Je, wajua mila na desturi vilivyochangia ongezeko kubwa la UKIMWI Kagera?

Je, wajua mila na desturi vilivyochangia ongezeko kubwa la UKIMWI Kagera?

ichumu lya

JF-Expert Member
Joined
Aug 11, 2016
Posts
2,651
Reaction score
2,790
Mnamo miaka ya 1988 Mkoa wa Kagera ulikumbwa na janga la UKIMWI, wakati huo hakukua na elimu yoyote juu ya maambukizi na jinsi ya kujikinga, hakukuwa na kindomu hata watu waliotahiliwa walikuwa wachache, matumizi ya vifaa kama sindano, pini na nyembe vilitumika hovyo ungekuta mashuleni pini moja inatumika kutoa funza darasa zima muingiliano wa damu ulikuwa mkubwa.

Walitokea wafanya biashara waliosafiri mipakani kutafuta pesa hasa kwenye magulio makubwa kama Rukunyu na Kikomera, Katerero nk. Huko magulioni yalifanyika mengi ikiwamo ulevi uzinzi na mengine mengi ndio hapo wengi wao walijikuta wakiambukizwa UKIMWI. Watu hao waliporudi makwao walirudi na mali pamoja na UKIMWI nakumbuka miaka hiyo UKIMWI ilijulikana kama JULIANA AU SILIMU kwa Kihaya.

Maambukizi yalifika vijijini nakumbuka vijiji kama Kanyigo, Buyango, Bugandika, Kiziba, Kyamutwara na maeneo mengine nyumba zilifungwa baada ya familia nzima kufariki ukipita kwenye maeneo tajwa utadhani ni makaburini.

Utamaduni wa Kihaya ulichangiaje maambukizi ya UKIMWI?

Ikumbukwe Wahaya wanatamaduni nyingi ikiwamo ya mtu anapofariki wanazika baada ya mazishi wanakaa siku mbili mpaka nne basi ndugu watoto wazazi na jamaa wa karibu hunyolewa nywere miaka hiyo walitumia wembe ungekuta kikundi cha watu 20 wananyolewa na mtu mmoja tena kwa wembe mmoja mpaka ukikatika kibaya zaidi walinyolewa vipara kitendo kilichopelekea damu kuingiliana kutokana na maumbile au na magonjwa ya ngozi unakuta mtu ana vipere kichwani na mwingine na wembe haukuoshwa baada ya Kumaliza mtu mmoja badala yake walipangusa kwenye kitambaa na kuendelea.

Kwa hiyo kwa siku moja watu zaidi ya 20 walijikuta wanambukizwa UKIMWI pasipokujua.
Misiba ilikuwa ni mingi kufika miaka ya 1992 watu wengi walikuwa wameathirika sana na ndipo taadhari ilianza kuchukuliwa.

Tafiti nyinyi sana tena za wasomi wakiwemo kina NSHOMILE Maprofesa na madakitari wote waliangukia pua kwa kutueleza kuwa marehemu wengi waliendekeza ngono zembe bila kufafanua watoto walifanya ngono na kina nani.

Kwa uzembe huu wa Wizara ya afya wahanga wana kila sababu ya kudai fidia na serikali kuwajibika kwa kushindwa kutimiza majukumu yao.

Nina ushahidi na mifano hai jinsi ambavyo Wahaya waliangamia kwa kukosa maarifa.
Ni mambo mengi sana yanyohusu UKIMWI Wahaya na serikali lakini niombee nikamilishe kitabu chenye utafiti wa kina kitakachozua maswali mengi kwa wanazuoni.
_99030932_633e5171-a7ef-416a-a384-1992eaf3675d.jpeg


Sio hiyo tu miaka iyo kulikuwa na funza wengi sana watu wa miaka iyo wengi wao hawana kucha miguuni na wengine miguu iligeukia upande kutokana na vidonda vilivyosababishwa na funza hao anaeleza " tulitumia pini moja darasa zima uku tukisimamiwa na Waalimu kwa viboko mgongoni hatukupewa muda wa kusafisha izo pini matokeo yake tulijikuta tuchangia kusambaza magonjwa Paspokujua".

