Je, Yanga ameshuka Kiwango na kutafuta visingizio au ndio Propaganda za soka la Tanzania?

Je, Yanga ameshuka Kiwango na kutafuta visingizio au ndio Propaganda za soka la Tanzania?

Waufukweni

JF-Expert Member
Joined
May 16, 2024
Posts
2,060
Reaction score
5,648
Wataalam wa Sayansi ya mpira tujadiliane kidogo kuhusu hili linaloendelea mitandaoni

Tangu mechi ya kwanza ya Ligi Kuu, Yanga akiwa ugenini dhidi ya Kagera Sugar licha ya kushinda bao 2-0 bado kulizuka mijadala kuhusu kiwango chao, hata mechi zilizofuata (na CEB 1-0, Ken Gold 1-0 zote ugenini).

Mjadala ulikufa baada ya ushindi wa bao 6 kwa mtungi kwenye mechi ya marudio na CBE pale Zanzibar kwani ilionekana kama wamerudi kwenye utaratibu wao wa msimu uliopita 2023/24 wa kutembeza vipigo vikubwa na kutamba kwamba mashabiki wao washangilie angalau kuanzia bao la tatu na kuendelea.

Baada ya ushindi wa bao 1-0 dhidi ya KMC ambao msimu uliopita Wana-Kino boys walipigwa jumla ya bao 8 kwenye mechi mbili, (5-0 na 3-0) hali ilirudi baada ya msemaji wao Ally Kamwe alibuka na tuhuma kwa Azam Tv akidai kuwa Wanapaswa kutafakari kuhusu utoaji wa habari zao, akionyesha tofauti katika mahojiano ya makocha wawili. Katika video ya kwanza, mwandishi anamuhoji kocha wa Yanga, Miguel Gamondi, ambaye anatoa maelezo kuhusu ushindi wa timu yake. Hata hivyo, mwandishi aliendelea kuuliza kuhusu goli moja, bila kuzingatia umuhimu wa pointi tatu.
Katika video ya pili, mwandishi wa maswali hayupo na anajikita tu katika majibu mazuri ya kocha wa "Panya Road" ambaye pia ameshinda. Kamwe alidai kuwa kuna ajenda inayofanywa ili kuonyesha kwamba ushindi wa Yanga ni dhambi, na anashangazwa na jinsi Azam TV inavyoshiriki katika ajenda hiyo. Alisisitiza kuwa mashabiki wanapaswa kuwalinda wachezaji na makocha wa Yanga katika wakati huu mgumu wa ushindani.
Hali hiyo ilimuibua Meneja wa Habari na Mawasiliano wa Klabu ya Simba, Ahmed Ally na kutoa kejeli kwa Watani zao kwa kuandika: Sasa hivi Azam Tv kabla hawajafanya Interview na Mwalimu wa Nyuma Mwiko wanatakiwa kupeleka Maswali kwa viongozi wa Nyuma Mwiko wakiyapenda ndio anaulizwa

Hivyo hivyo kwa idara ya Digitali ya Azam Tv kabla hawajaandika Caption wanatakiwa waitume kwa viongozi Nyuma Mwiko wakifurahishwa nayo ndio ipostiweeee
Screenshot 2024-10-01 122256.png
Je, Yanga ameshuka kiwango na sasa anatafuta visingizio au ndio Propaganda za soka la Tanzania?
 
YOUNG AFRICANS FOREVER! timu inaingia uwanjani kusaka pointi tatu tu! magoli ni extra mile,nafasi ikipatikana moja ya kufunga wanafunga. kikubwa 3points.
 
utafikiri hizo timu nyengine wao hawana mbinu,hawana wachezaji na hawana kocha!.
mbona yanga bado inatawala vyema nakuibuka na ushindi,timu nyingi wanachokifanya ni kupunguza idadi ya magoli tu ila wanajua kabisa watapigika!.
unacheza na timu dk 90 na hawajapata on target hata moja unafikiri walikuwa wanafanya nini kama si ku defence..?

msikariri na sio lazima kila siku yanga ishinde 5,wapinzani wowote sasahivi wakicheza na yanga wanakuwa makini mno wanajua nini kinaweza kuwakuta!.
 
Waache wajasahau waje kwa kujiamini tukabandike bango lingine.
 
Wataalam wa Sayansi ya mpira tujadiliane kidogo kuhusu hili linaloendelea mitandaoni

Tangu mechi ya kwanza ya Ligi Kuu, Yanga akiwa ugenini dhidi ya Kagera Sugar licha ya kushinda bao 2-0 bado kulizuka mijadala kuhusu kiwango chao, hata mechi zilizofuata (na CEB 1-0, Ken Gold 1-0 zote ugenini).

Mjadala ulikufa baada ya ushindi wa bao 6 kwa mtungi kwenye mechi ya marudio na CBE pale Zanzibar kwani ilionekana kama wamerudi kwenye utaratibu wao wa msimu uliopita 2023/24 wa kutembeza vipigo vikubwa na kutamba kwamba mashabiki wao washangilie angalau kuanzia bao la tatu na kuendelea.

Baada ya ushindi wa bao 1-0 dhidi ya KMC ambao msimu uliopita Wana-Kino boys walipigwa jumla ya bao 8 kwenye mechi mbili, (5-0 na 3-0) hali ilirudi baada ya msemaji wao Ally Kamwe alibuka na tuhuma kwa Azam Tv akidai kuwa Wanapaswa kutafakari kuhusu utoaji wa habari zao, akionyesha tofauti katika mahojiano ya makocha wawili. Katika video ya kwanza, mwandishi anamuhoji kocha wa Yanga, Miguel Gamondi, ambaye anatoa maelezo kuhusu ushindi wa timu yake. Hata hivyo, mwandishi aliendelea kuuliza kuhusu goli moja, bila kuzingatia umuhimu wa pointi tatu.
Katika video ya pili, mwandishi wa maswali hayupo na anajikita tu katika majibu mazuri ya kocha wa "Panya Road" ambaye pia ameshinda. Kamwe alidai kuwa kuna ajenda inayofanywa ili kuonyesha kwamba ushindi wa Yanga ni dhambi, na anashangazwa na jinsi Azam TV inavyoshiriki katika ajenda hiyo. Alisisitiza kuwa mashabiki wanapaswa kuwalinda wachezaji na makocha wa Yanga katika wakati huu mgumu wa ushindani.
Hali hiyo ilimuibua Meneja wa Habari na Mawasiliano wa Klabu ya Simba, Ahmed Ally na kutoa kejeli kwa Watani zao kwa kuandika: Sasa hivi Azam Tv kabla hawajafanya Interview na Mwalimu wa Nyuma Mwiko wanatakiwa kupeleka Maswali kwa viongozi wa Nyuma Mwiko wakiyapenda ndio anaulizwa

Hivyo hivyo kwa idara ya Digitali ya Azam Tv kabla hawajaandika Caption wanatakiwa waitume kwa viongozi Nyuma Mwiko wakifurahishwa nayo ndio ipostiweeee
Je, Yanga ameshuka kiwango na sasa anatafuta visingizio au ndio Propaganda za soka la Tanzania?
Yanga hawajashuka kiwango ila kuna mambo makuu mawili.
Moja ni kwamba Yanga ndiyo kipimo cha ubora wa soka la Tanzania kwa sasa. Fikiria timu inafungwa goli moja ama mbili halafu inashangilia huku mpinzani wake Simba akishangilia pia.
Pili ni kwamba huenda viwango vya timu zingine vimepandapanda mfano Simba alipigwa 5...2...1.
Tatu ni kwamba..........(Malizieni)
 
Back
Top Bottom