Je, wapinzani ni wakombozi?

Hii thread imekusanya mambo mengi kama wachangiaji wengine walivyosema na mimi ina hamu kubwa ya kujua hayo uliyoandika kwa kuthibitisha kwa ushahidi.

Lakini nikichangia kichwa cha habari tu nasena kwa uoza uliopo sasa hivi Wapinzani wayaweza kabisa angalau kututoa hapa tulipo na kuwashtaki mafisadi.
 
Setting the record straight,

Kuhusu rais Professor, Plato hakutoa maoni bali aliandika maoni ya Socrates kuwa wanafalsafa (ambao unaweza kusema arguably kuwa ni ma professors, since they are doctors of philosophy, otherwise unaweza ku argue kuwa PhDs are not necessarily "wanafalsafa" unless wame specialize katika Philosophy) hawawezi kuongoza na viongozi hawawezi kuwa wanafalsafa. A more meaningful translation ni ku substitute "wajuzi" for "wanafalsafa".

Kuhusu ma Professor kuwa ma-rais sina hakika kuhusu sasa lakini najua Professor Thomas Woodrow Wilson aliyefundisha na kuwa rais wa Princeton alienda kuwa rais wa 28 wa Marekani na ame influence foreign policy ya Marekani na historia ya dunia sana kwa "Fourteen Points" na proposition yake ya "League of Nations" a precursor to the UN.

Kwa hiyo hii Pol Pot like notion ya blanket anti-intellectualists haina nguvu, tuulize sababu kwa nini intellectuals wetu wanakuwa so mechanical.
 
Point noted... nadhani kuna watu kuchanganya elimu na mtu kuweza kuongoza. Siyo kila mwenye shahada ya Udaktari atakuwa kiongozi mzuri kwa sababu tu ya shahada yake. Hivi Rais Lula wa Brazili ana shahada ngapi za Udaktari na amesoma vyuo gani vikuu hadi akaupata urais wa moja ya nchi zinazoendelea kwa haraka?
 

Remember John Major...?
 
Naamini kabisa wapinzani wana uwezo mkubwa tu wa kutawala na kuongoza kwa ufanisi mkubwa iwapo watanzania watawapa ridhaa ya kuiongoza nchi.
 
Naamini kabisa wapinzani wana uwezo mkubwa tu wa kutawala na kuongoza kwa ufanisi mkubwa iwapo watanzania watawapa ridhaa ya kuiongoza nchi.

I agree with you Mazee!

Nchi haiwezi kuendelea kuuzwa day in day night na kisha watu wakaleta the same old song kuwa ccm ndiye baba na mama wa taifa letu!

Down with mafisadi wa CCM!
 
Si wapinzani wala CCM watakaoweza kuiendesha nchi vyema, ni mwamko wa wananchi wenyewe.

Viongozi wa kisiasa wa upinzani wakipewa nchi 2010 wanaweza kuanza na euphoria ya change, lakini wakajikuta na challenge nyingi sana hata kama waki u combat ufisadi, which itself is questionable, but due to the gross CCM record lets say they will be able to do better than CCM on that end, then what?

Kazi ya kuiendeleza nchi masikini kama Tanzania si lelemama andd before you know it people may deem the task insurmountable and become fatigued, and slip back into ufisadi.It happenned with Nyerere, Mwinyi hardly made an attempt, it happenned with Mkapa and now we are witnessing a Kikwete fiasco.

What we should focus on is institutions that will ensure checks and balances, good governance, civic education, freedom of the press and economic development for all.Once we have these institutions, the people will not wait for the rulers to hand good governance to them, the people will demand good government even before the rulers are sworn in.

If we focus on which party may do a better job but leave the presidency too powerful, the constitution parctically a one party charade and an uneducated mass, even a Gandhi will be tempted to take us for a ride.

Unless everybody in the opposition is a sage of the level of walii and nabii, they can only do so much without the stick to enforce some legal code.It has been said that the carrot of moral high ground and some Mohammed Ibrahim Award is too low compared to the temptations a ruling party "access granted" status can give.
 

Focus ya kwanza ni kukitoa madarakani chama kilichoshindwa kuongoza!
 
Focus ya kwanza ni kukitoa madarakani chama kilichoshindwa kuongoza!



Wazambia walisema hivyo hivyo, na kumuweka Chiluba.Akaenda kuwa rais muuza madawa ya kulevya Afrika ambaye hakuna aliyemfikia, akaitia aibu Zambia.

Wakenya walisema hivyo hivyo, na kumuweka Kibaki. Aka renege ahadi alizotoa kuhusu reforms na mpaka sasa anaendeleza wizi na kina Moi pamoja na largesse ya serikali at the expense of Kenyans.