Kwakweli Serkali hii ilitenga mkoa wa Kagera tangia zamani ndio maana ata waathirika wa vita vya Idd Amini hawakupewa fidia wakati serkali ndio ilimchokoza nakusababisha vita iliyoathiri Mkoa wa Kagera mpaka leo.

Wakati mwingine nikifikiri jinsi serkali hii sikivu inavyotenda kazi kwaubaguzi nabaki namlilia Mungu. Tukiorodhesha majanga ya Kagera na jinsi yilivyoshughlikiwa najua kila mtu atashika mdomo.

NB: HUJUMA HIZI ZINA MWISHO NA MWISHO WA MNAFIKI NI AIBU.

======

Upungufu wa Kinga Mwilini (kwa kifupi UKIMWI; kifupisho cha Kiingereza AIDS) ni ugonjwa unaotokana na virusi ambavyo kwa Kiswahili vinaitwa kifupi VVU ("Virusi vya UKIMWI"; kwa Kiingereza: HIV, yaani "Human Immunodeficiency Virus") na vinashambulia mwili kwa kuondoa nguvu zake za kupambana na maradhi.

Ukimwi ni ugonjwa hatari sana katika maisha ya binadamu kwa kuwa husababisha vifo (yaani kupotea kwa uhai wa watu hao). Kwa mujibu wa Shirika la Afya Duniani, kufikia mwaka 2014 ugonjwa huu umeua watu milioni 39, hasa kati ya wanaoishi barani Afrika upande wa kusini kwa Sahara. Kwa mwaka 2015 pekee wamefariki watu milioni 1.2 na kati yao watoto wengi.

UKIMWI umekuwa na madhara makubwa katika jamii, kama ugonjwa wa mwili na kama chanzo cha ubaguzi. Kuna sintofahamu kuhusu UKIMWI kama vile kwamba eti, unaweza kusambazwa kwa kugusana tu bila ngono.

Ugonjwa huu pia unasababisha madhara ya kiuchumi ambayo ni makubwa, hasa kwa nchi maskini.

UKIMWI hadi hivi sasa haina chanjo wala tiba, lakini tunaweza kuuepuka ugonjwa huu kwa kuachana na ngono ambayo huweza kusababisha ugonjwa huo, pia tunaweza kujikinga nao kwa kuepuka kuchangia vifaa au vitu vyenye ncha kali.

Kimsingi zaidi ni kwamba ugonjwa huo umetokana na kuenezwa hasa na maadili mabovu. Dhidi yake watu wanahitaji kuelewa tangu utotoni na ujanani maana ya jinsia na maisha kwa jumla, kwamba vinadai upendo, nidhamu na uwajibikaji, si kufuata tamaa tofautitofauti daima[1].
1576076110665.png

Tarehe 1 Desemba kila mwaka ni siku ya UKIMWI duniani.
 
Umeongea ukweli mwingi lakini tema mate chini kwanini serikali waidai ndiyo iliyowaambukiza refer to majibu ya tetemeko , " serikali hakuleta tetemeko kwannn ikujengee?"
Mwisho wa kunukuu
 
Ubabe hauondoi ukweli na ukweli unatabia ya kujitete, kizazi kitapita lakini ukweli utadumu milele.
Umeongea ukweli mwingi lakini tema mate chini kwanini serikali waidai ndyo iliyowaambukiza refer to majibu ya tetemeko , " serikali hakuleta tetemeko kwannn ikujengee?"
Mwisho wa kunukuu
 
ichumu lya,
Una maana gani kusema ''kudai fidia''? Ninavyojua UKIMWI kipindi hicho ilikuwa haujulikani vya kutosha, na siyo Tanzania tu bali duniani kote. Juhudi nyingine zote unazoziona sasa zimekuja baada ya watu kuujua. Kipindi hicho siyo Kagera tu hata Dar kuna jamaa mmoja mchaga alikuwa na msichana wa kihaya akamwambukiza.

Alipougua alirudi kwao na watu walikuwa wanasema amelogwa. Hakuna aliyekuwa anajua juu ya UKIMWI. Baada ya kufariki na muda mrefu kupita ndiyo watu wakaja kuelewa kumbe dalili alizokuwa nazo zote zilikuwa ni za UKIMWI.
 
