Emanuel Eckson
Member
- May 24, 2017
- 11
- 14
Mahakama ya Wilaya ya Temeke imemuhukumu Mkazi wa Chamanzi, Said Wanie (35) kifungo cha maisha kwa kosa la kumlawiti mtoto wa kiume mwenye umri wa miaka tisa.
Pia mahakama hiyo imemuagiza mshtakiwa huyo kumlipa mtoto huyo fidia ya kiasi cha Sh500,000.
Kati ya Mei 3, 2020 maeneo ya Chamanzi Wilaya ya Temeke mshtakiwa huyo alimlawiti mtoto huyo huku akijua kufanya hivyo ni kosa la kisheria.
Akitoa hukumu hiyo Hakimu Mkazi, Anna Mpessa alisema mahakama hiyo imejiridhisha na ushahidi uliotolewa na mtoto mwenyewe pamoja na vielelezo vilivyotolewa na daktari vikionyesha kuwa mtoto huyo amelawitiwa.
Chanzo: Mwananchi
Pia mahakama hiyo imemuagiza mshtakiwa huyo kumlipa mtoto huyo fidia ya kiasi cha Sh500,000.
Kati ya Mei 3, 2020 maeneo ya Chamanzi Wilaya ya Temeke mshtakiwa huyo alimlawiti mtoto huyo huku akijua kufanya hivyo ni kosa la kisheria.
Akitoa hukumu hiyo Hakimu Mkazi, Anna Mpessa alisema mahakama hiyo imejiridhisha na ushahidi uliotolewa na mtoto mwenyewe pamoja na vielelezo vilivyotolewa na daktari vikionyesha kuwa mtoto huyo amelawitiwa.
Chanzo: Mwananchi