Bashiru na polepole hawana tena uwezo wa kuiokoa ccm isife.
Chama kimegawanyika vipande vipande kwa sababu ya watu hawa wawili. Hawakuwahi kuwa wana CCM kabisa, wamekuja wameleta aidia za kizamani kabisa wakidhani Watanzania wako stone age. Hawa wapo chamani kwa maslahi yao tu ya kupata pesa, wala si kufanya chama kisonge mbele hata kidogo.
Wale CCM asili Waliokipigania chama hawataki kabisa kuwasikia hawa watu, wamekuja kuvamia chama, na kujiona wao ni bora sana kuliko waliowakuta.
Hawa ndio walikuja na wazo la kununua wapinzani. Unanunuaje mtu mmoja, wakati alipigiwa kura na maelelfu, yaani unachukua mayai, unaacha kuku, kuku ataendelea kutaga, halafu unashangilia umemkomoa kuku.
Hawa ndio walimdanganya raisi awekeze mamiradi ya fedha nyingi kuwa ndiyo yatakayompigia kura, leo hatuuziki kabisa kwa wananchi, unamwambia mtu tumejenga fly over wakati yeye anakunywa tope.
Hawa ndiyo walimsapoti raisi wetu, azibe mdomo vyombo vya habari visitangaze habari za upinzani, iwe ni CCM tu, leo sisi tunatafuta raia waje kwenye mikutano tena kwa gharama kubwa, wakati wapinzani wetu, raia wanamtafuta kwa gaharama zao mgombea wao kujua hata yuko wapi.
Ndio waliomdanganya ya kwamba upinzani umekufa, wamekaa kinafiki kabisa, leo kwa ground tunapata shida mnoo mpaka lazima tuwalazimisha watumishi woote wa serikali na wanafunzi kuja kuongeza vichwa kwenye mikutano yetu.
Walimdanganya sana mkuu kwamba anakubalika na asijali sana kelele za watu, ona mpaka leo tunafikia hatua ya kupiga magoti kwa raia tuliowaambia watalimia meno.
Yako mengi sana ndugu zangu, lakini kwa kweli tuna hali ngumu, kama chama tukubali tumekosea na hawa watu wawili wamesababisha magawanyiko mkubwa sana chamani. Sasa hivi tupo CCM asili na CCM Mpya, hii CCM Mpya ni kikundi kidogo sana cha Bashiru, Polepole na wahamiaji toka upinzani, ambao hawajawahi kuwa wana CCM, na wamekuja kuchukua nafasi za CCM asili waliokipigania chama.
Hawa watu wawili wamesababisha mpaka sasa tume ya uchaguzi na polisi wanaanza kutumika vibaya ili kuokoa jahazi, wakati chama kilipaswa kiwe na nafasi nzuri sana ya kushinda mwaka huu.
Chama kimegawanyika vipande vipande kwa sababu ya watu hawa wawili. Hawakuwahi kuwa wana CCM kabisa, wamekuja wameleta aidia za kizamani kabisa wakidhani Watanzania wako stone age. Hawa wapo chamani kwa maslahi yao tu ya kupata pesa, wala si kufanya chama kisonge mbele hata kidogo.
Wale CCM asili Waliokipigania chama hawataki kabisa kuwasikia hawa watu, wamekuja kuvamia chama, na kujiona wao ni bora sana kuliko waliowakuta.
Hawa ndio walikuja na wazo la kununua wapinzani. Unanunuaje mtu mmoja, wakati alipigiwa kura na maelelfu, yaani unachukua mayai, unaacha kuku, kuku ataendelea kutaga, halafu unashangilia umemkomoa kuku.
Hawa ndio walimdanganya raisi awekeze mamiradi ya fedha nyingi kuwa ndiyo yatakayompigia kura, leo hatuuziki kabisa kwa wananchi, unamwambia mtu tumejenga fly over wakati yeye anakunywa tope.
Hawa ndiyo walimsapoti raisi wetu, azibe mdomo vyombo vya habari visitangaze habari za upinzani, iwe ni CCM tu, leo sisi tunatafuta raia waje kwenye mikutano tena kwa gharama kubwa, wakati wapinzani wetu, raia wanamtafuta kwa gaharama zao mgombea wao kujua hata yuko wapi.
Ndio waliomdanganya ya kwamba upinzani umekufa, wamekaa kinafiki kabisa, leo kwa ground tunapata shida mnoo mpaka lazima tuwalazimisha watumishi woote wa serikali na wanafunzi kuja kuongeza vichwa kwenye mikutano yetu.
Walimdanganya sana mkuu kwamba anakubalika na asijali sana kelele za watu, ona mpaka leo tunafikia hatua ya kupiga magoti kwa raia tuliowaambia watalimia meno.
Yako mengi sana ndugu zangu, lakini kwa kweli tuna hali ngumu, kama chama tukubali tumekosea na hawa watu wawili wamesababisha magawanyiko mkubwa sana chamani. Sasa hivi tupo CCM asili na CCM Mpya, hii CCM Mpya ni kikundi kidogo sana cha Bashiru, Polepole na wahamiaji toka upinzani, ambao hawajawahi kuwa wana CCM, na wamekuja kuchukua nafasi za CCM asili waliokipigania chama.
Hawa watu wawili wamesababisha mpaka sasa tume ya uchaguzi na polisi wanaanza kutumika vibaya ili kuokoa jahazi, wakati chama kilipaswa kiwe na nafasi nzuri sana ya kushinda mwaka huu.