Nadhani hukunielewa kabisa.Swala la kutojulikana haliondoi lawama kwa serkali kushindwa kutoa taadhali mambo aya yamekuwa yakiendelea lakini hakuna taadhali. Mpaka sasa kuna mila zinaendelea ikiwamo ya ukeketaji, kunyoa vipara misibani kwakutumia kifaa kimoja kisicho salama so katika ili wizara husika lazima iwajibike kwa maana ya serkali.

Tatizo Waafrika hawana desturi ya kuwajibika ndio maana kuna visheria vinatungwa kulinda watawala.
Una maana gani kusema ''kudai fidia''? Ninavyojua UKIMWI kipindi hicho ilikuwa haujulikani vya kutosha, na siyo Tanzania tu bali duniani kote. Juhudi nyingine zote unazoziona sasa zimekuja baada ya watu kuujua. Kipindi hicho siyo Kagera tu hata Dar kuna jamaa mmoja mchaga alikuwa na msichana wa kihaya akamwambukiza. Alipougua alirudi kwao na watu walikuwa wanasema amelogwa. Hakuna aliyekuwa anajua juu ya UKIMWI. Baada ya kufariki na muda mrefu kupita ndiyo watu wakaja kuelewa kumbe dalili alizokuwa nazo zote zilikuwa ni za UKIMWI.
 
Kwa hiyo Wahaya ndo wamesambaza UKIMWI Tanzania nzima?
 
Nadhani hukunielewa kabisa.Swala la kutojulikana haliondoi lawama kwa serkali kushindwa kutoa taadhali mambo aya yamekuwa yakiendelea lakini hakuna taadhali. Mpaka sasa kuna mila zinaendelea ikiwamo ya ukeketaji, kunyoa vipara misibani kwakutumia kifaa kimoja kisicho salama so katika ili wizara husika lazima iwajibike kwa maana ya serkali.

Tatizo Waafrika hawana desturi ya kuwajibika ndio maana kuna visheria vinatungwa kulinda watawala.
Lakini kila siku hayo mambo yanakemewa. Ni juu ya wananchi kubadilika.
 
Binadamu wabishi sana
Pamoja na yote hayo yaliyotokea miaka hiyo lakini sasa ndio UKIMWI utafikiri ndio umeanza, maana kila leo badala upungue ndio unaongezeka pamoja na condom watu wanapiga kavu makusudi
 
Yanakemewa kisiasa sijaona msisitizo wa jambo hili, mfano watu walipogoma kujiandikisha uliona matangazo mpaka Rais wa nchi aliinuka.
Lakini kila siku hayo mambo yanakemewa. Ni juu ya wananchi kubadilika.
 
Kuna waliondikiwa kufa kwa UKIMWI hao huwezi kuwazuia ila wengine nibahati mbaya wanakutana nao kwa njia zisokuwa za ngono.
Binadamu wabishi sana
Pamoja na yote hayo yaliyotokea miaka hiyo lakini sasa ndio ukimwi utafikiri ndio umeanza, maana kila leo badala upungue ndio unaongezeka pamoja na condom watu wanapiga kavu makusudi
 
Kuna waliondikiwa kufa kwa UKIMWI ao huwezi kuwazuia ila wengine nibahati mbaya wanakutana nao kwa njia zisokuwa za ngono.

Kweli Mkuu nimesikia sana kuhusu waliopata maradhi Haya kwa njia tofauti
Inasikitisha sana
 
Jiulize familia ya watu kumi wote wanafariki kwa UKIMWI kuanzia baba mpaka mjukuu mpaka nyumba inafungwa mashamba yamekanda jumba linabaki na majoka na mizimu.
Kweli Mkuu nimesikia sana kuhusu waliopata maradhi Haya kwa njia tofauti
Inasikitisha sana
 
Tatizo %70 ya Watanzania wamekulia kwenye siasa na uongo hawataki kusikia ukweli. Ni lini wizara ya afya imeliweka jambo ili wazi? Ndiyo maana nikasema kuna haja ya serkali kukiri udhaifu huu na waanga kudai fidia.

Sema tumekuwa na watawala wa hovyo waliojaa viburi wasiokubali kama wamekosea, tafiti nyinyi zinaonyesha waliokufa kwa UKIMWI miaka iyo wengi waliupata kwa ngono lakini sio kweli wengi waliupata kwa njia nilizohainisha wachache ndo waliupata kwa ngono.

