Je, watu wa mikoani na vijijini wakianza vitimbwi wanavyofanyiwa wakienda kwa ndugu zao wa Dar patatosha?

Je, watu wa mikoani na vijijini wakianza vitimbwi wanavyofanyiwa wakienda kwa ndugu zao wa Dar patatosha?

Ulivyosema tu mkewe ni mpare nimekubali hii story ni ya kweli kabisa.
Mi maangu Mdogo aliolewa na mpare mbona cha moto alikipata, full ubahili, unyanyasaji, uchoyo, ushirikina na kujaza ndugu zake ndani.....hadi watu walikuwa wanamwambia we umebugi sana wapare ni nyoko wanajioaga na kuoana wenyewe maana matabia yao ya kingese yanajulikana na kila mtu hapa mjini
 
Wapare. Hawa watu waone hivi hivi. Kuna dogo mmoja na babu yake walienda kwa babake mdogo aliyeoa mama mpare. Kumbe mmama ule ugeni akawa hakuupenda. Basi akafanya jitihada chakula kisiliwe mchana mpaka arudi kazini. Dogo akakomplein kwa baba mdogo na kuambiwa shida iko wapi? Wewe ukisikia njaa ingia jikoni pika ule na babu yako ambaye Ni baba mzazi wa dime la nyumba hapa Ni kwenu. Habari hii ikamfikia mama wa kipare aliyekua anafanya kazi tanesko.
Hapa Dar watumishi wa tanesko hawalipi umeme hivyo wengi wanapikia umeme tafauti na sisi wengine.
Babu nae licha ya kupenda mapochopocho yaliyokua yanapikwa na dogo pia alikua mpenzi sana wa tiivii hasa ITV.
MAMA WA KIPARE KAONA KUWAKATA STIMU HAWA WAGENI NI KUONDOKA NA ILE CUT OUT. Cutout Ni ka kifaa Fulani ukikaondoa pale karibu na mita umeme hauingii ndani. Basi mpare asubuhi akienda kazini anachomoa cutout inamaana nyumbani hakupikwi Wala hakuna feni na tiivii mpaka jioni akirudi. Baba mwenye nyumba alipohoji alijibiwa live bila chenga kwamba weka mita yako Kama unataka ndugu zako wataidi umeme.
Siku tatu nyingi, mzee na dogo waliomba nauli ya kurudi Kanda maalum.
 
Walimfanyia ukatili [emoji23]

Ferry- dege kuna kipande kirefu tu
kilomita kama 30 hivi na zaidi alafu ukifikia mitaa ya mji mwema kwenda mbele kule kumetulia sana kama unaenda maporini mchana tu mtihani je usiku inakuwaje jamaa walimtesa sana
 
kilomita kama 30 hivi na zaidi alafu ukifikia mitaa ya mji mwema kwenda mbele kule kumetulia sana kama unaenda maporini mchana tu mtihani je usiku inakuwaje jamaa walimtesa sana
Panatisha sana, ana bahati boda alikubali kumpeleka kule night.
 
Ishu ya daslm ni muendelezo wa familia nyingi kukosa ule Utu na upendo wa dhati na hii yote inatokana na jinsi mlivyolelewa sio kweli watu wengi wa daslm wapo hivyo mimi nina jamaa zangu familia zao ni wakalimu balaa mpaka ukiwa daslm inabidi uwakwepe tuu mtu ukimwambia upo daslm kama huna gari anakuuliza akupe gari ufanyie shughuli zako ukimaliza umpe mimi siwezi kuwafata wengi ni wakalimu mno..ndugu yangu wa familia moja ukienda kwake ni story balaa kwa sababu watoto wao wakifunga shule buwa wanakuja home nami wakifunga shule nawapeleka kwao kwa siku kadhaa maisha yanaendelea msitegemee mapenzi ya ndugu yasipokuwepo mlipokua nyumbani hata akiwa Mtwara atakua na tabia za kienyeji tuu...
 
