Itovanilo
JF-Expert Member
- Jul 30, 2018
- 2,314
- 5,150
Wasalaam wanajamvi, hope mu wazima
Leo nimeona nigusie jambo moja ambalo Kila kiumbe chini ya jua anapendelea kuwa nayo. FURAHA naam FURAHA ile hali unayoipata mara baada ya kufanyiwa au kupewa kitu kizuri
Ni vile unasaini wakati wa kupokea mshahara,au kukubaliwa maombi ya kazi ni wakati ambao mishipa na viungo vingi vya mwili hu relax
Vyote hutengeneza furaha
Ulishawahi kupewa dhamana iwe mahakamani/mahabusu na ikakubalika? Yaani mwenyewe unajiona kabisa hapa siponi,lakini mwenyezi MUNGU anajalia,vipi kuhusu furaha yake. Hata unapotongoza,halafu unaona kabisa mhusika anaelekea huwa unajisikiaje?
Ni machache kati ya mengi ambayo huleta amani ya moyo.lakini lengo la mada Ni kwamba.....@..si tu ufurahi wewe tu,ila unapaswa kuwa chanzo Cha FURAHA kwa wengine
Maamuzi ya kupiga muziki mkubwa hususan maeneo ya uswahilini Ni ushahidi tosha kwa muhusika anapata vibe la kutosha lakini vipi wagonjwa,na wenye shida mbali mbali ambao huenda ikawa Ni kero kwa wakati huo,tujitathmini
Pia Kuna ile hali ya kutoa msaada iwe kwa mtu mmoja mmoja au kundi la watu usipokuwa makini,unaweza kugawa bahasha za hela zenye thamani ya milion Mia tano.na ukasababisha huzuni kubwa kwa watu tofauti na malengo yako
Kwanini?
Ni kwa vile umeshindwa kutumia hekima na busara kwenye uwasilishaji wa msaada wako. Kumfurahisha mtu sio lazima,bali ni uwajibikaji ambao utakuletea Faida na furaha baadae e.g kumridhisha mpenzi wako.huenda ikamfanya asiwaze kuchepuka,basi Ni faida kwako
Kufanya kazi kwa bidii unaweza kuwafurahisha waajiri/mabosi wako,lakini pia waweza kupata faida ikiwemo kupandishwa daraja/cheo au mshahara. Tengeneza furaha Iwe ndoa, familia na hata uhusiano mzuri na wafanyakazi wenzako maofisini/makazini kwenu.
Swali:Je umejitengenezea msimamo upi ili kuwa chanzo cha furaha kwenye jamii inayokuzunguka?
Tiririka kwa Faida ya wengi...
Pia muwe na wakati mwema wanajamvi.
Leo nimeona nigusie jambo moja ambalo Kila kiumbe chini ya jua anapendelea kuwa nayo. FURAHA naam FURAHA ile hali unayoipata mara baada ya kufanyiwa au kupewa kitu kizuri
Ni vile unasaini wakati wa kupokea mshahara,au kukubaliwa maombi ya kazi ni wakati ambao mishipa na viungo vingi vya mwili hu relax
Vyote hutengeneza furaha
Ulishawahi kupewa dhamana iwe mahakamani/mahabusu na ikakubalika? Yaani mwenyewe unajiona kabisa hapa siponi,lakini mwenyezi MUNGU anajalia,vipi kuhusu furaha yake. Hata unapotongoza,halafu unaona kabisa mhusika anaelekea huwa unajisikiaje?
Ni machache kati ya mengi ambayo huleta amani ya moyo.lakini lengo la mada Ni kwamba.....@..si tu ufurahi wewe tu,ila unapaswa kuwa chanzo Cha FURAHA kwa wengine
Maamuzi ya kupiga muziki mkubwa hususan maeneo ya uswahilini Ni ushahidi tosha kwa muhusika anapata vibe la kutosha lakini vipi wagonjwa,na wenye shida mbali mbali ambao huenda ikawa Ni kero kwa wakati huo,tujitathmini
Pia Kuna ile hali ya kutoa msaada iwe kwa mtu mmoja mmoja au kundi la watu usipokuwa makini,unaweza kugawa bahasha za hela zenye thamani ya milion Mia tano.na ukasababisha huzuni kubwa kwa watu tofauti na malengo yako
Kwanini?
Ni kwa vile umeshindwa kutumia hekima na busara kwenye uwasilishaji wa msaada wako. Kumfurahisha mtu sio lazima,bali ni uwajibikaji ambao utakuletea Faida na furaha baadae e.g kumridhisha mpenzi wako.huenda ikamfanya asiwaze kuchepuka,basi Ni faida kwako
Kufanya kazi kwa bidii unaweza kuwafurahisha waajiri/mabosi wako,lakini pia waweza kupata faida ikiwemo kupandishwa daraja/cheo au mshahara. Tengeneza furaha Iwe ndoa, familia na hata uhusiano mzuri na wafanyakazi wenzako maofisini/makazini kwenu.
Swali:Je umejitengenezea msimamo upi ili kuwa chanzo cha furaha kwenye jamii inayokuzunguka?
Tiririka kwa Faida ya wengi...
Pia muwe na wakati mwema wanajamvi.