Je, wajua tarehe 5 Februari mwaka 1977 ni Siku iliyobeba matukio matatu ya kufurahisha na kuhuzunisha?

Je, wajua tarehe 5 Februari mwaka 1977 ni Siku iliyobeba matukio matatu ya kufurahisha na kuhuzunisha?

anonymousafrica

JF-Expert Member
Joined
Aug 24, 2016
Posts
611
Reaction score
640
images.jpg

Tarehe 05 mwezi Februari mwaka 1997 ilikuwa siku muhimu yenye matukio ya kufurahisha na kuhuzunisha. Kabla haujayapitia hayo matukio matatu, Kumbuka siku hii chama cha TANU na ASP viliungana na kuunda Chama cha Mapinduzi (CCM).

Lakini 1. ASP ilikuwa inatimiza miaka 20 tangu kuanzishwa kwake na siku hiyo ilikua inaagwa rasmi huko mjini Unguja. 2. Tuliadhimisha miaka 10 ya tangu kutangazwa kwa azimio la Arusha 3. Ndio siku ambayo umoja wa Afrika Mashariki ulivunjika.

Rais Kenyatta (Baba) akazishikilia ndege za shirika la ndege kwa kulimbikiza madeni ya matumizi ya uwanja wa Ekmbakasi. Ndege hizo zilibeba baadhi ya viongozi ambao walikuwa wanakuja nchini Tanzania kwa shughuli za kuundwa kwa CCM na MIAKA 10 YA AZIMIO LA ARUSHA
 
Kuagwa kwa ASP wimbo ulikwenda kama hivi:

Afro mama tunakuaga, si kama umetufanyia baya, muungano kwetu ni usawa Afro (mistari mingine nimesahau).

Mambo yalikuwa live kwenye TV enzi hizo TVZ na bara hakuna TV wao labda wakisikiliza kwenye radio RTD.

Ila pale ndiyo fedha zilipigwa kweli kwenye zile sherehe.
 
Kuagwa kwa ASP wimbo ulikwenda kama hivi:
Afro mama tunakuaga, si kama umetufanyia baya, muungano kwetu ni usawa Afro.. (mistari mingine nimesahau).

Mambo yalikuwa live kwenye TV enzi hizo TVZ na bara hakuna TV wao labda wakisikiliza kwenye radio RTD.

Ila pale ndiyo fedha zilipigwa kweli kwenye zile sherehe.....
hahahahaaa nakuona mhenga
 

Tarehe 05 mwezi Februari mwaka 1997 ilikuwa siku muhimu yenye matukio ya kufurahisha na kuhuzunisha. Kabla haujayapitia hayo matukio matatu, Kumbuka siku hii chama cha TANU na ASP viliungana na kuunda Chama cha Mapinduzi (CCM).

Lakini 1. ASP ilikuwa inatimiza miaka 20 tangu kuanzishwa kwake na siku hiyo ilikua inaagwa rasmi huko mjini Unguja. 2. Tuliadhimisha miaka 10 ya tangu kutangazwa kwa azimio la Arusha 3. Ndio siku ambayo umoja wa Afrika Mashariki ulivunjika.

Rais Kenyatta (Baba) akazishikilia ndege za shirika la ndege kwa kulimbikiza madeni ya matumizi ya uwanja wa Ekmbakasi. Ndege hizo zilibeba baadhi ya viongozi ambao walikuwa wanakuja nchini Tanzania kwa shughuli za kuundwa kwa CCM na MIAKA 10 YA AZIMIO LA ARUSHA
Tarehe 05 mwezi Februari mwaka 1997

Mkuu umeona lkn huo mwaka uliouandika hapo?
 
Kwa hiyo siku hiyo ndio iliyozaa matatizo yote Tanzania,kutokana na Chama cha Nyerere kuweka misingi ya hovyo ya uongozi na uchumi.
 
Back
Top Bottom