Watu wa mjini hawana muda, elewa hilo......na kila kitu ni pesa, hivyo wanaishi kwa bajeti, sasa wewe ukitoka kijijini kwenu na yeboyebo ukifikiri kuna mtu wa mjini ataku entertain itakula kwako, ndo maana mnaishia kukodolea TV masaa 24.......
Nanyi mkija kijijini msitusumbue, maana nasi tunakuwa bize kwenda Mashambani.
 
Nanyi mkija kijijini msitusumbue, maana nasi tunakuwa bize kwenda Mashambani.
Tatizo watu wa vijijini mnakuwa na shobo kibao, kuwapigia simu kila mara watu wa mjini wakawatembelee ili na nyie muuze sura kwamba mna ndugu yenu anayekaa town, vinginevyo hakuna mtu yoyote wa town mwenye shobo na village.
 
Kila ndugu akae kwake
Sana.. Mimi hili nilishaweka msimamo kabisa!

Ndugu ntamsaidia akiwa kwake,

Siyo anakuja kwangu alafu tukikwaruzana na wife anapiga simu home hoo kaka/mjomba huku kila siku wanagombana na mkewe...

Na walivyo wajinga watasema inaonekana mwanamke kamtawala mmewe! [emoji23][emoji23][emoji23]
 
ila watu wa mijini na kwenye majiji kuna haja ya kujitafakari.

Mwana DSM ukienda mikoani huko au vijijini ukifika ni kawaida sana kukuta ndugu zako walikuwa wanakusubiri stendi zaidi ya saa ufike, umefika utachinjiwa kuku siku ya kwanza, utaishi hata mwezi na hakuna mtu atakupa maswali ya unaondoka lini, misosi utakula utasaza, ukiondoka utapewa hata debe la unga au maharage na hapo ukunbuke wewe ulipeleka tu mkate, unavyoondoka unasindikizwa kabisa wengine wanakubebea begi, kiufupi watu wa huko wengi ni wakarimu.

Ishu inakuja kwa watu wa Dar sasa, yani hata ndugu kaja kumpokea tu ni mtihani, mwenyeji anatoa maelekezo mgeni ampe simu bodaboda na malipo atalipa mgeni ambae hata hio hela haikuwa kwenye bajeti, akifika msosi ulioandaliwa ni ugali tembele yani ugeni wake ni kama hauthaminiki kama sio kumkomoa, baada ya salamu mwenyeji atakua bize na simu au mke wake kitu kinachoanza kukaribisha upweke kwa mgeni, mgeni akikaa siku 2 tu anaanza kuulizwa anaondoka lini, siku ya kuondoka pekee labda ndio mgeni husindikizwa maana ndio anasepa ni kama mzigo umetoka.

Sasa nauliza hivi watu wa huko mikoani nao wakiamua kwenda kwa style hizo kama zenu, je patatosha?
Kuna sehemu nimepita nimekutana na ujumbe huu
 
Tatizo watu wa vijijini mnakuwa na shobo kibao, kuwapigia simu kila mara watu wa mjini wakawatembelee ili na nyie muuze sura kwamba mna ndugu yenu anayekaa town, vinginevyo hakuna mtu yoyote wa town mwenye shobo na village.
Hizo dharau sasa, Kwani mjini huko kuna kipi Cha maana na Cha pekee??.
 
Ishu ya daslm ni muendelezo wa familia nyingi kukosa ule Utu na upendo wa dhati na hii yote inatokana na jinsi mlivyolelewa sio kweli watu wengi wa daslm wapo hivyo mimi nina jamaa zangu familia zao ni wakalimu balaa mpaka ukiwa daslm inabidi uwakwepe tuu mtu ukimwambia upo daslm kama huna gari anakuuliza akupe gari ufanyie shughuli zako ukimaliza umpe mimi siwezi kuwafata wengi ni wakalimu mno..ndugu yangu wa familia moja ukienda kwake ni story balaa kwa sababu watoto wao wakifunga shule buwa wanakuja home nami wakifunga shule nawapeleka kwao kwa siku kadhaa maisha yanaendelea msitegemee mapenzi ya ndugu yasipokuwepo mlipokua nyumbani hata akiwa Mtwara atakua na tabia za kienyeji tuu...

