi kanuni alizochukua zilizompa nguvu kubwa ndiyo maana kumshinda ni kisanga.

Ndiyo maana kuna watu wanaona mbona hizi kanuni zinafanana na za Mungu, ila tukumbuke Mungu anahukumu binadamu kutokana na lengo, nia au intention ya binadamu katika kutenda jambo fulani na siyo kwa kuangalia tu tendo lenyewe. Hapo tofauti kubwa ndipo ilipo.

Ziangalieni hizo kanuni kwa umakini mtaona kitu fulani.
Hamna hiko kitu hizo ni hadithi za wayahudi. Binadamu alipoanza kula na kushiba ndio ubongo wake ukaanza waza mambo alipogundua moto ndio akapata muda wa kusociolize kutengeneza dini na mungu . Yani hizo hadithi za mungu na shetani zipo vichwani mwetu tuu na ni idea za wayahudi ndio maana sehemu nyingine hawana idea za shetani wala mungu .
 
Hii ya 11 nilimuonya mtu aache akajifanya kichwa maji sasa ket me destroy them they will cry the whole clan
Screenshot_20211111-092622.jpg
 
Back
Top Bottom