Je, Watanzania mlio nje ni vibarua na wabeba maboksi?

Watanzania wengi,walio nje na walio ndani ni wavivu wa kufikiria kuhusu kesho.Hizo takwimu ni sahihi kabisa.Nashangaa mtua anaposema eti watanzania wanatuma pesa kwa njia ya mabulungutu,hivi kwani wakenya na waganda hawatumii hio njia?Au sisi ndio wajanja pekee tunaojua kutumia njia hizo za mabulunguti?Ok,hata kama ni mabulunguti mbona hatuoni kazi zake katika miji yetu?Binafsi natoka Mwanza lakini bado sijaona private estate hata moja ambayo unaweza kusema mwenye nayo anapiga kazi nje.watanzania hatutumii hela ipasavyo,tukubali udhaifu ili tuweze kupambana na hivyo virusi vya uzembe.
 




wabongo sijui tuna laana gani..tunaubinafsi uliopindukia..ona hata viongozi wetu wajiangalia wao tu na familia zao...!
 




mkuu inasemekana ninyi wabongo ambao tayari mmebahatika kwenda majuu mnabania sana wenzenu, tofauti na wakenya na waganda wanao peana sana mashavu...kama ni kweli bana acheni ubinafsi kama viongozi wa ccm
 
Kima cha chini kwa kibarua, "mbeba maboksi" kwa nchi nyingi za ulaya ni euro 800 kwa mwezi, japo maisha pia yako juu, lakini huwezi kudharau kipato hicho. Kwa tz ni hiyo ni zaidi ya tsh 1,700,000/=, ni mshahara wa juu kabisa.
Kwa marekani na kwingineko sifahamu.
Jambo lingine utatumaje hela kwa njia zinazoeleweka tz wakati kila siku ni kilio cha umeme, Western Union money transfer ni njia rahisi, ingawa ina makato makubwa, lakini haipo sehemu nyingi tz, hata baadhi ya sehemu zilizokuwepo zimefungwa kwa sababu ya tatizo la umeme, ukienda unaambia simu haifanyi kazi, utawezaje kupata data za internet bila umeme. Njia iliyobaki na inaaminika hadi sasa ni kutumia watu wanaofika tz, walau viwanja vya ndege vinafanya kazi kwa hiyo hela inafika salama bila ya kupitia kwa Beno Ndulu: nyumba zinajengwa, watoto wanasoma na maisha ya ndugu na marafiki yanasonga mbele.
 

Numbers don't lie!
Kuna wakenya zaidi ya 500,000 in the US
Kuna watanzania less than 25,000 in the US
Sasa do the math hapo
 
kaka unategemea nini kama hapo B.O.T kwenyewe wamejaa vihiyo kibao watatoaje hizo takwimu kuna mtindo mbaya sana unaendelea hapa Bongo kuna wasomali na Wadosi pale Karikakoo na Samora wanafanya biashara ya billions bila serikali kujua wala hawapati hata hizo kodi zinazotokana na kusafirishwa kwa hela hizo, mimi ka 2 weeks ago nilitakiwa kupokea kama Pound 5000 kutoka UK nilitumiwa number ya simu tu nikaenda pale karikakoo kuna msomali ana VAULT kama nyumba akaniuliza nahitaji currency gani $, pounds au Tzsh nikachoka mwenyewe. hii nchi inaliwa tu jamani.
 
Ndhani tatizo liliopo hapa nililile la tatizo sugu la Tanzania, system yetu haioni umuhimu wa kufuatilia na kutunza Takwimu wapo Bizy kuiba zaidi.

Ninachojuwa wakenya wanajitahidi sana kufuatilia takwimu na wanajuwa umuhimu wake, ndicho kinacho wasaidia sana serikali yao hata kufanya waaminike sana katika vyombo vya kimataifa, sisi hapa hata takwimu ya GDP yetu haipo ndani ya nchni kila mtu ana yake.

Kitu muhimu hapa katika hoja yako si kubeza kazi maana tabia ya kubeza kazi na kuchaguwa kazi ni chanzo kikubwa sana kilichoturudisha nyuma sisi kama nchni na Taifa, maana ilipo anza mtindo wa kumuona mkulima kama hana maana na neno Mkulima likafanywa tusi hapo ndipo Wakulima wetu wote walipoamua kukimbilia mijini, mijini pia walipofika wakakuta hakuna ajira wakaamua kufanya biashara ndogo ndogo lakini bado sisi kama kawa tukaendelea kuwa dharau, kuwabeza na hapo ndipo kamata kamata ya wamachinga ilipoanza hapa Dar, hapo ndipo Umaskini wetu ulipojikita.

