Jeff Lea punguza Uinglishi tafadhari

Jeff Lea AKA Cassidy wakimuita hivyo wenzake,Ni kipaji halisi na anajua mambo hasa. Mambo anayajua na nilimtabiria angeenda mbali sema hakuwa serious wakati akiwa kwenye twenties.Kiswahili anakijua na kiingereza pia, mtoto wa Mikocheni.

Jina la cassidy lilitokana na kung'ata kimalkia enzi za green acres

Jeff lea enzi zake alikuwa anamwaga ung'eng'e balaa
 
Penati, winga, umiliki wa mpira, madhambi, kiungo inawezekana tu, tatizo ni kuwa watu wengi wanadhani ukichomeka maneno ya kizungu basi wewe level nyingine. wasikilizaji wa Tz lugha yetu kiswahili lazima tujivunie. Mimi huwa najitahidi sana nikiwa naongea na mtu niepuke kutia neno la kizungu lakini unaweza wakati mwingine ikatokea ila hili ni shida sio kwa Lea tu hata huku mitaani mtu akihojiwa basi kama kapata fursa, wapenzi wako waswahili ongea lugha watayo kuelewa.
 
Wachambuzi wa kileo bila kiingilishi hawaridhiki utasikia huyu Chama Ni playmaker, very powerful ana mark v one by one, anaattack mpira anacreate chances.
Kagere ni most dangerous stricker akiwa within 20m off the goal anaweza kushuti na kuscore goal at unexpected angle of the goal Ni very creative pia miguu na akili yake havisalitiani.
Daah all in all wanachambua mpaka unahisi game za ulaya kumbe Ni VPL​
 
Mkuu kuwa mchambuzi wa mpira ni mpaka usomee habari? ndo kwanza nasikia kwako...hapana bwana unatudanganya maana hata ulaya wachambuzi si lazima wasomee habari...nakataa
 
Jamani
 
Mpuuzi mkia huyo..amakariri vocabulary ngoja aongee sentensi grammar mbovu...
 
Ila anajua. Wanaume wa Tanzania wana tabia ya kuonea wivu wanaume wenzao
 
Sawa, mbona hayo yanaeleweka mkuu. Tatizo naloliona ni pale anapojikakamua hata kwenye maneno ya kawaida tu ya Kiswahili yeye atajiumauma kutamka Kiinglishi. Mpaka kipindi kinakosa mvuto na mfano jana mpaka nikatafuta Wasafi FM.
 
Binadamu tuna tofautiana ajabu mimi hua namuelewa sana tu
 
Mkuu, kwani dhumuni la kipindi ni nini? Kama ni kuhabarisha wasikilizaji wa hapa nchini basi ni lugha ya Kiswahili ndo ina watu wengi. Kwa taarifa yako radio hii inasikika mikoa mingi kwa watu wasiozungumza Kiinglishi. Pana radio hapa zinazotangaza Kiinglishi, aende huko.
 
Hasara kweli mkuu, ndo hao wanaotudanganya EPL inapendwa na watu wengi kumbe ni wao tu kushindwa kuyatamka majina ya timu za nchi nyingine.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…