Je, Wakristo wanaongoza kubaguana kuliko dini nyingine?

Je, Wakristo wanaongoza kubaguana kuliko dini nyingine?

Girland

JF-Expert Member
Joined
Jan 24, 2016
Posts
2,489
Reaction score
4,253
Nimejaribu kuangalia hali ya upendo Kati ya madhehebu mbalimbali ya Kikristo, hali inasikitisha. Kila dhehebu linahubiri upendo kivyake ilhali wanawabagua wenzao wa dhehebu lingine.Hali hii inasababishwa na nini Je Kristo amegawanyika?

Binafsi familia niliyotoka nimefanikiwa kuona SDA (Wasabato) VS RC (Wakatoliki),huwezi kuamini kwamba wanatumia kitabu kimoja (BIBLE). Ushakutana na vita ya WALOKOLE (TAG, EAGT, EFATHA, MAKANISA YA MANABII) VS hao wengine?

Je, Mwili wa Kristo umejengwa kwa misingi ipi? Ni Nani aliye sahihi Kati yenu? Je mmeshindwa kabisa kupendana! Hakuna wanafiki Kama Hawa watu, ukitaka kujua hawapendani binti yake achumbiwe na dini nyingine! Utaona moto wake ilhali wote ni wakristo!

Mbona ndugu zetu waislamu pamoja na madhehebu yao wana umoja na upendo? Biblia inasema mpende jirani yako kama unavyojipenda je SDA anampenda RC Kama anavyojipenda? Je, RC anampenda mwamposa Kama anavyojipenda? Je, walokole wanawapenda wasabato Kama wanavyojipenda?

Tupendane ndugu zangu hii ni amri kubwa kuliko zote.
 
Usituvuruge Wewe, Kama Huna Upendo Ni Wewe Mwenyewe
 
Kubaguana kupo sana tu, mpaka masuala ya ndoa wanabaguana, mpentekoste hawezi kumuoa mkatoliki au mlutheri. Ilifika hadi wapentekoste kwa wapentekoste kutokuoana, yaani mshirika wa TAG kutoruhusiwa kuoa au kuolewa na mtu wa EAGT, FPCT na KLPT.

Japo wana umoja wao wa wapentekoste lakini kuna ushirikiano wa ibada haupo. Kuna wasabato na wakatoliki hawa huwaona wenzao kama wamepotea na wao wako sahihi.
 
Kubaguana kupo sana tu, mpaka masuala ya ndoa wanabaguana, mpentekoste hawezi kumuoa mkatoliki au mlutheri. Ilifika hadi wapentekoste kwa wapentekoste kutokuoana, yaani mshirika wa TAG kutoruhusiwa kuoa au kuolewa na mtu wa EAGT, FPCT na KLPT. Japo wana umoja wao wa wapentekoste lakini kuna ushirikiano wa ibada haupo. Kuna wasabato na wakatoliki hawa huwaona wenzao kama wamepotea na wao wako sahihi.
Nakwambia hatari kwelikweli! Kila mtu anajiona mwenye haki
 
Kwani Sunni, Shi'a, Ahmadiyya, Ibadi na Sufism wao wanapendana?

Waliofikiria dini waliwaza conflicts tu hakuna kingine, iwe Christianity or Islamic.
 
Kwani Sunni, Shi'a, Ahmadiyya, Ibadi na Sufism wao wanapendana?

Waliofikiria dini waliwaza conflicts tu hakuna kingine, iwe Christianity or Islamic.
Ngoja waje wanaojua vizuri watuelezee upande wa waislamu hali iko vipi, huku kwetu naona ni changamoto!
 
Kwani Sunni, Shi'a, Ahmadiyya, Ibadi na Sufism wao wanapendana?

Waliofikiria dini waliwaza conflicts tu hakuna kingine, iwe Christianity or Islamic.
Kweny uislamu hakuna madhehebu izo ni taasisi na asili ya watu fulani dini iliyotajwa ni uislamu wanatumia Qur an na Sunnah kama wako kinyume sio waislamu..Huku hakuna madhehebu narudia kama hayo majina ni taasisi tu!!

Waislamu wanamfuata Mungu mmoja na mtume Muhamad kupitia Qur an na Sunnah kinyume cha hapo sio uislamu na usiseme ni dhehebu la uislamu hakuna kitu kama icho.
 
Unakosea unaposema sabato vs Katoliki Unakosea sana Katoliki halijawahi kuweka hata kamhadhara kadogo kuongelea dhehebu lolote hata dini yoyote wao wauseme ukatoliki mpaka mashavu yavimbe koo zipasuke Katoliki haijawahi kuwakumbatia waumini eti wasiondoke kwenda dini zingine au madhehebu ya kikristo wataondoka ila Katoliki itawaongoza daima
 
Mshia anaweza kumuoa Msuni (ende vaisi vesa)?
Yeah! Anaoa kabisa, waislamu wanachozingatia ni ushuhudie mungu ni mmoja (Allah) na Muhammad (s.a.w) alikuwa ni nabii wake! Na waislamu wote wana base kwenye hiyo kauli mbili,awe shia,sunni au dhehebu gani.
 
Back
Top Bottom