Nadhani ni changamoto kwa serikali kuwa na mtindo wa kufuatilia na kutunza takwimu, naweza kukupa mfano wa Mke wangu yupo nje ya nchni kwa zaidi ya miaka mitatu sasa lakini sidhani kama kuna mtu anajuwa hili zaidi ya familia hata balozi zetu hazina na wala hazi-encorage kujuwa watu wanaoingia katika nchni za nje kutoka Tanzania
 
Cha msingi ndugu zangu mi naomba tusaidiane tu, regardless ya changamoto zilizopo kwenye hizo nchi za dunia ya kwanza( western countries) lakini bado kuna fursa ya kufanya kazi haijalishi ni casual au formal. Kuna Dr. Mmoja wa kike amenifundisha udsm alikuwa anasoma marekani, mwenyewe alisema alikuwa anafanya vibarua kwa masaa hata kufagia barabara, baada ya masomo yake kama miaka mitatu aliporudi bongo kapandisha majumba ya maana akaja na magari pia(NOT A STORY BUT A REALITY) .nawashukuru sana wachangiaji wengi ambao mmetupa uzoefu wenu huko ughaibuni, natambua mchango wako The Kop. Nimeumizwa mno na taarifa kwamba wengi wa wa-TZ wenzetu wanaonda ng'ambo badala ya ku-hustle ili wao ndio watume hela bongo eti wao ndio wanatumiwa.! Na hii inatokana na kwamba wengi wa wanaoenda huko ni watoto wa wenye nazo hasa wanasiasa ambao wengi wao ni legelege na wanajihurumia..tofauti na wenzetu wakenya ambao ni watafutaji matata, halafu wao kamwe hawaachani ingawa ni kwa makabila, hapa Tanzania graduates tunahaha ajira ngumu hadi uwe una mjuwa fulani, wanabana hata ku-volunteer, wanashobokea wakenya ambao sasa hv ni wengi na baadhi yao ndio mameneja waajiri.! Tanzania sasa hivi inaboa, MLIO UGHAIBUNI MTUSAIDIE NA SISI TUTOKE Tz .!
 
 
Mnatulaumu bure. Kwanza hiyo benki kuu iliyoshindwa kudhibiti wizi wa EPA haina takwimu wala mpango wa kuwa nazo. Kimsingi tatizo si watu kutuma au kutotuma bali ombwe la takwimu kwa nchi yetu. Halafu hili si jambo la kutulaumu maana wakati tunakuja huku hakuna aliyetutuma tukamtafutie. Si hilo tu, kupata pasi Tanzania ni mbinde kuliko nchi nyingine. Pia ni ukweli kuwa watanzania waishio nje ni wachache ukiinganisha na wenzetu ambao wengi wao walikimbia nchi zao kutokana na siasa mbaya huko nyuma mfano Uganda walimkimbia Idd Amin, Kenya wengi walimkimbia Moi mwaka 1982 wakati wa jaribio lililoshindwa. Nchi kama Ethiopia na Nigeria zinawapa moyo watu wake kwenda nje na kutafuta riziki na nafasi kwa watu wao wakati Tanzania unaulizwa upuuzi. Nitatoa mfano mke na watoto wangu walipokuwa wakijiandaa kuja huku walitakiwa kila aina ya upuuzi mara kibali cha mjumbe mara criminal check record mradi upuuzi mtupu. Pia si wote wanaotoka familia chovu. Na kutuma pesa siyo suala la kuzua ugomvi. Kwanini watu wategemee pesa ya watu wa nje wakati hiyo ya ndani wanawaachia wahindi wanaitorosha? Serikali ya Tanzania haipaswa kusema kwa vile ndiye mwizi mkuu. Nchini Kenya wana utaratibu wa kibenki wa kupokea pesa toka nje. Tanzania ni upuuzi mtupu na roho mbaya za watendaji wetu.
Pia si kweli kuwa wengi tulioko huku ni wabeba maboksi au vibarua. Hata wanaofanya vibarua wana maisha mazuri kuliko wafanyakazi wa serikali wa Tanzania otherwise waibe na kufanya ufisadi ndipo wanaweza kuwazidi. Investment nyingine huku ni kwa ajili ya elimu bora kwa watoto wetu nasi wenyewe kwa wale wenye kupenda kujiendeleza.
Nadhani hayo kwa kiasi fulani yametosha. Muhimu si kutegemea kupokea wakati tunaendelea kuwavumilia watawala vibaka waliopo sasa.
 
Kama vp nenda ww huko nje alafu tuma hzo pesa 2faidke watanzania wenzako!
 
Watanzania kwa kuomba jamani heee! haya usipotuma ndio hivyo unabeba box, Ukituma mjinga wewe ATM.. Basi ili mradi haijulikani ufanye nini.. Hakika Kwa mtanzania kila siku ni drama tu, na ajabu anayewahoji watu wa Ulaya yeye mwenyewe kibarua kesho kinaweza kuota...
 
Fareed, Kwanini watanzania watume hela bongo wakati Tanzania imejaa:

- Dhahabu, kwa takwimu za kimataifa ni nchi ya Tatu kwa uzalishaji ulimwenguni na ktk soko sasa hivi, ni ounce ni karibu USD 1,700.00
- Almasi
- Tanzanite
- Uranium
- Makaa ya mawe
- And so much more natural resources
- Samaki
- Mbuga za wanyama

Tanznians don't need handouts from anyone. Hata serikali yetu haihitaji msaada wowote kama uzalishaji wa madini na rasilimali ungesimamiwa vizuri. Hatujachelewa!
 