Tumeona matokeo.

Sheria zile zile za treason mkoloni alizotumia kuwashtaki kina Nyerere ndiyo hizo hizo kina Nyerere walizitumia kuwakandamiza wapinzani.

Ndiyo maana nasema inabidi tu focus kwenye institutions.
 

wazimbabwe na wanorth korea wamemwacha mugabe na kim madarakani na tumeona matokeo yake.
 
wazimbabwe na wanorth korea wamemwacha mugabe na kim madarakani na tumeona matokeo yake.

True dat!

CCM needs to go...wanayoyafanya ni mabaya mno kiasi kwamba tukiwachagua tena tutakuwa wanafiki. Mpaka sasa imeshadhihirika kuwa hawako interested na kubadilika au kubadilisha chochote including hizo "institutions"....So why keep them? Makes no sense.
 
wazimbabwe na wanorth korea wamemwacha mugabe na kim madarakani na tumeona matokeo yake.

Tatizo ni kwamba una interpret ninachokisema in a rather simplistic way, kwamba nina advocate kuacha regimes madarakani.Hasha.

Ninachosema ni kuwa hata kama tukibadili chama tawala leo lakini kama hatuna deeper institutional changes basi tutajikuta tunarudi square one kirahisi tu.Tena mtu mwingine anaweza kuleta argument kuwa hivyo vyama vya upinzani kwa sababu havijaweza kujijenga sana vikawa rather easily manipulated na watu influential ndani ya vyama.


Vyama vijengwe zaidi, networks ziimarishwe, institutions ziwezeshwe, wananchi waongeze uelewa na ushiriki, CCM iondolewe.Hapo vyama vitakuwa havina choice bali kuleta maendeleo.Lakini ukitoa mwanya wa longolongo ni human nature kuanza ku backslide na kuja na vi slogan vitakavyokuwa version mpya ya "kasi mpya..." or some bs like that.

They say a man is only as honest as his options, let us not give any options for abuse and have a guaranteed good government instead of playing Russian Roulette with our country.
 

Mkuu ninakuelewa vizuri sana na ninapata shule toka kwenye posting zako. Kinachogomba hapa ni kuongezea alichosema Ngabu hapo juu kuwa, ccm hawako tayari kubadili hizo institutions na wamesema hili on our faces.

Sasa je, tuwaache kwa kuwaangalia waliiofeli au tufanye our own way. Mimi ninapinga kumaintain status quo.



Nani atajenga hivyo vyama mkuu Pundit? CCM wanamiliki kila kitu hapo Tanzania na najua unaelewa hili. Wanapata mabilioni ya pesa za wizi toka bank kuu na institutions zingine. Hiyo ya kujenga vyama wakati sisiemu wanauza na kufilisi nchi ni excuse ambayo wengine tumeikataa!
 
Mkuu ninakuelewa vizuri sana na ninapata shule toka kwenye posting zako. Kinachogomba hapa ni kuongezea alichosema Ngabu hapo juu kuwa, ccm hawako tayari kubadili hizo institutions na wamesema hili on our faces.

CCM leadership hawawezi kuwa tayari kubadili hizo institutions, inabidi tuwalazimishe by hooks and crooks.Kama ni maandamano, pressure groups, makala za magazeti, exposees,JamboForum mradi tuweze kuwabana.Sasa hivi naona kuna focus kubwa kwenye kuitoa CCM bila kuhakikisha tunabadilisha katiba. Vipi kama tunaitoa CCM halafu Mbowe anatumia katiba hiyo hiyo ya kifisadi kuwabana wapinzani wake wote kama nyerere alivyotumia Sheria za kikoloni zilizombana yeye kuwabana wapinzani wake?

Sasa je, tuwaache kwa kuwaangalia waliiofeli au tufanye our own way. Mimi ninapinga kumaintain status quo.

Mimi pia sipo katika ku maintain status quo.In fact mimi najiona niko radical zaidi katika ku demand changes kwa sababu naona kubadili vyama bila kubadili katiba kama cosmetic change. Ili tuwe na meaningful change inabidi tubadili vyama na institutions pia, tuondokane na rubber stamp parliament, tuondokane na utamaduni wa rais kuwa na nguvu sana kiasi cha ku develop largesse ya kiungu mtu et cetera et cetera.





Tayari hii knowledge ya hapa inatia watu mshawasha wa kutaka kujua zaidi.Tayari tumeshakuwa na mapendekezo hapa, ingawa butu, ya kuanzisha kijarida kipelekwe kwa watu wasio na access ya internet periodically.Personally I am an independent who would like to participate in the political process without party affiliation, therefore I see my part in building political/civic awareness period.Wanavyama wanaweza kuchangia kujenga vyama vyao, lakini wakumbuke kama hawajengi hizi institutions itakuwa mechi tu ya kusema "tuwaondoe CCM tupate kula na sisi zamu yetu". I am not interested in that.

