Je, wajua mtembea kwa miguu anatakiwa atembee upande upi ili aweze kuepuka ajali?

Je, wajua mtembea kwa miguu anatakiwa atembee upande upi ili aweze kuepuka ajali?

Chulumeshy

Member
Joined
Jul 27, 2022
Posts
17
Reaction score
11
1661858378673.png

Tembea upande wa kulia wa barabara,


ili uweze kuyaona vizuri na kupishana na magari yanayotoka unakoelekea na iwe pembeni sana iwezekanavyo.

Upande utakaotembea itakusaidia wewe kuliona gari vizuri au vyombo vingine vya usafirikama vile pikipiki, bajaji na kuweza kukuepushia na madhara yanayoweza kusababishwa na vyombo vya moto mfano ajali kutokana na matatizo ya ghafla kama vile kukatika kwa breki, kupoteza mwelekeo, pancha na mengine yanayoweza kuleta madhara kwa kufanya hivyo inasaidia kuepusha ajali zinazoweza kuepukika.

Usidhani kamwe madereva wanakuona

Wanaweza kuwa na mawazo au matatizo mbalimbali yawezekana kutokana na mambo mbalimbali yanayoendelea katika maish ya kila siku ya dereva huyo. Ni bora kuwasiliana macho na madereva ili kuhakikisha kuwa unaonekana. Dereva anaweza kukuona kwa urahisi kwa kuvaa mavazi ya rangi angavu wakati wa mchana. Usiku, vaa vifaa vya kuakisi, au tumia tochi.

Ajali zinaweza kuepukika kama watumiaji wa barabara watazingatia sheria za barabarani.

 
Uko sahihi, nimewahi shuhudia ajali kama hiyo aliyekuwa nyuma yangu aligongwa na bodaboda kwa namna ile ile kama kwenye hiyo video na kupoteza maisha asingegongwa yeye huenda tungekuwa sisi tuliokuwa mbele yake(marehemu) mita 5
 
Uko sahihi, nimewahi shuhudia ajali kama hiyo aliyekuwa nyuma yangu aligongwa na bodaboda kwa namna ile ile kama kwenye hiyo video na kupoteza maisha asingegongwa yeye huenda tungekuwa sisi tuliokuwa mbele yake(marehemu) mita 5
ulijifunza nn kupitia ajali hiyo
 
hili somo kubwa sana tulipewa enzi hizo secondary yani face upande magari yanatokea ili yakija hata likikosea njia unaweza kulikwepa... hadi leo natumia huu utaratibu
hongera hata mimi najitahidi kuzingatia sheria hiyo kwa sababu chombo hata kikiacha njia unaweza kukikwepa endapo unakiface kuliko kilicho nyuma yako
 
tangu siku ile nimekuwa nikitembea kulia pembeni kabisa mwa barabara, cha pili suala la usalama wangu barabarani simwachii mtumiaji mwingine wa barabara niwapo barabarani kwa kisingizio eti ananiona.
wow vzuri hata mm nazid kujifunza kupitia wew
 
Hiyo video inatisha, jamaa sijui alikuwa haoni!..anyway, hilo mimi nililijua mapema kipind niko bwana mdogo tu, nilikuwa nikikaa nafikiria hivi mbona kutembea kushoto ni risk sana, sikupenda kitu kinakuja kwa nyuma halafu sikioni, nikajiongeza kwa kuona bora upande wa kulia itakuwa ni afadhali kidogo basi toka miaka hiyo napendelea zaidi nikitembea kwa miguu natembea kuliani mwa barabara ila bado inabidi uwe makini si umeona hiyo video hapo juu!...
 
Alisikika mlevi mmoja akisemaa ... "Malaika wanaotusindikiza usiku tulewapoo wanafanya kazi kubwa Sanaa"

Barabara haitabiriki, wanashauri utembee mwelekeo tofauti na magari
 
Back
Top Bottom