Piga box mkuu. Jali maisha yako na familia yako and move on
 
hii ni moja ya sababu watu hawatumi hela watu nyumbani wamekalia kukinga midomo tu
kama wewe unaona ni wapiga box na kenya wanafanya kazi safi kulingana na utafiti wako mwemba
kaa hapo piga majungu lakini hii ni issue complicated kuliko unavyoweza kutafakali
wakenya waliopo nje ni wangapi na watanzania ni wangapi?
wakenya walianza kusafiri miaka gani na watanzania je?
ndio maana makampuni ya kizungu yakija bongo wanataki kuona sura ya kikaragosi yeyote kwenye kampuni zao
maana tuko low sana katika kufikiria na kupambanua

leo hii mtanzania analipwa vijisent na serikali lakini bado anataka kujifananisha na mtu anayelisha zaidi ya Tsh 15,000 kwa saa huyo mtu akipiga masaa kumi tu ni minimum salary ya kibongo. sasa lipi bora maisha safi au kujibana na tai?
na watu watatengana sana kwa ujinga huu na matusi haya yasiyo na tija kwa ustawi wa taifa leo, wakenya hao unaosema hawana kauli za kijinga kama hizi kwa watu wao
 

Mosi serikali ya Tanzania haina mtazamo wa kiuchumi kwa wanaoishi nje na badala yake wanaita wanataka kule huku na huku ndivyo Rais Kikwete alivyowaambia watanzania waishio Marekani - Jimbo la Kalifonia.

Watanzania wengi walikuwa wanatuma pesa nyingi sana hawa wa kutoka Marekani kupitia mtandao wa kisomali ambapo watu walikuwa wanachukua dolla kavu kavu, mara serikali ikatia marufuku, na sasa watu wanatumi kutumia njia za panya. Huo mtandao wa wasomali ndio unaowanufaisha wakenya na waganda na ni rahisi kufuatilia kama pesa kiasi gani zinaingia. Huo ni mfano tu.

Watanzania siasa ndio tunajua lakini mambo ya uchumi tunayafanya siasa hapo ndo kuchanganya silabasi.
 
Mada imenigusa sana. Ni kweli waishio ughaibuni ni wazalendo sana na wanajitahidi, hii negative attitude dhidi yao sijui nani kaianzisha. Mnafikiri huku kuna loop holes za ufisadi kama bongo?
 

Nikupe pole sana, na labda ungejaribu kutoa kauli hiyo baada ya kufanya utafiti. Wengi unaofikiri unawafahamu ni wale wenzangu mimi, lakini tabala la wale wenye profession zao wengi wao wametulia na mambo yao, maana haya mambo ya kuumiza vichwa kila kukicha pale bongo yanachefua. Maisha ni po pote katika ulimwengu huu wa sasa, na kama mtu umetulia na mambo yanajipa bora kuendelea kushi na kazi ambayo inakupa lishe na maslani ya uhakika bila woga.

Zamani hata mimi nilikuwa nafikiri kama unavyosema kabla sijafanya utafiti, lakini kwa leo ni tofauti maana nazijua mbivu na mbichi. Wenzako wanaendelea na box lao hilo na wakishafikisha umri wa miaka 60 ya kustaafu wana hakika ya flow ya pensheni kila mwezi kwa kiwango cha mshahara wa watu wa kati huko nyumbani pamoja na uhakika wa matibabu. Leo sio ulimwengu wa kudanganyana, mwenye nafasi mwache aitumie anavyoona inamfaa. Alamsiki.
 

How many Kenyans would you say live in the US, both legally and illegally? And how many would you say live in South Africa, once again, both legally and illegally?
[h=2]Relevant LinkS[/h]
Depending on which website you believe, there are anything from 100,000 to 500,000 Kenyans in the US. And between 5,000 and 100,000 Kenyans in South Africa.

Allafrica.com

Main article: African Immigration to the United States
Nigerian Americans are citizens of the United States of America who are or descend from immigrants from Nigeria. Since the late 1960s and early 1970s, approximately one million Nigerians have immigrated in to the United States.
Similar to their proportion of population on the continent of Africa, Nigerians are the single largest contemporary African immigrant group in the United States. Nigeria's official current indigenous population is 140 million. It is estimated that 20 million people of Nigerian descent reside outside Nigeria, with the majority living in the United Kingdom (see Nigerian British) and the United States.[SUP][citation needed]
Source:Weekipedia

It is estimated over 2.5 million Kenyans live abroad, and last year alone they sent $609 million (Sh45.7 billion) in remittances ranking them as the fourth biggest source of foreign exchange and contributor to growth of the national economy after horticulture, tea and tourism. This might explain why on the eve of every General Election, all presidential candidates trawl communities abroad for financial and moral support. But what do they get in return? The community abroad remains disenfranchised[/SUP]

Allafrica.com

Some 45,000 Tanzanian-born people are currently living abroad, the overwhealming majority of these reside in the United Kingdom (over 32,000), whilst thousands also live in Canada, the United States and various European nations

Weekipedia
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…