Inabidi wanavyama waanze kuwapatia zali watu wa CCM wanaotumia mali za umma isivyo halali, kuanzia mambo ya BOT na EPA mpaka vitu kama viwanja vya michezo vilivyojengwa kwa pesa ya wote enzi ya one party na mpaka leo ni mali ya CCM (e.g Kirumba Mwanza)

Inabidi tuwe honest with ourselves na tusitafute majibu rahisi kwa maswali magumu.Matatizo yetu ni deeper than regime change, we need institutional change and to me institutional change needs to happen either simultaneously with regime change or before regime change.Otherwise mtu akishashika power kwa mara ya kwanza pale inakuwa vigumu sana kumshawishi afanye mabadiliko.
 
Mambo ya kulazimisha watu wasiotaka mabadiliko yamepitwa na wakati. Walikuwa na muda mwingi sana wa kubadilika lakini hawakutaka. Sasa hapo mimi sioni alternative nyingine zaidi ya kuwaondoa hao watu na kuweka wengine. Hao wengine watakaowekwa na wenyewe wakileta za kuleta tunawaondoa. Nchi ni ya kwetu sisi wananchi and we get to decide who leads us. Hakuna waliozaliwa kututawala. Nawaambia sisi wananchi tukiwa wakali hata viongozi wetu nao watakuwa makini maana watajua hatuna mchezo wala uvumilivu wa mambo ya kijinga. Kama mtu huwezi kazi tuliyokupa basi katafute nyingine unayoiweza. Hili linawezekana kabisa.
 

Ngabu,

Hili ndilo swali nimekuwa najiuliza kila mara nikisoma report ndefu ya kwa nini ni makosa kuwatoa sisiemu kabla hatujenga hizo institutions.

Nani atajenga kama hawa sisiemu wameshikilia dola na wanatuonesha vidole kila wakati tukiwauliza kufanya mabadiliko?
 

Inaonekana wewe mkuu ukiwa na panya amefia ndani ya nyumba wakati ukisubiria fundi aje kuifanyia repair, utamwacha huyo panya ndani ya nyumba kwa sababu kuwa nyumba yako itachafuka wakati wa repair so ni bora usubirie hadi repair imalizike ndipo usafishe vyote (uchafu na panya mfu)!
 


Nyani,

Ukisoma utaona sija entertain kabisa swala la kuibadili CCM ili iwe safi iendelee kutawala.Ninachosema ni kuwa instituonal change is imminent, regardless of who is in power, kwa hiyo tukibadili katiba sasa hivi siyo tunabadili katiba ili tui reform CCM, tutabadili katiba ili mtu yeyote atakayekuja kuwa in power abanwe na katiba explicitly.Kwamba mambo ya kupiga midili mikubwa mikubwa bila kushirikisha wawakilishi wa wananchi yakome, mambo ya kupeleka majeshi Comoro bila ridhaa ya wabunge yakome.This way hata jinsi ya kuwang'oa CCM itakuwa rahisi kwa sababu CCM washazoea za kunyonga (kuiba hela za uchaguzi BOT ETC) ikija system fair and square itakayokata mirija yao watatapatapa.

Lakini sisi tunaongelea kuing'oa CCM kabla ya kuikatia mirija yake inayoipa kiburi, hatuwezi kufanikiwa.

Ndiyo maana nasema institutional change inabidi ziende simultaneously na regime change au zitokee kabla ya regime change, kwa sababu regime yenyewe inaelea over the foundation of these lax institutions, usipoondoa foundation hiyo hata hiyo regime change itakuwa ndoto.

Si zitapigwa simu tu tume ya uchaguzi kama alivyopiga Nyerere na matokeo yatageuzwa hata kama upinzani umeshinda?

Lakini ukiwa na sheria zinazozuia rais kuteua Tume ya Uchaguzi, ukiwa na ma judge wenye integrity ambao hawatamuogopa rais, then thats a big step towards regime change.
 

Ndibalema:

Hata kama upinzani hauwezi kuleta maendeleo, si vizuri kuweka mayai yote kwenye kwenye kapu moja.
 
Nadhani swali la msingi ambalo bila ya shaka linakuwa wazi katika hoja ya Pundit ni kuwa tuiindoe CCM ili kiwe nini? au tuiondoe CCM alimradi imeondoka halafu tufikirie tufanye nini wakishaondoka?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…