Wachache sana wa hivyo na ukiona hivyo wameshika dini
 
Mimi nilifika dar.usiku saa tano kuangaza mwenyeji hayupo ubungo.kupiga sim hapatikani hee.baada ya masaa mawili ndio napigiwa na dada wa kazi umefika wapi dada kalala, chukua bodaboda ikupeleke fery uvuke kuja kigamboni saa saba na nusu hiyo usiku.nafika kigamboni sim haipatikani nikakaa hapo na walinzi baadae anapiga chukua boda tena ikulete dege.hata dege sipajui jamani huyo boda boda alikua ana pepeza pikipiki kila nikitaka kuongea midomo haiwezi sababu ya supidi, Tukawa tunatokomea tu nauliza bado anasema bado saa tisa usiku hiyo, mpaka nafika saa kumi.kufika hamna maji ya kuoga hamna chakula.nikalala nashtuka saa kumi ba mbili dada ananiambia amka tufanye usafi nikasema bado napumzika.Akasema Lazima tutoe magodoro.Nikahamia sebuleni ile usingizi unaanza naambiwa hata hapo nakuja kakae nje.Dah sitasahau nimeacha mkoani mjengo wangu wa maana kitanda nateseka wallah nilitoa chozi.Nilipata homa kali sikununua hata biashara nikarudi nyumbani baada ya siku tatu.mpaka leo nikija Dar nina ndugu lakini nafikia Hotel.Bora lawama kuliko fedheha
Dah,aisee nimecheka Sana!, maisha ya dar ni Kama chuo Cha mafunzo
 
Hata Mimi sipendi wageni.
Wanakuja kuchunguza unaishije na mkeo especially Kama mkeo sio kabila lako wapate la kumsema.
na huyo mkeo akikunyanyasa unakuja kuomba ushauri kwetu wakati tungekupa ushauri mapema kabla viwanja na mali hujaandika jina lake....
RIP Dk. Buberwa wa "Dental Formula Care", "Joy" nk
 
Hizo dharau sasa, Kwani mjini huko kuna kipi Cha maana na Cha pekee??.
Kusingekuwa na cha maana msingekuwa mnasumbua kuja mjini na kuharibia watu mishe zao kwa ajili ya kuwapokea stendi na kuwatembeza mjini...
 
Kusingekuwa na cha maana msingekuwa mnasumbua kuja mjini na kuharibia watu mishe zao kwa ajili ya kuwapokea stendi na kuwatembeza mjini...
Nanyi mnapokuja kwetu Village si huwa tunawahangaikia??
 
na huyo mkeo akikunyanyasa unakuja kuomba ushauri kwetu wakati tungekupa ushauri mapema kabla viwanja na mali hujaandika jina lake....
RIP Dk. Buberwa wa "Dental Formula Care", "Joy" nk
Sasa hutaki niandike viwanja vyangu jina la waif. Unataka niandike la Nani? Kila siku ananipa uroda Tena bila masharti ya vocha, nauli au chips.
 
Alikuaja Dar kwa mdogo wake toka ntoke mzee mmoja wa kipare anaitwa Mshana. Mdogo wa Mshana akachinja kuku Safi kabisa. Kule upareni Kama kuku imechinjwa wakati wa kula mnaanza na ugali tonge mbili tatu ndio yule mkubwa kuliko wote anaokota nyama , usually anaokota paja ,then anafuatia mwingine kwa ukubwa hivyo hivyo mpaka mdogo kabisa anaambulia ATC.
Sasa mzee wa kipare toka bush wakati anaanza kunawishwa yeye akajua taratibu za kipare zitazingatiwa. Ile mzee amekata tonge la kwanza akakuta watoto wa mdogo wake yaani watoto wa mjini Mwananyama ndaani ndani walishachukua nyama zote nzuri na kwenye sahani kimebaki kipande Cha shingo.
Hahahahaha mkuu umenichekesha, eti kipande cha shingo.
 
Back
Top Bottom