Nilini watawala wa Africa watakubali kuwajibika?
 
ichumu lya, Nakumbuka hiki kipindi kilikuwa kigumu sana.

Taasisi za kupambana na Ukimwi walielimisha kwa kuonesha bure sinema za waathirika kama sehemu ya uelimishaji wa kupambana na hilo gonjwa. Kuna nyumba zilifungwa kwa kukosa mtu wa kuishi.

Ila hili la viwembe kusababisha maambukizi mapya ndio nalisikia hapa. Mdau, hili ni jambo zito sana. Je jambo hili limefanyiwa utafiti wwte wa kina au ni mtazamo/hisia/maoni wako binafsi? Nachojua huo utaratibu wa kuchangia viwembe ulikuwepo kwenye jamii nyingi tena bila kujali kama kuna msiba.
 
Jiulize familia ya watu kumi wote wanafariki kwa UKIMWI kuanzia baba mpaka mjukuu mpaka nyumba inafungwa mashamba yamekanda jumba linabaki na majoka na mizimu.
Hii imenifikirisha kwa kweli. Ni kweli sikuwa najua namna gani nyumba nzima inaangamia kwa ugonjwa huo (Tuliambiwaga kuwa ni kwa sababu ya kuwahudumia wagonjwa pasipo kujikinga but mh........) Ahsante mkuu angalau ya wembe nimeielewa.
 
Nakumbuka hiki kipindi kilikuwa kigumu sana.

Taasisi za kupambana na Ukimwi walielimisha kwa kuonesha bure sinema za waathirika kama sehemu ya uelimishaji wa kupambana na hilo gonjwa. Kuna nyumba zilifungwa kwa kukosa mtu wa kuishi.

Ila hili la viwembe kusababisha maambukizi mapya ndio nalisikia hapa. Mdau, hili ni jambo zito sana. Je jambo hili limefanyiwa utafiti wwte wa kina au ni mtazamo/hisia/maoni wako binafsi? Nachojua huo utaratibu wa kuchangia viwembe ulikuwepo kwenye jamii nyingi tena bila kujali kama kuna msiba.
Sijui unataka utafiti gani zaidi ya mashuhuda au niweke video za waanga ndio uamini au umekuwa Petro aliyetaka kuhakikisha makovu ya YESU. Mambo aya yamebaki kuwa siri mioyoni mwa wana KAGERA.
 
Sio hiyo tu miaka iyo kulikuwa na funza wengi sana watu wa miaka iyo wengi wao hawana kucha miguuni na wengine miguu iligeukia upande kutokana na vidonda vilivyosababishwa na funza hao anaeleza " tulitumia pini moja darasa zima uku tukisimamiwa na Waalimu kwa viboko mgongoni hatukupewa muda wa kusafisha izo pini matokeo yake tulijikuta tunachangia kusambaza magonjwa Pasipokujua".

Kwakweli Serkali hii ilitenga mkoa wa Kagera tangia zamani ndio maana ata waathirika wa vita vya Idd Amini hawakupewa fidia wakati serkali ndio ilimchokoza nakusababisha vita iliyoathiri Mkoa wa Kagera mpaka leo.

Wakati mwingine nikifikiri jinsi serkali hii sikivu inavyotenda kazi kwaubaguzi nabaki namlilia Mungu. Tukiorodhesha majanga ya Kagera na jinsi yalivyoshughlikiwa najua kila mtu atashika mdomo.

NB: HUJUMA HIZI ZINA MWISHO NA MWISHO WA MNAFIKI NI AIBU.

Hii imenifikirisha kwa kweli. Ni kweli sikuwa najua namna gani nyumba nzima inaangamia kwa ugonjwa huo (Tuliambiwaga kuwa ni kwa sababu ya kuwahudumia wagonjwa pasipo kujikinga but mh........) Ahsante mkuu angalau ya wembe nimeielewa.
 
Sijui unataka utafiti gani zaidi ya mashuhuda au niweke video za waanga ndio uamini au umekuwa Petro aliyetaka kuhakikisha makovu ya YESU. Mambo aya yamebaki kuwa siri mioyoni mwa wanaKAGERA.
ichumu lya, Kiongozi. Naona umeamua kutuletea stori za vijiweni. Jipange.
 
Kwa hiyo lengo la post yako ni kudai fidia tu
 
Back
Top Bottom